Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kushoto: Mwisho-mwisho wa miaka ya 1930, dada huyu katika Alabama, États-Unis, anamusikilizisha mutu huyu hotuba ya Ndugu Rutherford ambayo ilirekodiwa; kuume: Inchi ya Uswisi

SEHEMU YA KWANZA

Kweli ya Ufalme​—Kutolea Watu wa Mungu Chakula cha Kiroho

Kweli ya Ufalme​—Kutolea Watu wa Mungu Chakula cha Kiroho

FIKIRIA jambo hili: Unajifunza na mutu Biblia, munasoma andiko fulani, unamuona mara moja anafungua macho na anakuangalia kwa sababu anaelewa maana ya andiko hilo. Kwa sauti ya mushangao na ya upole anakuuliza, “Unamaanisha kweli kwamba Biblia inafundisha kama tunaweza kuishi milele katika paradiso​—hapa duniani?” Ndugu anayekusindikiza katika mahubiri anacheka kidogo na anamujibia hivi, “Tulia, unasoma nini katika Biblia?” Mwanafunzi anajaa na furaha, anatikisa kichwa na kusema, “Ni ajabu kabisa, hakuna siku nilifundishwa jambo hili!” Unakumbuka kwamba alisema pia maneno kama hayo kumekwisha pita majuma fulani, siku ile alijifunza kwa mara ya kwanza kwamba jina la Mungu ni Yehova.

Je, umekwisha kukutana na jambo kama hilo? Ndugu na dada wengi wamekwisha kukutana na jambo hilo. Kuna mambo machache ambayo yanaweza kutukumbusha zawadi ya maana sana ambayo tumepewa, ni kusema, ujuzi wa ile kweli! Kwa hiyo fikiri kidogo na ujiulize ni namna gani wewe ulifikia kujua ile kweli? Katika sehemu hii tutazungumuzia ulizo hilo. Namna watu wa Mungu walipata nuru ya kiroho hatua kwa hatua ni ushuhuda ulio wazi kwamba Ufalme wa Mungu ni jambo la kweli kabisa. Kwa miaka 100, Mufalme wa Ufalme huo, Yesu Kristo, amefanya yote ili watu wa Mungu wafundishwe ile kweli.

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 3

Yehova Anafunua Kusudi Lake

Ufalme ulikuwa katika kusudi la Mungu la kwanza? Namna gani Yesu alifunua kweli juu ya Ufalme?

SURA YA 4

Yehova Analitukuza Jina Lake

Ufalme umetimiza nini juu ya jina la Mungu? Unaweza kufanya nini ili kulitakasa jina la Yehova?

SURA YA 5

Mufalme Anafunua Kweli Mbalimbali Juu ya Ufalme

Soma ili uelewe vizuri juu ya Ufalme wa Mungu, juu ya wale ambao watatawala katika ufalme huo, juu ya wale ambao watakuwa raia, na mambo mutu anapaswa kufanya ili kuonyesha kwamba anashikamana na Ufalme.