Ona video zinazopatikana

Je, Mashahidi wa Yehova Wanalipa Wale Wanaowasimamia?

Je, Mashahidi wa Yehova Wanalipa Wale Wanaowasimamia?

 Mashahidi wa Yehova wanafuata mufano wa Wakristo wa kwanza, kati yao hakuna wakubwa na watu wa kawaida. Mashahidi wote wenye kubatizwa ni wafanyakazi waliowekwa na Mungu na wote wanahubiri na kufundisha. Wanapatikana katika makutaniko mbalimbali. Kila kutaniko lina Mashahidi karibu 100. Kila kutaniko lina wanaume wenye kukomaa kiroho wanaoitwa “wanaume wazee,” ao wazee. (Tito 1:5) Wazee hao hawalipwe.