Ona video zinazopatikana

Kiongozi Fulani wa Dini Anapata Majibu

Kiongozi Fulani wa Dini Anapata Majibu

 Siku moja, wakati Eliso, Shahidi wa Yehova, alikuwa anajifunza Biblia na mwanamuke mumoja mwenye kupendezwa, ule mwanamuke akapata wageni fulani bila kutazamia. Ilikuwa kiongozi fulani wa dini na bibi yake, na Eliso alikuwa amesikia kama mutoto wao mumoja tu alikuwa amekufa hivi karibuni.

 Wakati Eliso aliwaambia kama kifo cha mutoto wao kilimuhuzunisha, ule kiongozi wa dini na bibi yake wakaanza kulia sana. Kisha ule kiongozi wa dini akasema hivi kwa kasirani: “Sielewe juu ya nini Mungu aliruhusu ile jaribu ya vile itupate! Juu ya nini alichukua mutoto wangu moja tu? Nimetumikia Mungu kwa miaka 28, na niko nafanya mambo mingi ya muzuri, ona sasa vile ananilipa! Juu ya nini Mungu aliua mutoto wangu?”

 Eliso aliwafasiria kama haiko Mungu njo mwenye alichukua mutoto wao. Kisha akazungumuzia bei ya ukombozi, ufufuo, na sababu zenye zinafanya Mungu aruhusu mambo ya mubaya itokee. Ule kiongozi wa dini na bibi yake wakamuambia Eliso kama ametoka kuwapatia majibu yenye walikuwa wanamuomba Mungu.

 Juma yenye kufuata, ule kiongozi wa dini na bibi yake walirudia tena kwa ule mwanamuke juu walipenda wakuwe pale wakati Eliso iko anajifunza naye. Eliso na ule mwanamuke walikuwa wanajifunza sura yenye kichwa “Tumaini la Kweli juu ya Watu Tuliowapenda Waliokufa,” mu kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Ule kiongozi wa dini na bibi yake walishiriki mu ile mazungumuzo.

 Kisha wote wawili walienda ku mukusanyiko wa pekee wa Mashahidi wa Yehova yenye ilifanywa mu Tbilisi, mu inchi ya Georgia, na walitiwa moyo sana kuona namna Mashahidi wa Yehova wako na upendo na umoja wa nguvu sana. Kwa muda murefu walijikaza kusaidia watu wa dini yao wakuwe na zile sifa, lakini haikuwezekana.