Ona video zinazopatikana

Kusafiri Katika Muto Maroni

Kusafiri Katika Muto Maroni

 Kuko watu wa makabila, luga, na mataifa mbalimbali wenye wanaishi mu pori ya Amazoni katika Amerika ya Kusini, mbali sana na miji mikubwa yenye kuwa na watu wengi na fujo mingi. Kwa hiyo, Mwezi wa 7, 2017, Mashahidi 13 walifanya safari katika Muto Maroni na mito yake midogo yenye kuwa upande wa mashariki katika Guiana ya Ufaransa. Juu ya nini walifanya ile safari? Ili kuenda kuhubiria watu wenye kuishi mu maeneo yenye kuwa pembeni-pembeni ya ule muto.

Kujitayarisha kwa Ajili ya Safari

 Mwezi moja mbele ile safari yenye ilifanya siku 12 ianze, wote wenye wangeenda mu ile safari walikutana ili kupanga safari. Winsley anakumbuka hivi: “Tulijifunza juu ya eneo na historia yake, na tulizungumuzia pia namna ya kujitayarisha kwa ajili ya safari.” Kila ndugu na dada alipewa fasi ya kuwekea kitu fulani ya kulalia na mustikere. Mu ile safari tulisafiri kwa ndege mara mbili na tulisafiri saa mingi mu mitumbwi.

Claude na Lisette

 Wale wenye walichaguliwa ili kuenda mu ile safari walijisikia namna gani? Claude na Lisette, wenye kuwa na miaka 65 hivi walikubali bila kusita. Claude anasema hivi: “Nilifurahi sana, lakini niliogopa kidogo. Nilikuwa nimesikia kama mu Muto Maroni munakuwaka maporomoko hatari.” Lisette naye alikuwa na wasiwasi juu ya jambo lingine. Anasema hivi: “Nilijiuliza ikiwa nitaweza kuzungumuza luga za Kiamerindia.”

 Mickaël, mwenye naye alienda mu ile safari, alikuwa na wasiwasi. Anasema hivi: “Hatukujua mambo mingi juu ya kabila la Wayana. Kwa hiyo, nilitafuta habari ku Enternete ili nijifunze maneno fulani juu nijue namna ya kuwasalimia mu luga yao.”

 Shirley mwenye alisafiri pamoja na bwana yake Johann, alifanya liste ya luga zenye kuzungumuziwa na watu wenye kuishi karibu na Muto Maroni. Anasema hivi: “Tulikamata ku jw.org video katika luga mingi kati ya zile luga na tulipata kitabu chenye kuwa na maneno fulani yenye watu wa kabila la Wayana wanazoea kutumia.”

Kufika Katika Maeneo ya Waamerindia

 Tarehe 4 Mwezi wa 7, wale Mashahidi walipanda ndege katika muji wa Saint-Laurent du Maroni ili kuenda Maripasoula, muji mudogo wenye kuwa ndani kabisa ya Guiana ya Ufaransa.

 Siku ine zenye zilifuata walienda kuhubiria watu wenye wanaishi katika miji yenye kuwa pembeni-pembeni ya mito midogo-midogo yenye inashukia mu Muto Maroni, kwenye upande wake wa juu. Walikuwa wanasafikiri kwa kutumia mitumbwi ya motere. Roland, mwenye alikuwa pia mu ile safari anasema hivi: “Tuliona kama Waamerindia wanafurahia sana ujumbe wa Biblia. Wako na maulizo mingi, na wamoja kati yao walipenda tujifunze nao Biblia.”

 Mu kijiji kimoja, Johann na Shirley, walikutana na bibi na bwana vijana, wenye mutu wa jamaa yao alikuwa ametokea kujiua. Johann anasema hivi: “Ku JW Télédiffusion, tuliwaonyesha video yenye kichwa Muamerindia Anapata Muumbaji Wake.” Ile video iliwagusa moyo sana. Walitupatia adresi yao ya e-mail kwa sababu walipenda tuendelee kuzungumuza nao.”

 Kwenye upande wa juu wa Muto Maroni, sehemu ya mbali zaidi yenye walifika ni Antécume Pata. Kule, mukubwa wa kijiji alipatia wale Mashahidi wa Yehova, wenye walikuwa wamechoka, fasi ya kupumuzikia. Walinawia pia mu muto, sawa vile watu wa mu ile eneo wanafanyaka.

 Kisha kutoka pale, walienda mu kijiji cha Twenké, kwa kutumia mutumbwi. Kule walikuta watu wako mu kilio. Éric, mumoja kati ya wenye walipanga ile safari, anasema hivi: “Mukubwa wa kile kijiji, mwenye wanaitaka ‛Grand Man,’ alituruhusu tutembelee watu wa mu kile kijiji ili tufariji wenye walikuwa wamefisha. Ule mukubwa na familia yake walifurahia maandiko yenye tuliwasomea mu Biblia ya luga ya Wayana. Tuliwaonyesha pia video zenye kuonyesha ahadi ya Mungu ya kufufua wafu.”

Safari ya Kuenda Grand-Santi na Apatou

 Kisha pale, tulipanda ndege kutoka Maripasoula na kuenda katika muji mudogo wa Grand-Santi, wenye kuwa kwenye upande wa chini wa Muto Maroni. Siku ya Pili na ya Tatu, wale Mashahidi walihubiri watu wa mu ile eneo. Siku ya Ine, walifanya safari ingine ya saa tano na nusu katika Muto Maroni ili kuenda mu kijiji cha Apatou.

Muto Maroni na pori ya Amazoni kati ya Maripasoula na Grand-Santi

 Mbele ya siku ya mwisho ya ile safari, wale Mashahidi walitembelea vijiji vyenye kuwa katika pori vya Wamaroni, wenye kuwa wazao wa watumwa Waafrika wenye waliletwa katika Amerika ya Kusini wakati inchi jirani ya Suriname ilikuwa katika ukoloni. Mashihidi walialika watu ku mukutano mu pori kwenye walikuwa wamejenga hema kubwa kwa ajili ya ile tukio. Claude anasema hivi: “Tulifurahi sana kuona watu wengi wanakuja. Tuliwaalika tu ile asubui.” Karsten, mwenye ilikuwa mara yake ya kwanza kuenda mu maeneo ya vijiji, alitoa hotuba mu luga ya Aukan. Ile hotuba ilikuwa na kichwa “Hii Tu Njo Maisha?” Watu 91 kutoka mu vijiji mbalimbali walikuja ku ule mukutano.

“Tuko Tayari Kuenda Tena!”

 Ku mwisho, wale Mashahidi walirudia mu muji wa Saint-Laurent du Maroni. Wote walifurahi kuona namna watu wa ile maeneo walipendezwa. Walikubali vichapo mingi na waliangalia video mingi zenye kutolewa na Mashahidi wa Yehova.

 Lisette anasema hivi: “Ninakosa maneno ya kueleza furaha yenye niko nayo kwa sababu nilienda mu ile safari.” Cindy anakubaliana naye. Anasema hivi: “Kama ninapata nafasi ingine, nitaenda bila kusita. Ili mutu aelewe furaha yenye niko nayo, inaomba tu yeye mwenyewe aende kujionea!”

 Ile safari ilipatia ndugu na dada fulani hamu ya kurudia. Mickaël anasema hivi: “Tuko tayari kuenda tena kule!” Winsley alihamia katika muji wa Saint-Laurent du Maroni. Claude na Lisette, waliamua kuhamia Apatou.