Hamia kwenye habari

Je, Ibilisi Ndiye Anayesababisha Kuteseka Kote?

Je, Ibilisi Ndiye Anayesababisha Kuteseka Kote?

Jibu la Biblia

 Biblia inafunua kwamba Shetani Ibilisi ni kiumbe halisi wa roho ambaye kama tu kiongozi mwenye nguvu wa kikundi cha wahalifu, anajaribu kutimiza makusudi yake kupitia “ishara za uwongo” na “udanganyifu.” Kwa kweli, kama Biblia inavyosema, Shetani “huendelea kujigeuza mwenyewe kuwa malaika wa nuru.” (2 Wathesalonike 2:9, 10; 2 Wakorintho 11:14) Tunaweza kujua kwamba Ibilisi ni kiumbe halisi kutokana na mambo anayotenda.

 Hata hivyo, Ibilisi hasababishi kuteseka kote kwa wanadamu. Kwa nini? Mungu alimuumba wanadamu akiwa na uwezo wa kuchagua kufanya mema au mabaya. (Yoshua 24:15) Tunapofanya maamuzi mabaya, tunavuna matokeo mabaya.—Wagalatia 6:7, 8.