Hamia kwenye habari

Je, Mungu Ndiye wa Kulaumiwa Kwa Sababu ya Kuteseka Kwetu?

Je, Mungu Ndiye wa Kulaumiwa Kwa Sababu ya Kuteseka Kwetu?

Jibu la Biblia

 Biblia inajibu kwa mkazo la! Kuteseka hakukuwa sehemu ya kusudi la Yehova Mungu kwa wanadamu. Hata hivyo, wanadamu wawili wa kwanza walikataa utawala wa Mungu, wakachagua kujiwekea wenyewe viwango vya mema na mabaya. Walimwacha Mungu na wakapata matokeo mabaya.

 Leo, tunateseka kwa sababu ya uamuzi wao mbaya. Kwa hiyo, kuteseka kwa wanadamu hakutokani na Mungu.

 Biblia inasema: “Mtu akiwa chini ya jaribu, yeye asiseme: ‘Mungu ananijaribu.’ Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na mambo maovu wala yeye mwenyewe hamjaribu yeyote.” (Yakobo 1:13) Mtu yeyote anaweza kuteseka—hata watu walio na kibali cha Mungu.