Hamia kwenye habari

Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ikiwa Nina Ugonjwa wa Kudumu?

Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ikiwa Nina Ugonjwa wa Kudumu?

Jibu la Biblia

 Ndiyo. Mungu huwajali watumishi wake walio wagonjwa. Biblia inasema hivi kuhusu mtumishi mwaminifu: “Yehova mwenyewe atamtegemeza katika kitanda cha ugonjwa.” (Zaburi 41:3) Ikiwa una ugonjwa wa kudumu, hatua tatu zifuatazo zinaweza kukusaidia kukabiliana nao:

  1.   Sali ili upate nguvu za kuvumilia. Unaweza kupata “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote,” inayoweza kupunguza wasiwasi na kukutegemeza.​—Wafilipi 4:6, 7.

  2.   Uwe na mtazamo unaofaa. Biblia inasema: “Moyo wenye shangwe ni dawa nzuri, lakini roho iliyopondeka huikausha mifupa.” (Methali 17:22) Uwe mcheshi kwa kuwa hilo linaweza kuondoa huzuni na pia kuboresha afya yako.

  3.   Uwe na tumaini katika ahadi za wakati ujao. Tumaini imara linaweza kukusaidia uwe na shangwe licha ya magonjwa ya kudumu. (Waroma 12:12) Biblia ilitabiri wakati ambapo “hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’” (Isaya 33:24) Wakati huo Mungu ataponya magonjwa yote yenye kudumu ambayo hawezi kutibiwa na sayansi ya kisasa. Kwa mfano, Biblia inasema hivi kuhusu uzee: “Nyama yake na iwe laini kuliko wakati wa ujana; na arudi kwenye siku za nguvu za ujana wake.”​—Ayubu 33:25.

 Taarifa: Ingawa Mashahidi wa Yehova wanakubali msaada ambao Mungu huandaa, wao pia hutafuta matibabu ya magonjwa ya kudumu. (Marko 2:17) Hata hivyo, hatupendekezi matibabu yoyote hususa; kila mtu anapaswa kufanya uamuzi wake kuhusiana na matibabu.