Hamia kwenye habari

Je, Mungu Ni Nguvu Zisizo na Utu?

Je, Mungu Ni Nguvu Zisizo na Utu?

Jibu la Biblia

 Mungu ana nguvu zisizo na kifani katika ulimwengu wote. Kuhusu jinsi alivyoumba mabilioni ya nyota zisizohesabika, Biblia inasema hivi: “Inueni macho yenu juu, mwone. Ni nani ameviumba vitu hivi? Ni Yeye anayelileta jeshi lake kulingana na hesabu, ambaye [Mungu] zote anaziita kwa jina. Kutokana na wingi wa nguvu zenye msukumo, yeye pia akiwa hodari katika nguvu, hakuna hata moja kati ya hizo inayokosekana.”—Isaya 40:25, 26.

 Lakini Mungu si nguvu tu zenye uwezo mkubwa. Biblia inasema kwamba ana hisia, kama vile upendo na chuki. (Zaburi 11:5; Yohana 3:16) Pia, inafunua kwamba Mungu anaweza kufurahishwa au kukasirishwa na matendo ya wanadamu.—Zaburi 78:40, 41.