Kulingana na Mathayo 6:1-34

  • MAHUBIRI YA MLIMANI (1-34)

    • Msijionyeshe kuwa waadilifu (1-4)

    • Jinsi ya kusali (5-15)

      • Sala ya mfano (9-13)

    • Kufunga (16-18)

    • Hazina duniani na mbinguni (19-24)

    • Acheni kuhangaika (25-34)

      • Endeleeni kuutafuta kwanza Ufalme (33)

6  “Iweni waangalifu msionyeshe uadilifu wenu mbele ya watu ili wawaone;+ la sivyo hamtapata thawabu kutoka kwa Baba yenu aliye mbinguni.  Basi unapotoa zawadi za rehema,* usipige tarumbeta mbele yako kama wanavyofanya wanafiki katika masinagogi na barabarani, ili wasifiwe na watu. Kwa kweli ninawaambia, wanapata thawabu yao kikamili.  Lakini wewe, unapotoa zawadi za rehema, usiache mkono wako wa kushoto ujue kile ambacho mkono wako wa kulia unafanya,  ili utoe zawadi za rehema kwa siri. Naye Baba yako anayetazama akiwa mahali pa siri atakulipa.+  “Pia, mnaposali msifanye kama wanafiki,+ kwa maana wanapenda kusali wakiwa wamesimama katika masinagogi na kwenye kona za barabara kuu ili watu wawaone.+ Kwa kweli ninawaambia, wanapata thawabu yao kikamili.  Lakini unaposali, ingia ndani ya chumba chako faraghani, baada ya kufunga mlango wako, sali kwa Baba yako aliye mahali pa siri.+ Naye Baba yako anayetazama akiwa mahali pa siri atakulipa.  Mnaposali msiseme mambo yaleyale tena na tena, kama vile watu wa mataifa wanavyofanya, kwa maana wao hufikiri watasikiwa kwa kutumia maneno mengi.  Kwa hiyo, msiwe kama wao, kwa sababu Baba yenu anajua kile mnachohitaji+ hata kabla hamjamwomba.  “Basi, salini hivi:+ “‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako+ na litakaswe.*+ 10  Ufalme wako+ na uje. Mapenzi yako+ na yatendeke duniani+ kama ilivyo mbinguni. 11  Utupatie leo mkate wetu kwa ajili ya siku hii;+ 12  na utusamehe madeni yetu, kama vile tunavyowasamehe wadeni wetu.+ 13  Na usituingize katika majaribu,+ bali utukomboe* kutoka kwa yule mwovu.’+ 14  “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia;+ 15  lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe makosa yenu.+ 16  “Mnapofunga,+ msiwe na nyuso zenye huzuni kama wanafiki, kwa maana wao hukunja nyuso zao* ili watu waone kwamba wanafunga.+ Kwa kweli ninawaambia, wanapata thawabu yao kikamili. 17  Lakini wewe unapofunga, paka kichwa chako mafuta na unawe uso, 18  ili usionekane kwamba unafunga kwa wanadamu bali kwa Baba yako aliye mahali pa siri. Naye Baba yako anayeona akiwa mahali pa siri atakulipa. 19  “Acheni kujiwekea hazina duniani,+ ambako nondo* na kutu hula na ambako wezi huvunja na kuiba. 20  Badala yake, jiwekeeni hazina mbinguni,+ ambako hazitaliwa na nondo* wala kutu,+ na ambako wezi hawatavunja na kuiba. 21  Kwa maana mahali ilipo hazina yako, ndipo moyo wako utakapokuwa pia. 22  “Taa ya mwili ni jicho.+ Basi, ikiwa jicho lako linakazia jambo hususa,* mwili wako wote utakuwa mwangavu.* 23  Lakini ikiwa jicho lako lina wivu,*+ mwili wako wote utakuwa na giza. Ikiwa nuru iliyo ndani yako kwa kweli ni giza, basi giza hilo ni kubwa sana! 24  “Hakuna anayeweza kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine,+ au atashikamana na mmoja na kumdharau mwingine. Hamwezi kutumikia Mungu na Utajiri.+ 25  “Kwa hiyo ninawaambia: Acheni kuhangaikia+ uhai wenu* kuhusu kile mtakachokula au kunywa, au juu ya miili yenu kuhusu kile mtakachovaa.+ Je, uhai* si zaidi ya chakula na mwili zaidi ya mavazi?+ 26  Waangalieni kwa makini ndege wa angani;+ hawapandi mbegu, hawavuni, wala kukusanya ghalani, na bado Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wenye thamani kuliko wao? 27  Ni nani kati yenu ambaye kwa kuhangaika anaweza kurefusha uhai wake kwa mkono mmoja?*+ 28  Pia, kwa nini mnahangaika kuhusu mavazi? Jifunzeni kutoka kwa mayungiyungi* ya shambani, jinsi yanavyokua; hayafanyi kazi, wala hayasokoti; 29  lakini ninawaambia hata Sulemani+ katika utukufu wake wote hakupambwa kama maua hayo. 30  Basi, ikiwa Mungu huivika hivyo mimea ya shambani, ambayo ipo hapa leo na kesho hutupwa ndani ya jiko, je, hatawavika vizuri zaidi ninyi wenye imani ndogo? 31  Kwa hiyo msihangaike+ kamwe na kusema, ‘Tutakula nini?’ au, ‘Tutakunywa nini?’ au, ‘Tutavaa nini?’+ 32  Kwa maana mataifa yanatafuta vitu hivi vyote kwa bidii. Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivi vyote. 33  “Basi, endeleeni kuutafuta kwanza Ufalme na uadilifu wake,* nanyi mtaongezewa hivi vitu vingine vyote.+ 34  Basi, msihangaike kamwe kuhusu kesho,+ kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe. Kila siku ina matatizo yake ya kutosha.

Maelezo ya Chini

Au “unapowapa maskini zawadi.” Angalia Kamusi.
Au “litukuzwe; lionwe kuwa takatifu.”
Au “utuokoe.”
Au “hawatunzi sura au mwonekano wao.”
Aina ya wadudu.
Aina ya wadudu.
Au “linaona vizuri.” Tnn., “ni rahisi.”
Au “utajawa na nuru.”
Tnn., “ni bovu; lina uovu.”
Au “nafsi.”
Au “nafsi zenu.”
Aina ya maua.
Yaani, uadilifu wa Mungu.