Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Unaweza Kuwa na Hekima

Unaweza Kuwa na Hekima

“Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Timotheo 3:16) Katika mstari huu neno “limeongozwa” linamaanisha kwamba Mungu Mweza-Yote aliweka mawazo yake kwenye akili za waandishi wa Biblia.

Mungu Anakualika Unufaike na Hekima Yake

“Mimi, Yehova . . . ninayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, ninayekuongoza katika njia unayopaswa kutembea. Laiti ungesikiliza amri zangu! Ndipo amani yako ingekuwa kama mto na uadilifu wako kama mawimbi ya bahari.”​​—ISAYA 48:17, 18.

Ona maneno hayo kuwa mwaliko ambao Mungu anakupatia wewe binafsi. Anataka uwe na amani ya akili na moyoni na pia uwe na furaha ya kweli, na anaweza kukusaidia kupata mambo hayo.

Unaweza Kupata Hekima Kutoka kwa Mungu!

“Katika mataifa yote, lazima habari njema ihubiriwe.”​​—MARKO 13:10.

“Habari njema” inatia ndani ahadi za Yehova za kukomesha kuteseka, kufanya dunia iwe paradiso, na kuwafufua wapendwa wetu waliokufa. Mashahidi wa Yehova wanahubiri ujumbe wa Biblia duniani pote.