Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HABARI KUU | JINSI YA KUSITAWISHA MAZOEA MAZURI

3 Usikate Tamaa

3 Usikate Tamaa

Inasemekana kwamba mtu anaweza kuzoea tabia mpya kwa siku 21. Hata hivyo, utafiti unaonyesha kwamba huenda baadhi ya watu wakatumia muda mfupi kuzoea jambo fulani ilhali wengine wakatumia muda mrefu. Je, hilo linapaswa kukuvunja moyo?

Hebu fikiria hali hii: Tuseme kwamba unataka kusitawisha mazoea ya kufanya mazoezi mara tatu kwa juma.

  • Juma la kwanza, unafaulu kufikia lengo lako.

  • Juma la pili, unakosa kufanya mazoezi kwa siku moja.

  • Juma la tatu, unafaulu tena.

  • Juma la nne, unashindwa kufanya mazoezi hata kwa siku moja.

  • Juma la tano, unafaulu tena, na kuanzia hapo unatimiza lengo lako kila juma.

Imechukua majuma matano kuzoea hali hiyo mpya. Huenda huo ukaonekana kuwa muda mrefu, hata hivyo, mara tu unapofikia lengo lako unafurahi kwamba ulisitawisha zoea zuri.

KANUNI YA BIBLIA: “Huenda mwadilifu akaanguka hata mara saba, naye hakika atasimama.”Methali 24:16.

Biblia inatutia moyo tusikate tamaa. Haijalishi tutashindwa mara ngapi lakini jambo la maana ni kufikia malengo yetu.

Haijalishi tutashindwa mara ngapi lakini jambo la maana ni kufikia malengo yetu

MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

  • Kumbuka kwamba kuteleza si kuanguka. Tarajia kupata vizuizi unapojitahidi kufikia malengo yako.

  • Kumbuka wakati ulipofikia malengo yako. Kwa mfano, ikiwa unajaribu kuboresha njia ya kuwasiliana na watoto wako, jiulize hivi: ‘Ni wakati gani nilipotaka kuwafokea watoto wangu lakini nikajizuia kufanya hivyo? Nilifanya nini? Ninawezaje kufanya hivyo tena?’ Maswali kama hayo yanaweza kukusaidia uimarishe azimio lako la kutaka kufanikiwa badala ya kukazia fikira makosa.

Je, ungependa kujua jinsi ambavyo kanuni za Biblia zinaweza kukusaidia kushughulikia mambo mengine maishani kama vile, mahangaiko, kuwa na maisha ya familia yenye furaha na jinsi ya kuwa na furaha ya kweli? Zungumza na Mashahidi wa Yehova, au tembelea tovuti yetu ya jw.org/sw.