Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Ndoa Yenu Inaweza Kuokolewa?

Je, Ndoa Yenu Inaweza Kuokolewa?

Wenye nyumba wanakubali kwamba nyumba yao iko katika hali mbaya, lakini wameamua kuirekebisha.

JE, MNGEPENDA kufanya vivyo hivyo katika ndoa yenu? Ikiwa ndivyo, mtaanzia wapi? Jaribuni kufuata madokezo yafuatayo.

 1 Azimieni.

Kubaliana na mwenzi wako kwamba mtashirikiana kufanya ndoa yenu iwe na amani tena. Andikeni maamuzi yenu. Nyote wawili mnapowajibika, mtashirikiana kuiokoa ndoa yenu.—Mhubiri 4:9, 10.

 2 Tambueni tatizo.

Ni nini kimesababisha matatizo katika ndoa yenu? Kwa maneno machache, andikeni jambo mnalofikiri limekosekana katika ndoa yenu au jambo ambalo mnataka libadilike. (Waefeso 4:22-24) Inaeleweka kwamba huenda wewe na mwenzi wako mtaandika matatizo tofauti.

 3 Wekeni mradi.

Mngependa kuona mabadiliko gani hususa katika ndoa yenu miezi sita ijayo? Andikeni mradi wenu. Mkijua ni mambo gani hususa mngependa katika ndoa yenu, itakuwa rahisi zaidi kufikia mradi wenu.—1 Wakorintho 9:26.

  4 Fuateni mashauri ya Biblia.

Baada ya kutambua tatizo na kuamua njia hususa ya kulirekebisha, tafuteni mashauri kutoka katika Biblia. Kanuni zake hazichakai, nazo huwa na manufaa sikuzote. (Isaya 48:17; 2 Timotheo 3:17) Kwa mfano, Biblia inakutia moyo wewe na mwenzi wako muwe tayari kusameheana. Kwa kweli, Biblia inasema kwamba ‘ni jambo lenye kupendeza kupita kosa.’—Methali 19:11; Waefeso 4:32.

Hata ingawa mwanzoni huenda jitihada zako zikaonekana kuwa za bure, usikate tamaa! Kitabu The Case for Marriage kinataja matokeo yenye kutia moyo ya uchunguzi mmoja kinaposema hivi: “Matokeo ni yenye kushangaza: asilimia 86 ya wenzi ambao wanaendelea kuishi pamoja licha ya ndoa yao kukosa furaha hugundua kwamba miaka mitano baadaye, ndoa yao huwa na furaha zaidi.” Hata wenzi wa ndoa ambao walisema kwamba hawakuwa na furaha kabisa walipata matokeo kama hayo.

Huenda ikawa hivyo kwa ndoa yako. Mashahidi wa Yehova ambao ndio wachapishaji wa gazeti hili, wamegundua kwamba Biblia ina kanuni zinazowafaidi wenzi wa ndoa. Kwa mfano, ndoa nyingi huwa bora wenzi wanapokuwa wenye fadhili, wenye huruma nyororo, na wanaposameheana kwa hiari. Wake wamejifunza umuhimu wa kuwa na “roho ya utulivu na ya upole,” na waume wameona faida za kutowakasirikia wake zao kwa uchungu.—1 Petro 3:4; Wakolosai 3:19.

Kanuni hizo za Kimaandiko hufanya kazi kwa sababu Mtungaji wa Biblia, Yehova Mungu, ndiye aliyeanzisha mpango wa ndoa. Mbona usiwaombe Mashahidi wa Yehova habari zaidi kuhusu jinsi ambavyo Biblia inaweza kusaidia ndoa yako? *

^ fu. 14 Ili kusaidia familia, Mashahidi wa Yehova wamechapisha kitabu chenye kurasa 192 kilicho na kichwa Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Kwa habari zaidi, waandikie barua wachapishaji wa gazeti hili kwa kutumia anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.