Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Je, Ulikuwa Uamuzi Mzuri?

Soma Hesabu 13:1, 2, 25-33; 14:3, 6-12. Sasa tazama picha, na uandike majibu yako kwenye mistari iliyo hapo chini.

1. Kwa nini wengi wa wapelelezi waliamua kuleta ripoti mbaya?

․․․․․

2. Ripoti mbaya ya wale wapelelezi kumi ilikuwa na matokeo gani?

DOKEZO: Soma Hesabu 14:26-38.

․․․․․

3. Kwa nini Yoshua na Kalebu walikuwa na uhakika kwamba watapata ushindi?

․․․․․

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Familia yenu inapokabili hali ngumu, mnaweza kuepuka jinsi gani kuwa kama wale wapelelezi kumi na badala yake muwe kama Yoshua na Kalebu?

UNAJUA NINI KUHUSU MTUME PETRO?

4. Petro anatajwa kwa majina gani matano katika Biblia?

DOKEZO: Soma Mathayo 10:2; 16:16; Yohana 1:42; Matendo 15:14.

․․․․․

5. Je, Petro aliwahi kuoa?

DOKEZO: Soma 1 Wakorintho 9:5.

․․․․․

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Eleza simulizi moja kumhusu Petro ambalo unapenda. Ungetaka kuiga sifa gani za Petro, na unaweza kufanya hivyo jinsi gani?

WATOTO WATAFUTE PICHA

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

KATIKA TOLEO HILI

Jibu maswali haya, na utaje mistari ya Biblia ambayo haijaonyeshwa.

UKURASA WA 7 Tunapaswa kusema nini na jirani zetu? Waefeso 4:________

UKURASA WA 8 Kweli inaweza kukusaidia jinsi gani? Yohana 8:________

UKURASA WA 11 Ni nini kitakachompata adui wa mwisho? 1 Wakorintho 15:________

UKURASA WA 24 Unapaswa kukimbia nini? 1 Wakorintho 6:________

● Majibu kwenye ukurasa wa 13

MAJIBU YA UKURASA WA 31

1. Walikubali kushindwa na woga na walikosa imani katika Yehova.—Hesabu 14:3, 11.

2. Wanaume wote wenye umri wa miaka 20 na kuendelea isipokuwa Yoshua na Kalebu walikufa nyikani.

3. Walikuwa na imani kwamba Yehova alikuwa pamoja nao.—Hesabu 14:9.

4. Simoni, Petro, Simoni Petro, Kefa, na Simioni.

5. Ndiyo.