Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Muumba Wetu Mwenye Upendo Anatujali

Muumba Wetu Mwenye Upendo Anatujali

1. MUUMBA WETU HUFANYA JUA LIANGAZE

Je, unafikiri ingewezekana kuishi duniani bila mwanga wa jua? Jua hutoa nishati ambayo husaidia miti kutokeza majani, maua, matunda, kokwa, na mbegu. Pia, husaidia mizizi ya miti kufyonza maji kutoka kwenye ardhi, kupeleka kwenye majani na kisha maji hayo hugeuka kuwa mvuke.

2. MUUMBA WETU HUFANYA MVUA INYESHE

Mvua ni zawadi bora kutoka kwa Mungu ambayo huwezesha dunia kuzalisha chakula kwa ajili yetu. Mungu hutupatia mvua kutoka mbinguni na majira ya mavuno, akitushibisha kwa chakula na kuijaza mioyo yetu furaha.

3. MUUMBA WETU HUTUANDALIA CHAKULA NA MAVAZI

Mara nyingi, akina baba huhangaika sana ili kupata chakula cha kutosha na mavazi kwa ajili ya familia zao. Maandiko yanasema hivi: “Waangalieni kwa makini ndege wa angani; hawapandi mbegu, hawavuni, wala kukusanya ghalani, na bado Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wenye thamani kuliko wao?”—Mathayo 6:25, 26.

“Jifunzeni kutoka kwa mayungiyungi ya shambani, jinsi yanavyokua . . . ; lakini ninawaambia hata [Mfalme] Sulemani katika utukufu wake wote hakupambwa kama maua hayo. Basi, ikiwa Mungu huivika hivyo mimea ya shambani . . . , je, hatawavika vizuri zaidi?”—Mathayo 6:28-30.

Kwa kuwa Mungu ana uwezo wa kutuandalia chakula na mavazi, bila shaka atatusaidia kupata mahitaji mengine maishani. Ikiwa tutajitahidi kufanya mapenzi ya Mungu, atabariki jitihada zetu za kuzalisha chakula, au atatusaidia kupata kazi ambayo itatuwezesha kupata mahitaji yetu.—Mathayo 6:32, 33.

Kwa kweli, tuna sababu nzuri za kumpenda Mungu tunapochunguza jua, mvua, ndege wa angani na maua. Makala inayofuata itazungumzia jinsi Muumba wetu anavyowasilisha ujumbe wake kwa wanadamu.