Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HABARI KUU | MALAIKA​—JE, WANAHUSIKA KATIKA MAISHA YAKO?

Je, Una Malaika Anayekulinda?

Je, Una Malaika Anayekulinda?

Biblia haifundishi kwamba kila mtu ana malaika wake anayemlinda. Ni kweli kwamba Yesu aliwahi kusema: “Angalieni msimdharau mmoja wa hawa wadogo [wanafunzi wa Kristo]; kwa maana ninawaambia ninyi kwamba malaika zao mbinguni sikuzote huuona uso wa Baba yangu aliye mbinguni.” (Mathayo 18:10) Hata hivyo, badala ya kumaanisha kwamba kila mtu ana malaika anayemlinda, Yesu alimaanisha kuwa malaika wanamhangaikia kila mwanafunzi wake. Hivyo, waabudu wa kweli hawafanyi maamuzi yasiyo ya hekima au kujihatarisha, huku wakidhani kwamba malaika wa Mungu watawalinda.

Je, hilo linamaanisha kwamba malaika hawawasaidii wanadamu? Jibu ni hapana. (Zaburi 91:11) Baadhi ya watu wanaamini kabisa kwamba Mungu amewalinda na kuwaongoza kupitia malaika. Kenneth aliyetajwa katika makala ya kwanza, ni mmoja wa wale wanaoamini hivyo. Huenda yuko sahihi. Mara nyingi, Mashahidi wa Yehova wameona mambo yanayothibitisha kwamba malaika wanaunga mkono kazi yao ya kuhubiri. Hata hivyo, kwa kuwa malaika hawaonekani, hatuwezi kusema kwa usahihi Mungu anawatumia kwa kadiri gani kuwasaidia watu katika mambo mbalimbali. Lakini, si kosa kumshukuru Mweza Yote kwa kila msaada anaotuandalia.—Wakolosai 3:15; Yakobo 1:17, 18.