Majibu ya Maswali ya Biblia
Yesu atafanya nini wakati ujao?
Katika mwaka wa 33 W.K., Yesu alikufa, akafufuliwa, kisha akarudi mbinguni. Baadaye, Yesu alipewa mamlaka ya kutawala akiwa Mfalme. (Danieli 7:13, 14) Wakati ujao, Yesu atachukua hatua akiwa Mfalme kuleta amani duniani na kuondoa umaskini.
Akiwa Mfalme, Yesu ataondoa uovu wote duniani
Yesu atafanya mambo ya kustaajabisha akiwa Mtawala wa wanadamu. Atatumia nguvu ambazo amepewa na Baba yake kuwarudishia wanadamu ukamilifu. Watafurahia kuishi duniani bila kuzeeka wala kufa.
Yesu anafanya nini sasa?
Sasa Yesu anaongoza kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote inayofanywa na wafuasi wake wa kweli. Wanawatembelea watu ili kuwaambia mambo ambayo Biblia inasema kuhusu Ufalme wa Mungu. Yesu alisema kwamba ataendelea kutegemeza kazi ya wanafunzi wake mpaka Ufalme wa Mungu utakapokomesha serikali za wanadamu.
Kupitia kutaniko la kweli la Kikristo, Yesu anawasaidia watu kuishi maisha bora. Ataendelea kuwaongoza wakati wa kuharibiwa kwa mfumo wa sasa wa mambo na kuingia kwenye ulimwengu mpya ulioahidiwa na Mungu.