Hamia kwenye habari

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Wamebadili Baadhi ya Imani Zao?

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Wamebadili Baadhi ya Imani Zao?

 Sikuzote tumetumia Biblia kuwa msingi pekee wa imani zetu, kwa hiyo tumebadili imani zetu kadiri ambavyo uelewaji wetu wa Maandiko umeboreshwa. *

 Mabadiliko hayo yanapatana na kanuni ya Biblia inayopatikana kwenye Methali 4:18: “Njia ya waadilifu ni kama nuru inayong’aa, inayozidi kuongezeka mpaka mchana mkamilifu.” Kama tu jua linapochomoza linavyoangaza eneo fulani hatua kwa hatua, Mungu anatupa uelewaji wa kweli ya neno la Mungu hatua kwa hatua, kwa wakati wake mwenyewe. (1 Petro 1:10-12) Kama Biblia ilivyotabiri, ameharakisha jambo hilo katika ‘wakati huu wa mwisho.’​—Danieli 12:4.

 Mabadiliko hayo katika uelewaji wetu hayapaswi kutushangaza wala kutusumbua. Waabudu wa Mungu katika nyakati za kale walikuwa pia na maoni na matarajio yasiyofaa na walihitaji kubadili maoni yao.

 Baadaye Mungu alisahihisha maoni yao, na tunasali kwamba ataendelea kutufanyia vivyo hivyo.​—Yakobo 1:5.

^ Hatujaribu kuficha mabadiliko hayo katika uelewaji wetu wa Biblia. Hata tunayaandika na kuyachapisha. Kwa mfano, angalia habari zilizo chini ya kichwa kidogo “Uelewaji wa Mafundisho Uliorekebishwa” kwenye sehemu yenye kichwa “Mashahidi wa Yehova” katika machapisho yetu mtandaoni