Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Huwakataza Wafuasi Wao Sinema, Vitabu, au Nyimbo Fulani?

Je, Mashahidi wa Yehova Huwakataza Wafuasi Wao Sinema, Vitabu, au Nyimbo Fulani?

 Hapana. Tengenezo letu halikagui sinema, vitabu, au nyimbo fulani ili kuona ni zipi ambazo wafuasi wetu wanapaswa kuepuka. Kwa nini halifanyi hivyo?

  Biblia inamtia moyo kila mtu azoeze ‘nguvu zake za ufahamu’ kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa.—Waebrania 5:14.

  Maandiko yana kanuni za msingi ambazo Mkristo anaweza kutumia anapochagua burudani. * Katika sehemu zote za maisha, lengo letu ni ‘kuendelea kuhakikisha lile linalokubalika kwa Bwana.’​—Waefeso 5:10.

  Biblia inafundisha kwamba vichwa vya familia wana mamlaka kwa kiasi fulani, kwa hiyo wanaweza kuamua kutoruhusu burudani fulani katika familia zao. (1 Wakorintho 11:3; Waefeso 6:1-4) Hata hivyo, nje ya familia, hakuna mtu yeyote aliye na mamlaka ya kukataza watu kutanikoni kutazama sinema fulani, kusikiliza nyimbo, au kupenda wasanii fulani kwa kuwa anaona hazifai.​—Wagalatia 6:5.

^ Kwa mfano, Biblia inashutumu kitu chochote kinachowachochea watu wajihusishe na kuwasiliana na pepo, mwenendo mchafu kingono, au jeuri.​—Kumbukumbu la Torati 18:10-13; Waefeso 5:3; Wakolosai 3:8.