Hamia kwenye habari

Kazi ya Mashahidi wa Yehova Inagharimiwaje?

Kazi ya Mashahidi wa Yehova Inagharimiwaje?

 Kazi yetu ya ulimwenguni pote inategemezwa na michango ya hiari ya watu ambao ni Mashahidi wa Yehova. * Wanaweka michango yao kwenye masanduku ya michango inayopatikana kwenye maeneo tunayokutanikia, na kupitia njia nyingine zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa Michango. Kuna njia tofauti-tofauti zinazomwezesha mtu kutoa mchango kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote, gharama za eneo lake au mambo yote mawili.

 Mashahidi wa Yehova hawatazamiwi kutoa fungu la kumi au kiasi fulani maalumu au kiwango hususa cha kipato chao. (2 Wakorintho 9:7) Hatukusanyi sadaka kamwe wala kutoza kiingilio katika mikutano yetu, wahudumu wetu hawatozi fedha za ubatizo, mazishi, harusi, au kwa ajili ya huduma nyingine zozote za kidini. Hatutafuti fedha kupitia utendaji mbalimbali wa kukusanya fedha kama vile kuandaa masoko au michezo ya bahati nasibu, na pia hatuombi-ombi misaada. Habari za yule anayetoa mchango hazitangazwi kamwe. (Mathayo 6:2-4) Machapisho na tovuti zetu hazina matangazo yanayotuingizia fedha.

 Kila mwezi makutaniko ya Mashahidi wa Yehova hutoa ripoti wakati wa mikutano ya jinsi gharama zilivyoshughulikiwa, na watu wote wanaweza kuhudhuria mikutano hiyo. Rekodi za kila kutaniko hufanyiwa ukaguzi mara kwa mara ili kuhakikisha kwamba michango iliyotolewa inashughulikiwa kwa njia nzuri.—2 Wakorintho 8:20, 21.

Njia za kuchangia

  •   Masanduku ya Michango: Unaweza kuweka mchango wa fedha taslimu au cheki za benki kwenye masanduku ya michango katika Majumba ya Ufalme, Majumba ya Kusanyiko, au katika maeneo mengine ambapo mikutano yetu hufanyiwa.

  •   Michango Kupitia Mtandao: Katika nchi nyingi, unaweza kwenda kwenye ukurasa wa “Changia Mashahidi wa Yehova” ili kutoa mchango kupitia kadi za benki, kuhamisha pesa kutoka benki moja hadi nyingine, na njia zingine za kuchangia kwa njia ya kielektroni. * Baadhi ya Mashahidi wamefanya mpango wa “kuweka kando kitu fulani” kila mwezi kwa kutumia moja kati ya mbinu hizi.—1 Wakorintho 16:2.

  •   Utoaji uliopangwa: Njia fulani za kuchangia zinahitaji mtu apange mapema au hata aombe ushauri wa kisheria. Kwa kufanya hivyo, huenda ukapunguziwa kodi nchini kwenu. Watu wengi wamefaidika kujua kwamba wanaweza kutoa zawadi wakiwa hai au baada ya kufa. Tafadhali piga simu kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova iliyo katika eneo lenu ikiwa unataka kutoa mchango wa:

    •   akaunti ya benki

    •   bima na malipo ya kustaafu

    •   ardhi na nyumba

    •   hisa na dhamana

    •   wosia na amana

 Ili upate habari zaidi kuhusu njia za kutoa michango katika eneo lenu, ona ukurasa wenye kichwa “Changia Mashahidi wa Yehova.”

^ Watu fulani ambao si Mashahidi wanapenda pia kutoa mchango ili kuunga mkono kazi yetu.

^ Ili kujua mengi zaidi, ona video yenye kichwa Mwongozo wa Kutoa Michango Kielektroni.