Ona video zinazopatikana

Dunia Itaharibiwa?

Dunia Itaharibiwa?

Jibu ya Biblia

 Hapana, Dunia haitaharibiwaka, haitalunguziwaka, ao kubadilishwa na planete ingine hata siku moya. Biblia inafundisha kama Mungu aliiumba dunia juu iikaliwe milele.

  •   “Wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.”​—Zaburi 37:29.

  •   “[Mungu] ameweka dunia imara juu ya misingi yake; haitahamishwa kutoka mahali pake milele na milele.”​—Zaburi 104:5.

  •   “Dunia inadumu milele.”​—Muhubiri 1:4.

  •   “Mwenye alifanya dunia, Mutengenezaji wake mwenye aliifanya imara kabisa, . . . hakuiumba tu bila sababu, lakini aliifanya ili ikaliwe na watu.”​—Isaya 45:18.

Wanadamu wataharibu dunia?

 Mungu hataruhusu wanadamu waharibu kabisa dunia kupitia uchafu, vita, ao njia ingine yoyote. Lakini, ‘atawaharibu wale wenye wanaharibu dunia.’ (Ufunuo 11:18) Atafanya vile namna gani?

 Mungu atatosha serikali ao guvernema za wanadamu kwa sababu zimeshindwa kulinda dunia, na kisha atatia Ufalme wa mbinguni wenye kuwa mukamilifu. (Danieli 2:44; Matayo 6:9, 10) Ule Ufalme utatawaliwa na Mwana wa Mungu, Yesu Kristo. (Isaya 9:6, 7) Wakati Yesu alikuwa ku dunia alifanya miujiza ya kutuliza hata nguvu za asili. (Marko 4:35-41) Mu siku zenye ziko nakuya atatawala juu ya dunia yote na ataongoza muzuri nguvu za asili za dunia. Ataleta mambo ya mupya ku dunia, na kufanya hali ya dunia ikuwe tena sawa vile ilikuwa mu bustani ya Edeni.​—Matayo 19:28; Luka 23:43.

Biblia haifundishe kama dunia italunguziwa?

 Hapana, haifundishe vile. Watu wanakuwa na ile maoni yenye haiko ya kweli juu ya kuelewa mubaya andiko ya 2 Petro 3:7, yenye inasema: “Mbingu zenye ziko sasa na dunia yenye iko sasa vimewekwa pembeni kwa ajili ya moto.” Ona hii mambo mbili ya lazima yenye inatusaidia tuelewe ile maneno:

  1.   Biblia inatumia maneno “mbingu,” “dunia,” na “moto” juu ya kumaanisha mambo mingi. Kwa mufano, Mwanzo 11:1 inasema hivi: “Dunia yote iliendelea kuwa na luga moja.” Mu ile mustari, “dunia” inamaanisha watu.

  2.   Habari yenye kuzungumuziwa katika sura ya 3 ya Petro wa 2, inaonyesha maana ya mbingu, dunia, na moto vyenye kutajwa mu mustari wa 7. Mistari ya 5 na 6 inaonyesha mambo yenye kufanana na ile ya Garika ya siku za Noa. Ile wakati, ulimwengu wa zamani uliharibiwa, lakini planete yetu haikupotea. Garika ilifutilia mbali watu, ao “dunia,” yenye ilikuwa imejaa mambo ya mubaya sana. (Mwanzo 6:11) Tena, iliharibu aina fulani ya “mbingu”​—watu wenye walitawala ile wakati. Kwa hiyo ni watu wabaya njo waliharibiwa, hapana planete yetu. Noa na familia yake waliokoka na wakaendelea kuishi ku dunia kisha Garika.​—Mwanzo 8:15-18.

 Vile tu ile maji ya Garika ilifanya, uharibifu, ao “moto,” yenye kutajwa mu 2 Petro 3:7 utaleta mwisho wa watu wabaya, hapana mwisho wa hii dunia. Mungu anaahidi kama kutakuwa “mbingu mupya na dunia mupya, na mule haki itakaa.” (2 Petro 3:13) “Dunia mupya,” ao jamii mupya ya watu, itatawaliwa na “mbingu mupya,” ao utawala mupya, ni kusema, Ufalme wa Mungu. Ile wakati, dunia itakuwa paradiso yenye amani.​—Ufunuo 21:1-4.