Ona video zinazopatikana

Sababu Gani Tunapaswa Kusali Katika Jina la Yesu?

Sababu Gani Tunapaswa Kusali Katika Jina la Yesu?

Jibu la Biblia

 Tunapaswa kusali katika jina la Yesu kwa sababu hiyo ndiyo njia pekee ambayo Mungu amekubali tutumie ili tumukaribie. Yesu alisema hivi: “Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu.” (Yohana 14:6) Yesu aliwaambia pia mitume wake waaminifu hivi: ‘Kwa kweli kabisa ninawaambia, Mukimuomba Baba jambo lolote atawapa katika jina langu.’—Yohana 16:23.

Sababu zingine zinazotuchochea tusali katika jina la Yesu

  •   Tunamuheshimu Yesu na Baba yake, Yehova Mungu.—Wafilipi 2:9-11.

  •   Tunaonyesha kwamba tunakubali kifo cha Yesu kuwa mupango ambao Mungu alifanya ili tuokolewe.—Mathayo 20:28; Matendo 4:12.

  •   Tunakubali kwamba Yesu pekee ndiye Mupatanishi kati ya Mungu na wanadamu.—Waebrania 7:25.

  •   Tunaheshimu Yesu kuwa Kuhani Mukubwa anayeweza kutusaidia tuwe na uhusiano muzuri pamoja na Mungu.—Waebrania 4:14-16.