Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tunapaswa Kusali kwa Yesu?

Tunapaswa Kusali kwa Yesu?

MUCHUNGUZI mumoja alifanya uchunguzi hivi karibuni juu ya vijana zaidi ya 800 wa dini zaidi ya kumi na mbili. Aliwauliza ikiwa wanaamini kuwa Yesu anajibia sala. Vijana zaidi ya 60 juu ya 100 walisema kama wanaamini kabisa kuwa Yesu anajibia sala. Lakini, kijana mumoja alifuta jina Yesu kwenye karatasi ya uchunguzi na kuandika “Mungu” nafasi hiyo.

Unawaza namna gani? Tunapaswa kusali kwa Yesu ao kwa Mungu? * Ili kupata jibu, kwanza acha tuchunguze namna Yesu alifundisha wanafunzi wake kusali.

YESU ALITUFUNDISHA TUSALI KWA NANI?

Yesu alitufundisha na kutuonyesha tunapaswa kusali kwa nani.

Kwa kusali kwa Baba yake wa mbinguni, Yesu alituachia mufano tunaopaswa kufuata

MAFUNDISHO YAKE: Wakati fulani mwanafunzi mumoja alimuambia Yesu hivi: “Bwana, tufundishe jinsi ya kusali.” Yesu alimujibia hivi: ‘Wakati wowote munaposali, museme, Baba.’ (Luka 11:1, 2) Tena, katika Mahubiri yake ya Mulimani yenye kujulikana sana, Yesu aliwatia moyo wasikilizaji wake wakuwe wanasali. Aliwaambia hivi: ‘Musali kwa Baba yenu.’ Aliwatia moyo pia kwa kusema hivi: ‘Baba yenu anajua ni vitu gani munahitaji hata kabla hamujamuomba.’ (Mathayo 6:6, 8) Katika usiku wake wa mwisho akiwa mwanadamu, Yesu aliwaambia wafuasi wake hivi: ‘Mukimuomba Baba jambo lolote atawapa katika jina langu.’ (Yohana 16:23) Kwa hiyo, Yesu alitufundisha kusali kwa Yehova Mungu, aliye Baba yake na Baba yetu pia.—Yohana 20:17.

MUFANO WAKE: Kulingana na namna alifundisha wengine kusali, Yesu mwenyewe alisali hivi: ‘Ninakusifu hazarani [mbele ya watu] wewe, Baba, Bwana wa mbingu na dunia.’ (Luka 10:21) Wakati mwingine, ‘Yesu aliinua macho yake kuelekea mbinguni na kusema: Baba, ninakushukuru kwamba umenisikia.’ (Yohana 11:41) Na alipokaribia kufa, Yesu alisali hivi: ‘Baba, ninaikabizi [ninatoa] roho yangu mikononi mwako.’ (Luka 23:46) Kwa kusali kwa Baba yake wa mbinguni, aliye “Bwana wa mbingu na dunia,” Yesu alituachia sisi wote mufano tunaopaswa kufuata. (Mathayo 11:25; 26:41, 42; 1 Yohana 2:6) Ni hivyo wanafunzi wa kwanza wa Yesu walielewa maagizo yake?

NI KWA NANI WAKRISTO WA KWANZA WALIKUWA WANASALI?

Majuma machache kisha Yesu kurudia mbinguni, wanafunzi wake walisumbuliwa na kuogopeshwa na wapinzani wao. (Matendo 4:18) Kwa kweli, walisali ili kupata musaada, lakini walisali kwa nani? ‘Walimupaazia Mungu sauti zao kwa umoja,’ wakisali kwamba aendelee kuwasaidia ‘kupitia jina la mutumishi [wake] mutakatifu Yesu.’ (Matendo 4:24, 30) Kwa hiyo, wanafunzi walifuata maagizo ya Yesu juu ya sala. Walisali kwa Mungu, lakini haiko kwa Yesu.

Miaka fulani kisha hapo, mutume Paulo alieleza namna yeye na Wakristo wenzake walisali. Wakati aliwaandikia, alisema hivi: ‘Sikuzote sisi tunamushukuru Mungu Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo tunaposali kwa ajili yenu.’ (Wakolosai 1:3) Paulo aliandikia pia Wakristo wenzake juu ya ‘kumushukuru Mungu Baba, sikuzote na kwa ajili ya vitu vyote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.’ (Waefeso 5:20, Verbum Bible) Kupitia maneno hayo, tunaona kuwa Paulo alitia wengine moyo wasali kwa “Mungu Baba, sikuzote na kwa ajili ya vitu vyote,” lakini, bila shaka, kwa jina la Yesu.—Wakolosai 3:17.

Kama Wakristo wa zamani, tunaweza kuonyesha upendo wetu kwa Yesu kwa kufuata mashauri yake juu ya sala. (Yohana 14:15) Tunaposali kwa Baba yetu wa mbinguni peke yake tu, tutaelewa zaidi maana ya maneno ya Zaburi 116:1, 2. Andiko hilo linasema hivi: ‘Ninajawa na upendo, kwa sababu Yehova anasikia sauti yangu . . . nitaita siku zangu zote.’ *

^ fu. 3 Kulingana na Maandiko, Mungu na Yesu hawako sawa. Ili kupata habari zaidi, soma sura ya 4 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

^ fu. 11 Ili Mungu akubali sala zetu, tunapaswa kujikaza kwa moyo wote kuishi kulingana na mambo anataka tufanye. Ili kupata habari zaidi, soma sura ya 17 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini?