Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA | SERIKALI YENYE HAINA RUSHWA

Ufalme wa Mungu—Serikali Yenye Haina Rushwa

Ufalme wa Mungu—Serikali Yenye Haina Rushwa

“Mwishoni mwa siku, wakubwa wa serikali wangali tu raia na sisi wote tunatokana na jamii.” Musimamizi wa Uchunguzi katika Nicaragua alisema hivyo wakati alieleza sababu gani aliona kuwa haiwezekane kumaliza rushwa katika serikali.

Haukubali kuwa ikiwa jamii ya wanadamu ni yenye rushwa, serikali yoyote iliyo sehemu ya jamii hiyo itakuwa yenye rushwa? Ikiwa ni hivyo, basi serikali yenye haina rushwa haipaswe kutokana na watu. Biblia inazungumuzia serikali kama hiyo, ni kusema, Ufalme wa Mungu, serikali yenye Yesu alifundisha wafuasi wake waombe ikuje.—Mathayo 6:9, 10.

Ufalme wa Mungu ni serikali ya kweli inayotawala kutoka mbinguni. Itachukua nafasi ya serikali zote za watu. (Zaburi 2:8, 9; Ufunuo 16:14; 19:19-21) Kumaliza rushwa katika serikali ni kati ya baraka zenye Ufalme huo utaletea watu. Tuchunguze mambo sita juu ya Ufalme huo yanayohakikisha jambo hilo.

1. NGUVU

TATIZO: Serikali za watu zinapata feza kupitia raia zao, zaidi sana kupitia kodi na ushuru. Uwingi huo wa feza unasukuma wakubwa fulani wa serikali waibe, wengine wanakubali rushwa kutoka kwa watu wanaotaka wawapunguzie kodi ao malipo mengine wanayopaswa kulipa serikali. Hilo linaweza kutokeza hali yenye kuendelea, serikali inaongeza kodi ili kujaribu kurudisha feza zenye haikupata, na hilo linafanya rushwa iendelee sana. Katika hali kama hiyo, watu wanaofuatia haki wanaweza kuteseka sana.

NJIA YA KUMALIZA TATIZO HILO: Ufalme wa Mungu unapata nguvu zake kutoka kwa Yehova *, Mungu mweza-yote. (Ufunuo 11:15) Ufalme huo hauna lazima ya kukusanya kodi ili kufanya kazi. Tofauti na hilo, Mungu ni “hodari katika nguvu” na anatoa bila kutafuta faida zake mwenyewe, mambo hayo yanatuhakikishia kuwa Ufalme huo utahangaikia sana mahitaji ya raia zake wote.—Isaya 40:26; Zaburi 145:16.

2. MUTAWALA

TATIZO: Susan Rose-Ackerman, aliyetajwa katika habari iliyotangulia, anasema kuwa bidii ya kumaliza rushwa “inapaswa kuanzia juu.” Serikali zinapoteza uaminifu wakati zinajaribu kumaliza rushwa kati ya polisi na viongozi wa duane wakati ambapo zinaiacha iendelee kati ya viongozi wa serikali wa cheo cha juu. Na hata kiongozi muzuri zaidi ameriti pia kutokamilika. Kama vile Biblia inasema, ‘hakuna mwanadamu aliye muadilifu [mwenye haki] duniani ambaye anaendelea kufanya mema.’—Mhubiri 7:20.

Yesu alikataa rushwa kubwa sana kuliko zote

NJIA YA KUMALIZA TATIZO HILO: Yesu Kristo, mwenye Mungu alichagua ili akuwe Mutawala wa Ufalme huo, haiko kama watu wasiokamilika, yeye hawezi kushawishiwa kufanya mambo mabaya. Yesu alionyesha hivyo kwa kukataa rushwa kubwa sana kuliko zote, ni kusema, “falme zote za ulimwengu na utukufu wazo.” Yesu alitolewa ahadi ya kupewa falme hizo ikiwa tu anamufanyia Ibilisi, mutawala wa ulimwengu, tendo moja la ibada ya uongo. (Mathayo 4:8-10; Yohana 14:30) Hata wakati Yesu aliteswa mupaka kufa, alikusudia kubaki muaminifu. Ndiyo maana alikataa dawa ya kulewesha yenye ingepunguza maumivu yake na kumufanya asitumie kabisa uwezo wake mbalimbali. (Mathayo 27:34) Alipofufuliwa na Mungu na kurudia mbinguni, Yesu alionyesha waziwazi kuwa anastahili kabisa kutawala Ufalme huo.—Wafilipi 2:8-11.

3. KUTOBADILISHWA

TATIZO: Inchi nyingi zinafanya uchaguzi mara kwa mara, jambo wanalowazia kuwa linawaruhusu waondoe viongozi wenye rushwa. Hata hivyo, ukweli ni kwamba, mambo kama vile kampanye na uchaguzi yanaendeleza rushwa, hata katika inchi zinazojiita kuwa ni zenye kuendelea. Kupitia michango ya kampanye na matendo mengine, tajiri anaweza kuchochea zaidi watu wenye vyeo wa sasa na wa wakati unaokuja.

Mwanasheria John Paul Stevens wa Mahakama ya Juu ya Amerika aliandika kuwa hali hiyo inafanya kuwe “serikali isiyostahili, inaharibisha uwezo wa serikali wa kufanya kazi muzuri, na pia inafanya watu wasiitumainie.” Kwa hiyo, haishangaze kuwa watu wengi duniani wanaona vyama vya kisiasa kuwa na rushwa sana kuliko mashirika mengine yote.

NJIA YA KUMALIZA TATIZO HILO: Hakutakuwa kampanye ao uchaguzi wa udanganyifu katika Ufalme wa Mungu kwa sababu Ufalme huo ni serikali ya milele na yenye haitabadilishwa. (Danieli 7:13, 14) Kwa kuwa Mutawala wake anachaguliwa na Mungu, Ufalme huo hautegemee uchaguzi wa watu na hauwezi kuondolewa na watu. Kwa sababu Ufalme huo hautabadilishwa, hilo linasaidia kuhakikisha kuwa mambo utafanya sikuzote yataletea raia zake faida za milele.

4. SHERIA

Ufalme wa Mungu ni serikali ya kweli inayotawala kutoka mbinguni

TATIZO: Kwanza, unaweza kuwaza kuwa kutunga sheria za mupya kunaweza kutengeneza mambo. Lakini, watu wenye elimu wamevumbua kuwa katika hali nyingi, kuongeza sheria nyingi kunaongeza nafasi za kutoa rushwa. Tena, sheria zinazotungwa ili kupunguza rushwa mara nyingi zinaomba mambo mengi ili kuzifanya zifuatwe lakini zinaleta matokeo madogo tu.

NJIA YA KUMALIZA TATIZO HILO: Sheria za Ufalme wa Mungu ni za muzuri sana kuliko sheria za serikali za watu. Kwa mufano, kuliko kutolea watu sheria nyingi sana, Yesu alitoa ile inayoitwa mara nyingi Kanuni ya Muzuri Sana. Alisema hivi: ‘Kwa hiyo, mambo yote munayotaka watu wawatendee ninyi, lazima muwatendee wao pia vivyo hivyo.’ (Mathayo 7:12) Pengine jambo la maana zaidi, sheria za Ufalme zinachochea watu kuwa na nia na kutenda. Yesu alisema hivi: ‘Umupende jirani yako kama wewe mwenyewe.’ (Mathayo 22:39) Kwa kweli, Mungu anayeweza kusoma moyo, ana uwezo wa kufanya amri hizo zifuatwe.—1 Samweli 16:7.

5. NIA

TATIZO: Pupa na watu kutafuta faida zao wenyewe ndiyo mambo yanayofanya kuwe rushwa. Wakubwa wa serikali na raia mara nyingi wanaonyesha tabia hizo mbaya. Juu ya duka kubwa lililobomoka katika muji wa Seoul kama ilivyoonyeshwa katika habari iliyotangulia, viongozi wa serikali walikubali rushwa kutoka kwa wajenzi. Wajenzi hao walikuwa wanajua kama kupana rushwa kungewaomba feza kidogo kuliko kutumia ufundi na vyombo vinavyofaa vya ujenzi.

Kwa hiyo, ili kumaliza rushwa watu wanapaswa kufundishwa namna ya kuondoa nia zenye mizizi katika mioyo yao kama vile pupa na mutu kutafuta faida zake mwenyewe. Lakini, serikali za watu zinakosa nia na uwezo wa kuingiza mafundisho ya aina hiyo katika mioyo ya watu.

NJIA YA KUMALIZA TATIZO HILO: Ufalme wa Mungu unapiganisha rushwa kuanzia kwenye mizizi yake kwa kufundisha watu namna ya kuondoa nia mbaya zinazoileta. * Mafundisho hayo yanawasaidia “kufanywa upya katika nguvu zinazoendesha akili [zao].” (Waefeso 4:23) Wanajifunza kutosheka na kutafuta faida za wengine na wanaacha pupa na kujipenda wenyewe.—Wafilipi 2:4; 1 Timotheo 6:6.

6. RAIA

TATIZO: Hata ikiwa wanaishi katika mazingira ya muzuri na wanapewa mafundisho ya muzuri kuhusu mwenendo, watu fulani watachagua kuwa wadanganyifu na wenye kukubali rushwa. Watu wenye elimu wanakubali kuwa hiyo ndiyo sababu serikali za watu haziwezi kumaliza rushwa. Jambo linaloweza kutumainiwa ni kwamba serikali zinaweza tu kupunguza rushwa na kuzuia matokeo yake mabaya.

NJIA YA KUMALIZA TATIZO HILO: Kulingana na Mapatano ya Umoja wa Mataifa Juu ya Kumaliza Rushwa, ili kupiganisha rushwa, serikali zinapaswa kuchochea watu wawe “waaminifu, wenye kufuatia haki na wenye kutimiza madaraka yao.” Hata ikiwa huo ni muradi muzuri, Ufalme wa Mungu hauzungumuzie tu sifa hizo, lakini unaomba raia zake wakuwe nazo. Biblia inasema kuwa “watu wenye pupa” na “waongo” hawatauriti Ufalme.—1 Wakorintho 6:9-11; Ufunuo 21:8.

Watu wanaweza kujifunza namna ya kufuata kanuni hizo za muzuri za mwenendo, kama vile Wakristo wa zamani walifanya. Kwa mufano, wakati fulani mwanafunzi anayeitwa Simoni alijaribu kununua roho takatifu kutoka kwa mitume. Mitume walikataa rushwa hiyo na kumuambia hivi: “Tubu ubaya wako huu.” Simoni alipoona hatari ya tamaa yake mbaya, aliomba mitume wasali kwa ajili yake ili aweze kuishinda.—Matendo 8:18-24.

NAMNA YA KUWA RAIA WA UFALME

Hata ukuwe wa inchi gani, unaweza kuwa raia wa Ufalme wa Mungu. (Matendo 10:34, 35) Utajua namna ya kufanya hivyo kupitia programu ya mafundisho inayotolewa na Ufalme katika dunia yote leo. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukuonyesha namna wanajifunza Biblia na watu nyumbani kwao bila kulipa. Mupango huo unaweza kuchukua dakika kumi tu kila juma. Kati ya mambo mengine, unaweza kujifunza mengi juu ya “habari njema ya ufalme wa Mungu,” kutia ndani namna utamaliza serikali zenye rushwa. (Luka 4:43) Tunakuomba uzungumuze na Mashahidi wa eneo lenu ao ufungue adresi yetu ya Internete, jw.org.

Unapenda kujifunza Biblia nyumbani bila kulipa?

^ fu. 8 Yehova ni jina la Mungu kama inavyoonyeshwa katika Biblia.

^ fu. 22 Kwa mufano, soma habari “Je, Inawezekana Kufuatia Haki Katika Dunia hii Yenye Kujaa Rushwa?” katika gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 01/10/2012.