Ona video zinazopatikana

Biblia Inasema Nini Juu ya Kutoa?

Biblia Inasema Nini Juu ya Kutoa?

Jibu ya Biblia

 Biblia inatutia moyo tutoe kwa kujipendea na kwa nia ya muzuri. Inaonyesha kama kutoa kunaleteaka furaha mwenye anapokea na mwenye anatoa. (Mezali 11:25; Luka 6:38) Yesu alisema hivi: “Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.”​—Matendo 20:35.

 Ni kutoa ya namna gani njo inafurahishaka Mungu?

 Mungu anafurahiaka wakati tunatoa kwa kujipendea. Biblia inasema hivi: “Kila mumoja afanye kama vile alikusudia katika moyo wake, haiko kwa kutokutaka wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mutu mwenye anatoa kwa furaha.”​—2 Wakorinto 9:7, maelezo ya chini.

 Tunapaswa kutoa kwa moyo wote ikiwa tunapenda Mungu akubali “ibada” yetu. (Yakobo 1:27) Mutu mwenye kuwa tayari kusaidia wale wenye kuwa na lazima ya musaada anamufurahisha Mungu, na Mungu anaona kama kufanya vile ni kumukopesha. (Mezali 19:17) Biblia inafundisha kama Mungu yeye mwenyewe atamulipa.​—Luka 14:12-​14.

 Ni kutoa ya namna gani njo haifurahishake Mungu?

 Wakati nia ya mubaya njo inatuchochea kutoa. Kwa mufano, wakati tunatoa:

 Wakati tunatoa juu ya kutegemeza mambo yenye Mungu anakataza. Kwa mufano, ni mubaya kupatia mutu makuta juu aende kucheza michezo ya makuta, juu auze dawa za kulewesha, ao juu akunywe pombe kupita kiasi. (1 Wakorinto 6:9, 10; 2 Wakorinto 7:1) Vilevile, haiko muzuri kupatia mutu mwenye iko na nguvu ya kutumika juu ajitimizie mahitaji yake, lakini hapendi tu kutumika.​—2 Watesalonike 3:10.

 Wakati tunatoa kupita kiasi mupaka familia yetu inakosa mambo ya lazima. Biblia inafundisha kama vichwa vya familia wanapaswa kutimiza mahitaji ya watu wa familia yao. (1 Timoteo 5:8) Haiko muzuri kichwa cha familia akuwe mukarimu sana na kisha watu wa familia yake wakose mambo ya lazima. Vilevile, Yesu alilaumu wale wenye walikatala kuhangaikia wazazi wao wenye kuzeeka juu ya kusema kama mali yao yote ilikuwa “zawadi yenye imetolewa kwa Mungu.”​—Marko 7:9-​13.