Ona video zinazopatikana

Sababu Gani Yesu Alikufa?

Sababu Gani Yesu Alikufa?

Jibu la Biblia

 Yesu alikufa ili wanadamu waweze kusamehewa zambi zao na ili waweze kupata uzima wa milele. (Waroma 6:​23; Waefeso 1:7) Kifo cha Yesu kilionyesha wazi kuwa mwanadamu anaweza kubakia mwaminifu kwa Mungu hata kama anapata majaribu makali zaidi.—Waebrania 4:​15.

 Tuone namna kifo cha mutu mumoja kingeweza kutimiza mambo mengi sana.

  1.   Yesu alikufa ili ‘tusamehewe zambi zetu.’​—Wakolosai 1:​14.

     Adamu, mwanadamu wa kwanza, aliumbwa akiwa mukamilifu, bila zambi. Lakini, alichagua kukataa kumutii Mungu. Kukosa kutii kwa Adamu, ao zambi yake, kulikuwa na matokeo ya mubaya sana juu ya watoto wake wote. Biblia inasema hivi: ‘Kupitia kutotii [ao, kukosa kutii] kwa mutu mumoja wengi walifanywa watenda-zambi.’​—Waroma 5:​19.

     Yesu alikuwa pia mukamilifu, lakini hakufanya zambi hata kidogo. Kwa hiyo, angekuwa ‘zabihu ya upatanisho kwa ajili ya zambi zetu.’ (1 Yohana 2:2) Kama vile tu kukosa kutii kwa Adamu kulifanya familia ya wanadamu ikuwe na zambi, vilevile kifo cha Yesu kiliondoa doa la zambi kwa wote wenye kutia imani katika yeye.

     Tunaweza kusema kwamba Adamu aliuzisha watoto wake katika zambi. Yesu kwa kujipendea alikufa kwa ajili yetu; kwa hiyo, aliuza wanadamu kama vile watu wake. Matokeo ni kwamba, ‘yeyote akitenda zambi, tuna musaidizi kwa Baba, Yesu Kristo, mutu mwadilifu [ao, mwenye haki].’​—1 Yohana 2:1.

  2.   Yesu alikufa ili kila mutu mwenye anamuamini asiangamizwe lakini akuwe na uzima wa milele.​—Yohana 3:​16.

     Hata kama Adamu aliumbwa ili aishi milele, zambi yake ilifanya apate azabu ya kifo. Kupitia Adamu, “zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.”​—Waroma 5:​12.

     Tofauti na hilo, kifo cha Yesu hakikuondoa tu zambi, lakini kiliondoa pia hukumu ya kifo kwa wote wenye kuonyesha imani katika yeye. Biblia inafasiria hivi kwa kifupi: ‘Kama vile zambi ilitawala kama mufalme pamoja na kifo, vivyo hivyo pia fazili zisizostahiliwa zitawale kama mufalme kupitia uadilifu kwa tazamio la uzima wa milele kupitia Yesu Kristo Bwana wetu.’​—Waroma 5:​21.

     Ni kweli kwamba leo wanadamu hawajakuwa na uzima wa milele. Hata hivyo, Mungu anaahidi kwamba atapatia uzima wa milele wanadamu wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa na atafufua wafu ili wao pia waweze kufaidika na kifo cha Yesu.​—Zaburi 37:29; 1 Wakorintho 15:22.

  3.   Yesu ‘alikuwa mutiifu mupaka kifo,’ kwa hiyo, alionyesha kwamba mwanadamu anaweza kuwa muaminifu kwa Mungu hata kama anapata jaribu gani.​—Wafilipi 2:8.

     Hata kama alikuwa na mwili na akili yenye kukamilika, Adamu alikosa kumutii Mungu kwa sababu alitamani kwa uchoyo kitu chenye hakikuwa chake. (Mwanzo 2:​16, 17; 3:6) Wakati fulani kisha, Shetani, adui mukubwa wa Mungu alisema kwamba hakuna mwanadamu mwenye angemutii Mungu kwa kupenda, zaidi sana wakati maisha yake yako katika hatari. (Ayubu 2:4) Lakini, Yesu, mwenye alikuwa mwanadamu mukamilifu, alimutii Mungu na alibakia mwaminifu kwake, alivumilia hata kifo cha haya na chenye maumivu. (Waebrania 7:​26) Jambo hilo lilionyesha wazi kwamba Shetani ni muongo: Mwanadamu anaweza kubakia mwaminifu kwa Mungu hata kama anajaribiwa ao anapata magumu gani.

Maulizo juu ya kifo cha Yesu

  •   Sababu gani ilikuwa lazima Yesu ateseke na kufa ili kukomboa wanadamu? Sababu gani Mungu hakutosha tu hukumu ya kifo?

     Sheria ya Mungu inasema kwamba ‘mushahara ambao zambi inalipa ni kifo.’ (Waroma 6:​23) Kuliko kumuficha Adamu sheria hiyo, Mungu alimwambia kuwa malipizi yenye angepata kwa sababu ya kukosa kutii ni kifo. (Mwanzo 3:3) Wakati Adamu alifanya zambi, Mungu, mwenye ‘hawezi kusema uwongo,’ hakubadilisha maneno yake. (Tito 1:2) Adamu hakuambukizia tu watoto wake zambi, lakini pia mushahara wenye zambi inalipa, ni kusema, kifo.

     Hata kama wanadamu wenye zambi wanastahili azabu ya kifo, Mungu aliwaonyesha ‘utajiri wa fazili zake zisizostahiliwa.’ (Waefeso 1:7) Mupango wake wa kukomboa wanadamu​—kumutuma Yesu kama zabihu kamilifu​—ulikuwa wa haki kabisa na wenye rehema sana.

  •   Yesu alikufa wakati gani?

     Yesu alikufa na “saa tisa [ao, kenda]” kisha kuchomoza kwa jua, ao saa tatu hivi kisha midi (15:00) katika Pasaka ya Wayahudi. (Marko 15:33-​37) Tarehe hiyo inapatana na Siku ya tano, tarehe 1 Mwezi wa 4, mwaka wa 33 wakati wetu, kulingana na kalendari za siku zetu.

  •   Yesu alikufia wapi?

     Yesu alikufia nafasi “penye kuitwa Mahali pa Fuvu la Kichwa, katika kiebrania, Golʹgo·tha.” (Yohana 19:17, 18) Katika siku za Yesu, nafasi hiyo ilikuwa ‘inje ya lango’ la Yerusalemu. (Waebrania 13:12) Pengine ilikuwa ni kwenye kilima, kwa sababu Biblia inasema kwamba watu fulani waliona kuuawa kwa Yesu “wakiwa mbali.” (Marko 15:40) Lakini leo, hakuna mwenye anaweza kusema kwa uhakika mahali kwenye Golgotha ilipatikana.

  •   Yesu alikufa namna gani?

     Hata kama watu wengi wanaamini kuwa Yesu alitundikwa juu ya musalaba; Biblia inasema hivi: “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti.” (1 Petro 2:​24, Union Version) Waandikaji wa Biblia walitumia maneno mbili ya Kigiriki ili kuonyesha chombo chenye kilitumiwa juu ya kifo cha Yesu​—stau·rosʹ na xyʹlon. Watu wengi wenye elimu ya Biblia wamefikia kutambua kwamba maneno hayo yanazungumuzia kipande kimoja cha muti chenye kunyooka.

  •   Namna gani kifo cha Yesu kinapaswa kukumbukwa?

     Usiku moja wa Pasaka ya Wayahudi ya kila mwaka, Yesu pamoja na wanafunzi wake alianzisha mupango wenye hauombe mambo mengi na kuwaambia hivi: ‘Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.” (1 Wakorintho 11:24) Saa nyingi kisha hapo, Yesu aliuawa.

     Waandikaji wa Biblia walilinganisha Yesu na mwana-kondoo mwenye alitolewa kuwa zabihu wakati wa Pasaka. (1 Wakorintho 5:7) Kama tu vile Pasaka ilikumbusha Waisraeli kwamba walikuwa wamekombolewa katika utumwa, vilevile Ukumbusho wa kifo cha Yesu Kristo unakumbusha Wakristo kwamba wamekombolewa katika zambi na kifo. Pasaka yenye ilifanywa tarehe 14 Mwezi wa Nisani kulingana na kalendari ya mwezi, ilikuwa tukio la kila mwaka; vilevile Wakristo wa kwanza-kwanza walifanya Ukumbusho mara moja kila mwaka.

     Kila mwaka, mamilioni ya watu katika dunia yote wanakumbuka kifo cha Yesu katika tarehe yenye kupatana na tarehe 14, Mwezi wa Nisani.