Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Juu ya Nini Ni Muzuri Ufike ku Mikutano ku Jumba ya Ufalme?

Juu ya Nini Ni Muzuri Ufike ku Mikutano ku Jumba ya Ufalme?

 Mashahidi wa Yehova wanakusanyikaka mara mbili kila juma kwenye nafasi zao za ibada, zenye zinaitwa Majumba ya Ufalme. Nini njo inafanyikaka kule? Na unaweza kupata faida gani kama unafika ku ile mikutano?

 Nini njo inafanyikaka ku Jumba ya Ufalme?

 Jumba ya Ufalme ni fasi kwenye watu wanakutanaka juu ya kujifunza namna ya kutumikisha mafundisho ya Biblia. Mikutano yenye inafanyikaka ku Jumba ya Ufalme inaweza kukusaidia:

  •   ujifunze kweli juu ya Mungu.

  •   uelewe kama mambo yenye iko inatokea leo mu dunia inaonyesha nini.

  •   ukuwe mutu muzuri zaidi.

  •    upate marafiki wazuri.

 Ulijua? Fasi kwenye Mashahidi wa Yehova wanafanyiaka mikutano inaitwa Jumba ya Ufalme juu Ufalme wa Mungu njo jambo yenye wanazungumuziaka sana ku mikutano yao.​—Matayo 6:9, 10; 24:14; Luka 4:43.

 Juu ya nini ni muzuri ufike ku mikutano yetu?

 Habari yenye utajifunza kule itakusaidia. Kanuni za Biblia zenye wanazungumuziaka ku mikutano ya Mashahidi wa Yehova zitakusaidia ‘upate hekima.’ (Mezali 4:5) Ni kusema Biblia inaweza kukusaidia ukamate maamuzi ya muzuri mu maisha. Inaweza pia kukusaidia upate majibu ya maulizo ya maana sana yenye watu wanajiulizaka, sawa vile:

 Ona vichwa fulani vya hotuba zenye zinatolewaka ku mikutano yetu ya mwisho wa juma:

  •   Kwa Nini Tuongozwe na Biblia?

  •   Unaweza Kupata Wapi Musaada Katika Nyakati za Taabu?

  •   Mambo Ambayo Ufalme wa Mungu Unatufanyia Leo.

 “Mwanafunzi mwenzangu alikuya ku mikutano. Aliikala na familia yetu, na tulimusaidia kufuata mikutano mu vitabu vyetu. Kisha, aliniambia kama alifurahia sana maelezo yenye watu walikuwa wanatoa mu sehemu za maulizo na majibu. Alisema tena kama mu kanisa yao hawakuwake na vitabu vya kujifunzia ndani sawa vile siye.”​—Brenda.

 Ulijua? Kuingia ni bure, na hatulombake sadaka.

 Wengine watakutia moyo. Biblia inasema kama sababu moja kati ya sababu zenye zinafanyaka Wakristo wakutane pamoja ni juu ya ‘kutiana moyo.’ (Waebrania 10:24, 25) Kupitisha wakati pamoja na watu wenye wanamupenda Mungu na kuhangaikia wengine kunatia sana moyo mu hii dunia yenye inayala watu wenye kujipenda tu wao wenyewe.

 “Kisha kupitisha siku murefu sana, ninachokaka sana, na kukosa furaha. Lakini watu wenye ninakutanaka nao ku Jumba ya Ufalme wanafanyaka nijisikie muzuri. Wakati niko narudia ku nyumba kisha mikutano, ninakuwaka na furaha na ninakuwaka tayari kupambana na siku ya kufuata.”​—Elisa.

 Ulijua? Mu dunia yote, Mashahidi wa Yehova wako na makutaniko zaidi ya 120 000, na wanakutanaka mu Majumba ya Ufalme zaidi ya 60 000. Kila mwaka wanajengaka Majumba ya Ufalme 1 500 hivi kwa sababu hesabu ya watu wenye kufika ku mikutano inaendelea kuongezeka. *

^ Juu upate fasi kwenye Mashahidi wa Yehova wanafanyiaka mikutano yao, fungua ukurasa wenye kichwa, “Mikutano ya Kutaniko ya Mashahidi wa Yehova” kisha ufungue sehemu “Tafuta Adresi Karibu na Wewe.”