Ona video zinazopatikana

Video za Biblia: Mafundisho ya Musingi

Hizi video za mufupi za mafundisho ya Biblia zinajibu maulizo ya musingi yenye watu wanajiulizaka juu ya mafundisho ya Biblia na zinapatana na masomo ya mu broshua Habari Njema Yenye Inatoka Kwa Mungu!

Ulimwengu Uliumbwa?

Watu wengi hawaelewe habari ya Biblia juu ya uumbaji na hata wanawaza kama ni hadisi ya kuwazia-wazia. Unaweza kuamini mambo yenye Biblia inasema?

Mungu Anakuwaka?

Chunguza mambo yenye kuhakikisha kama kuamini kuwa Mungu iko inaeleweka.

Mungu Ana Jina?

Mungu ana majina mengi ya cheo, kama vile Mweza-Yote, Muumbaji, na Bwana. Lakini jina la pekee la Mungu linatajwa zaidi ya mara 7000 hivi katika Biblia.

Ni Nani Aliandikisha Biblia?

Kwa sababu wanadamu ndio waliiandika, inafaa kabisa kuitwa Neno la Mungu? Mawazo yenye kuwa katika Biblia ni ya nani?

Namna Gani Tunaweza Kuwa Hakika Kama Biblia Inasema Kweli?

Kama ni Mungu aliandikisha Biblia, inapaswa kuwa tofauti kabisa na vitabu vingine vyote.

Sababu Gani Mungu Aliumba Dunia?

Dunia inajaa vitu vya muzuri. Imewekwa mahali penye kufaa mbali na jua, imeinamishwa muzuri kabisa, na inazunguka kwa mwendo wenye kufaa kabisa. Sababu gani Mungu alifanya kazi nyingi hivyo ili kuumba dunia?

Watu Wenye Wamekufa Wako Katika Hali Gani?

Biblia inaahidi kama kuko wakati watu wengi watafufuliwa, ao kuamushwa kutoka katika kifo, kama vile tu Lazaro.

Yesu Kristo Ni Mungu?

Yesu Kristo njo uleule tu Mungu Mweza-Yote? Ao ni watu mbili tofauti?

Sababu Gani Yesu Alikufa?

Kulingana na Biblia, kifo cha Yesu ndicho cha maana sana. Kifo chake kilikuwa na kusudi gani?

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Katika mahubiri yake, Yesu alizungumuzia Ufalme wa Mungu kuliko jambo lingine lolote. Kwa miaka mingi, wanafunzi wake wamesali ili Ufalme huo ukuje.

Mungu njo Analetaka Misiba ya Asili?

Watu wawili wenye walipatwa na misiba ya asili wanaeleza kuhusu mambo yenye walijifunza mu Biblia .

Sababu Gani Mungu Anaacha Mateso?

Watu wengi wanajiuliza sababu gani dunia inajaa sana chuki na mateso. Biblia inatoa jibu lenye kuwa wazi na lenye kutia moyo.

Mungu Anakubali Dini Zote?

Watu mingi wanaamini kama dini zote ni za kweli.

Mungu Anapendaka Tutumie Sanamu Wakati Tuko Tunamuabudu?

Zinaweza kutusaidia tumukaribie Mungu juu hatuwezi kumuona?

Mungu Anasikilizaka Sala Zote?

Itakuwa je kama mutu anasali juu ya mambo yake mwenyewe tu? Itakuwa je kama bwana anatendea bibi yake mubaya kisha anaomba Mungu amubariki?

Pornografia ni zambi mbele ya Mungu?

Neno “pornografia” inakuwaka hata mu Biblia? Nini njo itatusaidia kujua mawazo ya Mungu kuhusu pornografia?