Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Tuliguswa Moyo Kuona Upendo Kama Huo

“Tuliguswa Moyo Kuona Upendo Kama Huo

SIKU YA POSHO, tarehe 25 Mwezi wa 4, 2015, tetemeko la inchi la kipimo cha 7.8 lilitikisa Nepali, inchi yenye milima mingi kaskazini mwa India. Tetemeko hilo lilifanyika kwenye kilometre 80 hivi kaskazini-mangaribi mwa Kathmandu, muji mukuu wa Nepali. Jambo la huzuni ni kwamba zaidi ya watu 8500 walikufa, na hilo lilifanya musiba huo kuwa wenye uliua watu wengi kuliko misiba ingine ya asili katika inchi ya Nepali. Zaidi ya nyumba 500000 ziliharibiwa. Katika Nepali kuna Mashahidi wa Yehova 2200, na wengi kati yao waliishi katika eneo lenye liliguswa na tetemeko hilo. Jambo lenye kuhuzunisha ni kwamba Shahidi mumoja na watoto wake wawili walikufa.

Shahidi wa Yehova mwenye kuitwa Michelle alisema hivi: “Tetemeko la inchi lilitokea wakati makutaniko mengi ya eneo lenye liliguswa sana yalikuwa katika mikutano yao ya Kikristo. Kama musiba huo ungetokea wakati wengi walikuwa nyumbani kwao, wengi wangeumia ao kufa.” Sababu gani wale wenye walikuwa kwenye mikutano walikuwa salama? Walikuwa salama zaidi sana kwa sababu ya namna Majumba ya Ufalme yalijengwa.

“SASA TUNAONA FAIDA!”

Majumba ya Ufalme ya sasa katika inchi ya Nepali yanajengwa ili yasibomoke wakati tetemeko la inchi linatokea. Man Bahadur, mwenye anatumika katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme, anasema hivi: “Mara nyingi watu walituuliza sababu gani tuliweka musingi wenye kuwa nguvu kwa ajili ya majengo madogo-madogo. Sasa tunaona faida!” Kisha tetemeko la inchi, ilikubaliwa kwamba Majumba ya Ufalme yatumiwe kama mahali pa kukimbilia. Hata kama matetemeko mengine madogo-madogo yalitokea, Mashahidi wa Yehova na majirani wao walijikuta salama katika Majumba hayo.

Mashahidi wa Yehova na majirani wao walikimbilia katika Majumba ya Ufalme

Wazee Wakristo walianza mara moja kutafuta washiriki wa kutaniko wenye walikuwa hawajapatikana. Shahidi mwenye kuitwa Babita alisema hivi: “Wazee walihangaikia usalama wa washiriki wa kutaniko mbele ya usalama wao. Tuliguswa moyo kuona upendo kama huo.” Siku yenye kufuata, ndugu watatu wa halmashauri yenye kusimamia kazi ya Mashahidi wa Yehova katika inchi ya Nepali pamoja na watumishi wenye kusafiri, ao waangalizi wa muzunguko, walianza kutembelea makutaniko ili kuona kama yako na lazima ya nini na kutegemeza wazee wa eneo hilo.

Gary Breaux, kutoka kwenye makao makubwa ya Mashahidi wa Yehova, alitembelea wenye walipatwa na musiba

Siku sita kisha tetemeko la inchi kutokea, ndugu Gary Breaux, kutoka kwenye makao makubwa ya Mashahidi wa Yehova katika inchi ya Amerika, alikuja Nepali pamoja na Ruby bibi yake. Ndugu Reuben wa halmashauri yenye tumekwisha kutaja alisema hivi: “Kwa sababu kulikuwa muvurugo katika muji wa Kathmandu, na pia matetemeko madogo-madogo yenye yalitokea, hatukuwa hakika kama Ndugu Breaux angekuja. Lakini aliazimia kuja hapa, na alifanya hivyo! Mashahidi wa eneo hilo walifurahi sana kuona anakuja kuwatembelea.”

‘TUNAJISIKIA KUWA KARIBU SANA KULIKO ZAMANI’

Silas, ndugu mwenye anatumika kwenye biro ya Mashahidi wa Yehova ya Nepali, alisema hivi: “Wakati iliwezekana tu kutumia tena telefone zetu, telefone ilianza kulia muchana na usiku! Mashahidi wenzetu katika dunia yote walituhangaikia sana. Hata kama wamoja kati yao walisema luga yenye hatuelewe, tuliona namna walikuwa na tamaa ya kutusaidia.”

Kikundi cha wanganga tano, Mashahidi wa Yehova, kutoka Ulaya kilisaidia wenye walipatwa na musiba

Kisha tetemeko kutokea, Mashahidi wa Yehova wa eneo walileta chakula kwa muda wa siku nyingi kwenye Majumba ya Ufalme ili kupatia wale wenye kuwa katika uhitaji. Tena kulianzishwa Halmashauri ya Misaada ya Wakati wa Misiba, na mara moja misaada ilianza kumwangika, zaidi sana kutoka Bangladesh, India, na Japani. Kisha siku fulani, kikundi cha wanganga, Mashahidi wa Yehova, kutoka Ulaya kilifika na kuanza kutumikia katika Jumba moja la Ufalme. Wanganga hao walianza kazi mara moja. Hawakuangalia tu hali ya kimwili ya wale wenye waliguswa na tetemeko lakini pia waliwasaidia kupambana na mahangaiko ya moyo.

Akionyesha namna watu wengi walijisikia, mwanamuke mwenye kuitwa Uttara alisema hivi: “Tetemeko la inchi lilikuwa la mubaya sana na lenye kuogopesha. Lakini, tulijisikia kuwa karibu sana kuliko zamani.” Kuliko kuregeza upendo wao kwa Yehova na kwa Wakristo wenzao, tetemeko hilo lilitia nguvu upendo huo.