Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Habari Fulani za Ulimwengu

Habari Fulani za Ulimwengu

Ujerumani

Katika mwaka wa 2012, moja kati ya mahakama ao tribinali kubwa za inchi ya Ujerumani iliamua kwamba watu hawawezi kuacha kanisa lao wakiwa katika shirika la watu wote na bado waendelee kuwa washiriki wa dini hiyo. Wakatoliki ambao waliacha kuenda kanisani, na ambao hawalipe tena kodi ya kanisa, lakini ambao wanaendelea na imani yao wanaweza kukatazwa kupokea ao kula Ekaristia, kuungama zambi zao, kupewa vyeo vya uongozi, na ikiwezekana, kutofanyiwa maziko na kanisa wakati wanakufa.

Ulimwengu

Uchunguzi uliofanywa juu ya dini za ulimwengu ulionyesha kwamba watu ambao wanasema kuwa “hawana dini yoyote,” hata ikiwa wao si watu ambao hawaamini kwamba kuna Mungu, sasa wanafikia hesabu ya watu miliare 1.1. Walichukua nafasi ya tatu kisha dini zinazojiita kuwa za Kikristo ambazo zina hesabu ya watu miliare 2.2 na dini ya Kiislamu iliyo na hesabu ya watu miliare 1.6. Dini ya Kihindu ilichukua nafasi ya ine, ikiwa na hesabu ya watu miliare 1.

Japani

Wanasayansi Wajapani wameonyesha kwamba “kusifiwa kunachochea sehemu za ubongo zinazohusiana na zawadi,” na hilo linamufanya mutu “ajisikie mwenye furaha.” Uvumbuzi huo unaonekana kuwa unahakikisha jambo la kwamba kusifiwa ni njia nzuri ya kumuchochea mutu afanye mambo mengi zaidi.

Bolivia

Mwishoni mwa mwaka wa 2012, watu wote wa inchi ya Bolivia walihesabiwa. Ili hesabu ya watu isiwe na makosa, wakaaji wa inchi ya Bolivia waliombwa wabaki nyumbani siku hiyo. Zaidi ya hiyo, watu walikatazwa kutembeza motokari zao, walikatazwa kunywa pombe, na mipaka ya inchi ilifungwa.

Italia

Katika uchunguzi fulani, wakaaji wa inchi ya Italia walisema kwamba, kwa kukadiria, wazazi walicheza na watoto wao kwa dakika 15 kila siku. Gazeti La Repubblica linasema kwamba “muzazi mumoja tu kati ya wazazi watano ndiye anafikiri kwamba kucheza na watoto ni njia ya kuwafundisha.” Kupitia michezo, wazazi wanasaidia watoto wao kukomalisha uwezo wa kufikiria mambo na kama vile Andrea Angiolino, mutu mwenye elimu ya michezo inayochezwa kwenye vibao, alivyosema, michezo inawasaidia pia “kuheshimu sheria.”