Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 KICHWA

Siri ya Kuwa na Furaha Katika Maisha

Siri ya Kuwa na Furaha Katika Maisha

“Nitakuwa mwenye furaha wakati nitafunga ndoa na kuwa na watoto.”

“Nitakuwa mwenye furaha wakati nitakuwa na nyumba yangu.”

“Nitakuwa mwenye furaha wakati nitapata kazi.”

“Nitakuwa mwenye furaha wakati . . .”

UMEKWISHA kuwa na mawazo kama hayo? Wakati ulifikia muradi wako ao wakati ulipata kitu ulichotamani, je, furaha yako iliendelea? Ao ilianza kupunguka? Ni kweli kwamba, kufikia muradi fulani ao kupata kitu tulichotamani kunaweza kutuletea furaha, lakini furaha hiyo ni ya muda mufupi. Furaha ya kudumu haitegemee tu kufikia miradi ao kupata vitu fulani. Inaomba mambo mengi ili kuwa na afya nzuri, vilevile furaha ya kweli inategemea mambo mengi.

Kila mutu iko tofauti na mwengine. Pengine mambo ambayo inakufurahisha haitamufurahisha mwengine. Tena, kadiri tunaendelea kukomaa, tunabadilika. Hata hivyo, ushuhuda unaonyesha kwamba kuna mambo fulani yanayoleta furaha. Kwa mufano, ili kuwa na furaha ya kweli inaomba kutosheka, kuepuka tamaa, kuwapenda wengine, na kuwa na uwezo wa kupambana na matatizo. Tuone sababu gani.

 1. TOSHEKA

Kisha kuchunguza maisha ya watu, mutu mwenye hekima alisema hivi: “Pesa ni ulinzi.” Lakini aliongeza hivi: ‘Anayependa feza hatatosheka na feza, wala anayependa mali hatatosheka na mapato. Hilo pia ni ubatili.’ (Mhubiri 5:10; 7:12) Alitaka kusema nini? Hata kama tunahitaji feza ili tuishi, tunapaswa kuepuka tamaa, sababu hatuwezi kushiba feza! Muandikaji Sulemani aliyekuwa Mufalme katika Israeli, alitafuta kujua ikiwa maisha ya utajiri na vitu vya kimwili yanaweza kuleta furaha ya kweli. Aliandika hivi: “Wala sikuyanyima macho yangu chochote ambacho yaliomba. Sikuunyima moyo wangu shangwe ya aina yoyote.”—Mhubiri 1:13; 2:10.

Kisha kupata mali mingi, Sulemani alijenga manyumba makubwa, alijifanyia mabustani mazuri na mahali pa kuogelea na alikuwa na wafanyakazi wengi. Kila kitu alitamani, alikipata. Alijifunza nini? Alipata furaha kwa kiasi fulani, lakini furaha ya muda tu. Alisema hivi: “Nilitazama kila kitu kilikuwa ubatili, na hapakuwa na lolote lenye faida chini ya jua.” Alifikia hata kuchukia maisha! (Mhubiri 2:11, 17, 18) Sulemani alijifunza kwamba kufuatia tu raha mwishowe kunamufanya mutu akose furaha na kutosheka. *

Uchunguzi wa leo unakubaliana na hekima hiyo ya zamani? Kitabu kimoja kinaonyesha kwamba “kisha kutimiza mahitaji ya lazima, kupata feza za zaidi hakuongezee mutu furaha kabisa.” (Journal of Happiness Studies) Pia, ushuhuda unaonyesha kwamba kufuatia sana vitu vya kimwili, zaidi sana ikiwa kunatufanya tuzarau mambo ya kiroho, kunaweza kumaliza furaha ya mutu.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Namna yenu ya maisha iwe bila upendo wa pesa, huku mukirizika na vitu vya sasa.’Waebrania 13:5.

2. EPUKA WIVU

Wivu ni “kujisikia mubaya ao kuwa na kinyongo kwa sababu ya vitu vya mutu mwengine, na hivyo, kutamani kuwa na vitu hivyo.” Kama vile ugonjwa wa kansa unaua chembe za mwili pole pole, wivu unamaliza pole pole furaha ya mutu. Wivu unaweza kuanza namna gani? Tunaweza kujua namna gani kwamba tuna wivu? Na tutapambana nao namna gani?

Kitabu fulani kinaonyesha kwamba watu wana mwelekeo wa kusikilia wivu watu walio kama wao, pengine, wana miaka moja ya kuzaliwa, uzoefu mumoja, ao hali moja ya maisha. Kwa mufano, mufanya biashara hawezi kusikilia wivu muchezaji mwenye kujulikana sana wa filme. Lakini atamusikilia wivu mufanya biashara mwenzake kwa sababu biashara yake inavuma. (Encyclopedia of Social Psychology)

Tuchukue mufano: Maofisa wakubwa katika utawala wa Uajemi ya zamani walimusikilia wivu ofisa mwenzao mwenye akili nyingi anayeitwa Danieli; hawakumusikilia wivu mufalme. Ili kuonyesha kama walimusikilia wivu sana, walipanga hata kumuua Danieli! Lakini hawakuweza. (Danieli 6:1-24) Kitabu tulichozungumuzia  kinasema hivi: “Ni jambo la lazima kujua kwamba wivu utakuchochea uwatendee wengine mambo mabaya. Hilo linaonyesha sababu gani katika historia watu wengi ambao walihusika katika jeuri walichochewa na wivu.” *

Wivu unaweza kuharibu uwezo wa mutu wa kufurahia mambo mazuri katika maisha

Unaweza kutambua namna gani kwamba una wivu? Jiulize: ‘Ikiwa mwenzangu anapata faida fulani, ninafurahi ao ninajiona wa bure? Ikiwa kaka ao dada yangu, mwanafunzi mwenzangu mwenye akili, ao mufanya kazi mwenzangu anashindwa, ninahuzunika ao ninafurahi?’ Ikiwa “unajiona wa bure” na “unafurahi,” hilo linaonyesha kwamba pengine wivu umekuwa na mizizi katika moyo wako. (Mwanzo 26:12-14) Kitabu kimoja kinasema “wivu unaweza kuharibu uwezo wa mutu wa kufurahia mambo mazuri katika maisha na kumufanya mutu asiwe mwenye shukrani kwa zawadi nyingi tunazopata katika maisha. . . . Muelekeo huo unamukosesha mutu furaha.” (Encyclopedia of Social Psychology)

Ili kuondoa wivu katika mioyo yetu inaomba tuonyeshe unyenyekevu wa kweli na kiasi. Sifa hizo zinatusaidia tupendezwe kabisa na uwezo mbalimbali na sifa nzuri za wengine. Biblia inasema hivi: ‘Bila kufanya jambo lolote kwa ugomvi ao kwa kujisifu, bali kwa unyenyekevu wa akili mukiwaona wengine kuwa ni bora kuliko ninyi.’—Wafilipi 2:3

KANUNI YA BIBLIA: ‘Na tusiwe wenye kujisifu, wenye kuchochea mashindano juu ya mutu na mwenzake, tukioneana wivu.’Wagalatia 5:26.

3. PENDA WENGINE

Kitabu kimoja kinasema: “Namna watu wanaona uhusiano wao na wengine inaweza kuwasaidia sana wawe wenye kutosheka katika maisha kuliko kazi yao, feza, jamii, ao hata afya yao.” (Social Psychology) Kwa kifupi, ili mutu awe na furaha ya kweli, ni lazima apende na kupendwa na wengine. Mwandikaji fulani wa Biblia alisema hivi: “Ikiwa . . . sina upendo, mimi si kitu.”—1 Wakorintho 13:2.

Ukitaka kujifunza kuwapenda wengine, haujachelewa. Kwa mufano, baba wa Vanessa alikuwa mukali na mulevi. Wakati alikuwa na miaka 14, alitoka nyumbani kwao ili kuishi katika familia fulani zilizokubali kumukaribisha, na pia, katika nyumba moja ya watu wasio na makao ambako anakumbuka kwamba alianza kumuomba Mungu amusaidie. Kisha, aliwekwa katika familia ambayo ilitumikisha kanuni ya Biblia inayosema kwamba ‘upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fazili.’ Pengine hiyo ilikuwa jibu kwa sala yake. (1 Wakorintho 13:4) Hali ya familia hiyo, na yale alikuwa anajifunza kupitia funzo lake la Biblia, yalimusaidia Vanessa apate kitulizo katika moyo na akili. Alisema hivi: “Nilianza kuweza masomo.”

Vanessa angali anaumia katika moyo wake. Hata hivyo, kwa sasa yeye ni mama mwenye furaha, na ana mabinti wawili.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Mujivike upendo, kwa maana huo ni kifungo kikamilifu cha muungano.’—Wakolosai 3:14.

 4. JIFUNZE KUPAMBANA NA MATATIZO

Kuna mutu asiye na magumu katika maisha? Kama vile Biblia inasema, kuna “wakati wa kulia” na “wakati wa kuomboleza.” (Mhubiri 3:4) Uwezo wa kupambana na matatizo unatusaidia tuendelee mbele ijapokuwa magumu. Fikiria mufano wa Carol na Mildred.

Carol ana ugonjwa wa uti wa mugongo, diabete ao ugonjwa wa sukari, kushindwa kupumua anapolala, na ugonjwa ambao umefanya jicho lake la kushoto lisione tena. Lakini anasema: “Ninajikaza ili nisiwe mwenye kuvunjika moyo kwa wakati murefu sana. Wakati fulani ninajisikilia huruma. Lakini kisha ninasahau magumu yangu na kumushukuru Mungu kwa yale ninaweza kufanya, zaidi sana kwa ajili ya wengine.”

Mildred naye ana magonjwa mengi, kama vile maumivu ya sehemu zinazounganisha viungo, kansa ya maziba, na diabete. Lakini kama Carol, anajikaza ili asiwaze mingi juu ya magumu yake. Aliandika hivi: “Nimejifunza kuwapenda watu na kuwafariji wengine wakati wanagonjwa, kufanya hivyo kunanisaidia mimi pia. Tena, ninatambua kwamba wakati ninafariji wengine, ninasahau magumu yangu.”

Carol na Mildred walipata furaha kwa kuwafariji wengine

Hata kama wanawake hao wawili wanapenda kupata matunzo mazuri, hawahangaikie tu afya yao ya kimwili, lakini wanajikaza kuwa na maoni yanayofaa juu ya matatizo yao na wanatumia vizuri wakati wao. Kwa hiyo, wanapata furaha ya moyoni ambayo hakuna mutu anaweza kuwanyanganya. Tena, wanapendwa na wengine na wanakuwa mufano muzuri kwa watu walio na magumu.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Mwenye furaha ni mutu anayeendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima.’Yakobo 1:12.

Shauri hilo lenye hekima la Biblia linapotumikishwa ni ‘muti wa uzima kwa wale wanaoishika, na wale wanaoishika sana wataitwa wenye furaha.’ (Methali 3:13-18) Unaweza kutambua kweli hiyo wewe mwenyewe kwa kutumikisha hekima inayopatikana katika Biblia. Kwa vyovyote, Mutungaji wa kitabu hicho kitakatifu, anayeitwa “Mungu mwenye furaha” anataka wewe pia uwe mwenye furaha. —1 Timotheo 1:11.

^ fu. 11 Mambo ambayo Sulemani alijionea yanapatikana kwenye Mhubiri 2:1-11.

^ fu. 17 Mufano mwengine wa pekee unahusu namna Yesu Kristo alivyoonewa wivu. Andiko la Marko 15:10 linasema hivi: ‘Wakubwa wa makuhani walikuwa wamemutia mikononi mwake kwa sababu ya wivu’ ili Yesu auawe.