Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA | BIBLIA NI YA MAANA LEO?

Kanuni Zinazotumika Sikuzote na Zenye Kufaa Kila Mutu—Kufuatia Haki

Kanuni Zinazotumika Sikuzote na Zenye Kufaa Kila Mutu—Kufuatia Haki

KANUNI YA BIBLIA: ‘Ni nani atakayekuwa mugeni katika hema [la Mungu]? . . . Yeye anayetembea bila kosa na kuzoea kutenda uadilifu [ao haki] na kusema kweli katika moyo wake.’Zaburi 15:1, 2.

FAIDA: Watu wengi wanaona kufuatia haki na utimilifu kuwa jambo la maana. Lakini wanafanya namna gani wakati nafasi ya kufaidika kwa kukosa kufuatia haki inajitokeza, na hakuna mutu anayejua jambo hilo? Katika hali hiyo, mukazo unatiliwa juu ya moyo, ni kusema, mutu wa ndani.

Raquel, ambaye kazi yake inatia ndani kununua vitu kwa ajili ya kompanyi yake, anasema hivi: “Watu fulani waliokuwa ­wanauzisha vitu walinitolea hongo (kata-midomo, kanyaka). Waliniahidi kuwa ikiwa ninanunua vitu kwao, wataniachia ‘faida’ fulani kuliko kuipatia kompanyi yangu. Lakini nilikumbuka shauri la Biblia la kufuatia haki na nikakataa. Mukubwa wangu wa kazi alisikia juu ya habari hiyo, na akanitumainia zaidi.”

Raquel angejiacha ashawishiwe na mambo waliyomutolea, angepata feza nyingi katika muda kidogo. Lakini, ingekuwa namna gani ikiwa mukubwa wake wa kazi angejua jambo hilo? Raquel angeendelea na kazi yake? Na je, angetumaini kupata kazi ingine? Zamiri na kujiheshimia ndiyo yalikuwa mambo ya maana kwa Raquel. Andiko la Methali 22:1 linasema hivi: ‘Ni afazali [muzuri] kuchagua jina badala ya utajiri mwingi; kibali [kukubaliwa] ni bora kuliko hata feza na zahabu.’

Jessie alijifanyia jina la muzuri kwa sababu ya kuwa mufanyakazi mwenye kufuatia haki

Jessie pia alikuwa mutu mwenye kufuatia haki na mwenye kutumainika, kwa hiyo akajifanyia jina la muzuri kwa mukubwa wake wa kazi. Alipata faida gani? Alipewa cheo cha usimamizi katika kazi na uhuru zaidi katika programu yake ya kazi. Hilo lilimuwezesha kupata wakati mwingi wa kupitisha pamoja na bibi yake na watoto wake na katika kazi za kiroho.

Wakati wakubwa fulani wa kazi wanatafuta wafanyakazi, wanaenda kwenye vikundi vya watu wanaojulikana kuwa wenye kufuatia haki. Kwa mufano, kiongozi wa kompanyi moja katika Ufilipino aliandikia biro ya Mashahidi wa Yehova wa eneo hilo kuwa Mashahidi waombe kazi katika kompanyi yake. Alisema hivi: “Wanatumika kwa bidii, ni wenye kufuatia haki, na wanajitoa kabisa.” Sifa kwa ajili ya jambo hilo inapaswa kumuendea Yehova Mungu, anayetufundisha ‘kuchukia yaliyo mabaya’ na ‘kupenda yaliyo mema.’—Amosi 5:15.