Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | KULEA WATOTO

Wakati Mutoto Wako Anauliza Juu ya Kifo

Wakati Mutoto Wako Anauliza Juu ya Kifo

TATIZO

Mutoto wako mwenye miaka sita anakuuliza, “Utakufaka siku moja?” Unashangazwa sana na ulizo lake na unajiuliza hivi: ‘Mutoto wangu amekomaa vya kutosha ili kuelewa jibu nitamupatia? Namna gani ninaweza kuzungumuza naye juu ya kifo?’

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Watoto wanawaza kabisa juu ya kifo. Watoto fulani wanafanya hata michezo ambamo mumoja anajifanya kuwa anakufa. Kwa hiyo, haupaswi kuona kifo kuwa habari isiyofaa kuzungumuziwa, na unapaswa kuzungumuzia kila ulizo lenye mutoto wako anaweza kuuliza juu ya kifo. Mara kwa mara unapozungumuza waziwazi juu ya kifo, unamusaidia mutoto wako ajifunze namna ya kupambana na kifo cha mutu anayependa.

Kuzungumuza juu ya kifo hakutafanya mutoto wako akuwe na mawazo yenye kuogopesha. Lakini, kutamusaidia kupunguza woga. Hata hivyo, unaweza kubadilisha mawazo fulani yanayoeleweka mubaya. Kwa mufano, watu fulani wenye elimu wanasema kuwa watoto wengi wenye kuwa na miaka chini ya sita hawaone kifo kuwa mwisho. Katika michezo yao, mutoto anaweza kujifanya kuwa “anakufa” wakati fulani na kuwa mwenye “kuishi” wakati mwengine.

Lakini, wakati wanakomaa kidogo, watoto wanaanza kukamata kifo kwa uzito na jambo hilo linaweza kuwafanya wakuwe na maulizo mengi, mahangaiko, ao hata woga, zaidi sana ikiwa mutu fulani walikuwa wanapenda amekufa. Kwa hiyo, ni lazima kuzungumuzia jambo hilo. Marion Haza, mutu mwenye elimu ya afya ya akili anasema hivi: “Mutoto anaweza kuwa na mahangaiko juu ya kifo ikiwa anajisikia kuwa hana ruhusa ya kuzungumuza juu ya habari hiyo nyumbani.”

• Haupaswe kuogopa sana juu ya mambo yenye utasema. Kulingana na uchunguzi fulani, watoto wanataka tu “kusikia kweli yenye kuelezwa katika maneno ya muzuri.” Ukuwe hakika kuwa mara nyingi mutoto atauliza ulizo ikiwa tu iko hakika kuwa atapata jibu.

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Utumie nafasi zenye kujitokeza ili kuzungumuza juu ya kifo. Ikiwa mutoto wako anaona ndege aliyekufa pembeni ya barabara ao ikiwa munyama wa kufuga aliyekuwa anapenda anakufa, tumia maulizo mepesi ili kumutia moyo azungumuze. Kwa mufano, unaweza kumuuliza: “Munyama aliyekufa anateseka? Anasikia baridi ao njaa? Namna gani unajua kuwa munyama ao mutu amekufa?”—Kanuni ya Biblia: Mhubiri 3:1, 7.

Usifiche kweli. Wakati rafiki ao mutu wa familia amekufa, epuka kutumia maneno ya mifano kama vile “Ameenda zake.” Mutoto wako anaweza kuwa na mawazo ya makosa kwamba mutu aliyekufa atarudia nyumbani bila kukawia. Kuliko kufanya hivyo, tumia maneno mepesi na ya moja kwa moja. Kwa mufano, unaweza kusema hivi: “Wakati tate (nkambo) mwanamuke alikufa, mwili wake uliacha kutumika. Hatuwezi kuzungumuza naye, lakini hatutamusahau hata siku moja.”—Kanuni ya Biblia: Waefeso 4:25.

Kwa sababu mutoto mudogo anaweza kufikiri kuwa kifo kinaweza kuambukizwa, umuhakikishie kuwa kifo hakitamuambukiza

Umutulize mutoto wako. Mutoto anaweza kuwaza kuwa matendo ao mawazo yake ndiyo yalitokeza kifo cha mutu fulani. Kuliko tu kumuambia kama haiko yeye ndiye alitokeza jambo hilo, unaweza kumuuliza, “Ni nini kinakufanya uwaze kuwa ni kosa lako?” Umusikilize kwa uangalifu, bila kuzarau namna anajisikia. Tena, kwa sababu mutoto mudogo anaweza kufikiri kuwa kifo kinaweza kuambukizwa, umuhakikishie kuwa kifo hakitamuambukiza.

Umusaidie mutoto wako afunue mambo yenye kuwa katika moyo wake. Zungumuza kwa uhuru juu ya watu munaopenda ambao wamekufa, hata watu wa jamaa yako wenye mutoto wako hakuona. Unaweza kuzungumuzia mambo mazuri ya zamani juu ya shangazi, mujomba, ao tate na kueleza mambo yenye kuchekesha juu yao. Wakati unazungumuza waziwazi juu ya watu kama hao, unamusaidia mutoto wako aelewe kuwa hapaswi kuepuka kuzungumuza ao kuwaza juu yao. Lakini, usimulazimishe mutoto wako azungumuze. Unaweza kutokeza habari hiyo baadaye, ukiona kuwa huo ndio wakati wenye kufaa.—Kanuni ya Biblia: Methali 20:5.

Sura ya 34 na ya 35 ya kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu zinaweza kusaidia mutoto wako ajifunze mambo Biblia inafundisha juu ya kifo. Unaweza kuchukua Fungua kichwa MACHAPISHO > VITABU & BROSHUA

Although we refer to the child as a boy, the principles discussed apply to girls as well.