Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Walijitoa kwa Kujipendea​—Katika Madagaska

Walijitoa kwa Kujipendea​—Katika Madagaska

Sylviana, dada painia mwenye kuwa na miaka 27 anasema hivi: “Wakati nilisikiliza mambo yenye marafiki wangu wenye walitumikia katika maeneo yenye kuwa na lazima kubwa ya mapainia walikutana nayo, nilipenda pia kuonja furaha hiyo.” Anaongeza hivi: “Lakini niliogopa kuwa singeweza kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri.”

Wewe pia unakubaliana na maneno hayo ya Sylviana? Wewe pia unapenda kutumikia katika eneo lenye kuwa na lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme, lakini unajiuliza ikiwa utaweza kufikia muradi huo? Kama ni hivyo, usivunjike moyo! Kwa musaada wa Yehova, maelfu ya ndugu na dada wamepata ushindi juu ya mambo yenye yaliwazuia kupanua utumishi wao. Ili kujua namna Yehova amefungulia njia wamoja kati yao, tutatembelea Madagaska, kisiwa cha ine chenye kuwa na ukubwa zaidi katika dunia.

Kwa miaka kumi yenye imepita, wahubiri na mapainia wenye bidii zaidi ya 70 kutoka katika inchi 11 * wamekuja kutumikia katika eneo hili la Afrika lenye matokeo ya muzuri, kwenye watu wanaheshimia sana Biblia. Pia, wahubiri wengi wa inchi hiyo wamependa kuhamia katika maeneo mengine ili kusaidia kutangaza ujumbe wa Ufalme katika eneo kubwa la kisiwa hicho. Tuzungumuze basi na wamoja kati yao.

KUMALIZA WOGA NA KUACHA KUVUNJIKA MOYO

Perrine na Louis

Louis na Perrine bibi yake, wenye kuwa na zaidi ya miaka 30, walitoka Ufaransa na kuhamia Madagaska. Kwa miaka mingi, walikuwa wanafikiria namna ya kupanua utumishi wao kwa kuhamia katika inchi ingine, lakini Perrine alisita kuhama. Anasema hivi: “Niliogopa kuenda nafasi yenye sijue. Nilikuwa na wasiwasi juu ya kuacha familia yetu, kutaniko, nyumba, nafasi zote zenye nilikuwa ninazoea, na mambo yenye tulikuwa tunazoea kufanya. Kwa kweli, wasiwasi wangu ndio ulikuwa kizuizi kikubwa chenye nilipaswa kumaliza.” Katika mwaka wa 2012, Perrine alijikaza sana kumaliza woga, na yeye na Louis wakahama. Anajisikia namna gani juu ya uamuzi wao? Anasema hivi: “Wakati ninakumbuka, ninaweza kusema kama imani yetu imetiwa nguvu kuona mukono wa Yehova katika maisha yetu.” Louis anaongezea hivi: “Wazia jambo hili, kwenye ukumbusho wetu wa kwanza katika Madagaska, watu kumi kati ya wanafunzi wetu wa Biblia walihuzuria!”

Ni nini iliwapatia nguvu ya kubakia katika mugawo wao wakati magumu yalitokea? Walimulilia Yehova katika sala ili awapatie nguvu yenye wako nayo lazima ili kuvumilia. (Flp. 4:13) Louis anaeleza hivi: “Tuliona kuwa Yehova alijibia sala zetu na akatupatia ‘amani ya Mungu.’ Tuliweza kukaza akili juu ya furaha yenye utumishi wetu ulikuwa unatuletea. Pia, marafiki wetu wa Ufaransa walikuwa wanatutumia ujumbe kwenye Internete na barua ili kututia moyo tusiache utumishi wetu.”​—Flp. 4:6, 7; 2 Kor. 4:7.

Yehova alibariki sana uvumilivu wenye Louis na Perrine walionyesha. Louis anasema hivi: “Katika Mwezi wa 10, 2014, tulisoma Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu na Bibi Zao * katika Ufaransa. Kusoma masomo hayo ni zawadi kutoka kwa Yehova yenye hatuwezi kusahau hata kidogo.” Kisha tu kumaliza masomo hayo, Louis na Perrine walifurahi kutumwa tena katika Madagaska.

“TUTAFURAHI SANA KWA AJILI YENU!”

Nadine na Didier

Wakati Didier na Nadine, bibi yake kutoka Ufaransa walihamia Madagaska katika mwaka wa 2010, walikuwa na zaidi ya miaka 50. Didier anasema hivi: “Tulifanya kazi ya upainia wakati tulikuwa tungali vijana, na kisha tukalea watoto 3. Wakati walikomaa na kuwa watu wazima, tulifikiri ikiwa tunaweza kutumikia katika inchi ingine.” Nadine anasema hivi: “Kuwaza kama ningekuwa mbali na watoto kulinifanya nisite, lakini walituambia hivi: ‘Ikiwa munahamia katika inchi ingine ili kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri, tutafurahi sana kwa ajili yenu!’ Maneno yao yalituchochea kuhama. Hata kama sasa tunaishi mbali na watoto wetu, tunafurahi kwa sababu tunaweza kuzungumuza nao mara kwa mara.”

Ilikuwa vigumu kwa Didier na Nadine kujifunza luga ya Kimalagasi. Nadine anasema hivi kwa kicheko: “Hatuna tena miaka 20.” Namna gani waliweza kujifunza luga hiyo? Kwanza waliingia katika kutaniko lenye kutumia luga ya Kifaransa. Kisha, wakati waliona kuwa wanaweza kutumia wakati mwingi zaidi ili kujifunza luga hiyo, walihamia katika kutaniko lenye kutumia luga ya Kimalagasi. Nadine anasema hivi: “Watu wengi wenye tunakutana nao katika kazi ya kuhubiri, wanapenda kujifunza Biblia. Mara nyingi wanatushukuru kwa sababu tunawatembelea. Mwanzoni nilifikiri kama nilikuwa ninaota ndoto. Ninapenda kufanya kazi ya upainia katika eneo hili. Wakati ninaamuka asubui, ninajiambia hivi, ‘ni muzuri sana​—ninaenda kuhubiri leo!’”

Didier anaonyesha sura ya kicheko wakati anakumbuka namna alianza kujifunza luga ya Kimalagasi. Anasema hivi: “Nilikuwa ninaongoza mukutano wa kutaniko, lakini sikuelewa majibu yenye ndugu na dada walikuwa wanatoa. Jambo moja tu lenye nilikuwa ninasema lilikuwa, ‘Aksanti.’ Kisha kumushukuru dada mumoja juu ya jibu lake, watu fulani wenye walikuwa wanakaa nyuma yake walianza kufanya ishara fulani ili kuniambia kama jibu hilo halikukuwa la kweli. Mara moja nilitaja ndugu mwenye alitoa jibu la muzuri; kwa kweli, ninafikiri alitoa jibu la muzuri.”

ALIKUBALI KWA FURAHA MUALIKO

Kwenye mukusanyiko moja katika mwaka wa 2005, Thierry na Nadia, bibi yake, waliangalia muchezo wenye kutegemea Biblia wenye kichwa “Fuatia Miradi Inayomletea Mungu Heshima.” Muchezo huo wenye kutegemea Biblia wenye kuzungumuzia Timotheo uligusa moyo wao na kuwafanya wakuwe na hamu sana ya kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme. Thierry anasema hivi: “Mwishoni mwa muchezo huo, wakati tulikuwa tunapiga mikono, nilisegemea bibi yangu, na kumuuliza hivi, ‘Tunaweza kuhamia wapi?’ Bibi yangu aliniambia kama yeye pia alikuwa anafikiria jambo hilo.” Muda mufupi kisha hapo, walianza kukamata mipango ya kuwasaidia kufikia muradi wao. Nadia anasema hivi: “Hatua kwa hatua tulipunguza vitu vyenye tulikuwa navyo, mupaka vikaenea katika valize ine!”

Kushoto sana: Nadia na Marie-Madeleine; Kuume sana: Thierry

Walifika katika Madagaska mwaka wa 2006 na walifurahia kazi yao ya kuhubiri tangu wakati huo. Nadia anasema hivi: “Watu wenye tunazungumuza nao wanatuletea furaha nyingi.”

Lakini, kisha kupita miaka sita, ndugu huyo na bibi yake walipata magumu. Marie-Madeleine, mama ya Nadia, mwenye alikuwa anaishi katika Ufaransa, alianguka na kuvunjika mukono na akaumia kwenye kichwa. Kisha ndugu huyo na bibi yake kuzungumuza na munganga wa Marie-Madeleine, waliomba mama yao ahame na kuishi pamoja nao katika Madagaska. Hata kama alikuwa na miaka 80 wakati huo, alikubali kwa furaha mualiko huo. Anajisikia namna gani juu ya kuishi katika inchi ingine? Asema hivi: “Wakati fulani ni vigumu kuzoea, lakini hata kama niko na nguvu kidogo, ninajiona kuwa mutu wa maana katika kutaniko. Na jambo lenye kuniletea furaha kabisa ni kwamba kukubali mupango huu kunasaidia watoto wangu waendelee kuhubiri katika eneo hili lenye kuzaa matunda.”

“NILIONA MUSAADA WA MUKONO WA YEHOVA”

Riana anatoa hotuba katika luga ya Tandroy

Riana ni ndugu mwenye kuwa na miaka 22. Alikomalia katika Alaotra Mangoro, eneo lenye kuzaa sana chakula katika mashariki mwa Madagaska. Alitumika muzuri kwenye masomo na alipenda kusoma masomo ya juu. Lakini, kisha kujifunza Biblia, akabadilisha mawazo yake. Anasema hivi: “Nilijikaza kumaliza masomo ya segondere mbele ya wakati na kumuahidi Yehova, ‘Kama tu ninaweza mashindano ya mwisho, nitaanza kufanya kazi ya upainia.’” Kisha kumaliza masomo ya segondere, Riana alitimiza ahadi yake. Alihama pamoja na ndugu mumoja painia, akapata kazi yenye haikumukamata wakati mwingi, na akaanza kufanya kazi ya upainia. Anasema hivi: “Huo ndio uamuzi wa muzuri zaidi wenye nimefanya.”

Hata hivyo, watu wa jamaa ya Riana hawakuelewa sababu gani hakufuatia kazi ya kimwili. Anasema hivi: “Baba yangu, na baba yangu mudogo, na shangazi (mudogo wa mama ya baba yangu), wote walinitia moyo nifuatie masomo ya juu. Lakini sikupenda kuacha kazi ya upainia hata kidogo.” Bila kukawia, Riana alipenda kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri. Ni nini ilichochea zaidi tamaa yake? Anasema hivi: “Wezi waliingia katika nyumba yetu na wakaiba vitu vyangu vingi. Tukio hilo lilinichochea nifikirie maneno yenye Yesu alisema juu ya ‘kuweka hazina mbinguni.’ Niliamua kutumika sana ili kupata utajiri wa kiroho.” (Mt. 6:19, 20) Alihamia katika eneo la mbali sana kusini mwa inchi; eneo lenye kukauka lenye lilikuwa kwenye umbali wa kilometre 1300 kutoka mahali kwenye alikuwa anaishi. Watu wa kabila la Antandroy ndio wanaishi katika eneo hilo. Sababu gani alihamia huko?

Mwezi mumoja mbele wezi waibe vitu vyake, Riana alikuwa ameanzisha funzo moja la Biblia pamoja na wanaume wawili wa kabila la Antandroy. Alijifunza maneno fulani katika luga yao na kufikiria sana watu wengi wa kabila la Antandroy wenye walikuwa hawajahubiriwa ujumbe wa Ufalme. Anasema hivi: “Nilisali kwa Yehova anisaidie nihamie katika eneo kwenye watu wanazungumuza luga ya Tandroy.”

Riana alihamia huko, na mara moja alipambana na magumu. Hakuweza kupata kazi. Mwanaume mumoja alimuambia hivi: “Sababu gani ulihamia katika eneo hili? Ili kupata kazi, watu wenye kuishi hapa wanahamia kule kwenye ulitoka!” Kisha juma mbili Riana aliondoka bila feza ili kuhuzuria mukusanyiko wa eneo, na alikuwa anajiuliza ikiwa atafanya nini. Kwenye siku ya mwisho ya mukusanyiko huo, ndugu mumoja aliweka kitu fulani katika mufuko wa koti la Riana. Ilikuwa kiasi cha feza zenye alikuwa nazo lazima ili kufanya safari ya kurudia katika eneo la Antandroy na kumusaidia kuanza kazi kidogo ya kuuzisha maziwa yenye kuganda. Riana anasema hivi: “Niliona musaada wa mukono wa Yehova kwa wakati wenye kufaa kabisa. Ningeweza kuendelea kusaidia wale wenye walikuwa hawajapata nafasi ya kujifunza juu ya Yehova!” Kulikuwa pia mengi ya kufanya katika kutaniko. Riana anaongeza hivi: “Nilipewa mugawo wa kutoa hotuba ya watu wote kisha kila juma moja. Yehova alikuwa ananizoeza kupitia tengenezo lake.” Leo, Riana anaendelea kuhubiria ujumbe wa Ufalme watu wengi wenye kuzungumuza luga ya Tandroy wenye wanapenda kumujua Yehova.

BARAKA KUTOKA KWA MUNGU WA UKWELI

Yehova anatuhakikishia kama “yeyote anayejibariki duniani atajibariki kwa Mungu wa imani [ao, ukweli].” (Isa. 65:16) Wakati tunajikaza sana ili kumaliza vizuizi na kupanua utumishi wetu, tunapata baraka kutoka kwa Yehova. Fikiria mufano wa Sylviana, mwenye kuzungumuziwa kwenye mwanzo wa habari hii. Ukumbuke kama, aliogopa kwamba hakukuwa na uwezo wa kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri. Sababu gani alifikiri hivyo? Anaeleza hivi: “Muguu wangu wa kushoto uko na ufupi wa santimetre 9 kuliko muguu wangu wa kuume. Kwa hiyo, sitembee muzuri na ninachoka mbio sana.”

Sylviana (kushoto) na Sylvie Ann (kuume) pamoja na Doratine siku ya ubatizo wake

Hata hivyo, katika mwaka wa 2014, Sylviana alijiunga na Sylvie Ann, dada kijana painia wa kutaniko lake, na wakahamia katika kijiji kidogo chenye kuwa kwenye umbali wa kilometre 85 kutoka kwenye muji wao. Hata kama alipambana na magumu, Sylviana alifikia muradi wake, na alipata baraka za muzuri sana! Anasema hivi: “Kisha kutumikia mwaka moja tu katika mugawo wangu mupya, Doratine, mama kijana mwenye nilikuwa ninajifunza naye Biblia alibatizwa kwenye mukusanyiko wetu wa muzunguko.”

“NITAKUSAIDIA”

Kama vile imani ya wale wenye kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri inaonyesha, wakati tunajikaza kumaliza vizuizi ili kupanua utumishi wetu, tunajionea ukweli wa ahadi hii ya Yehova kwa watumishi wake: “Nitakutia nguvu. Nitakusaidia kwelikweli.” (Isa. 41:10) Kwa hiyo, urafiki wetu pamoja na Yehova unakuwa wenye nguvu zaidi. Zaidi ya hilo, kujitoa kwa kujipendea​—katika eneo kwenye tunaishi ao katika inchi ingine, kunatutayarisha kwa ajili ya kazi ya kiteokrasi yenye tunangojea kufanya katika dunia mupya. Kama vile Didier mwenye tulizungumuzia mwanzoni anasema, “kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri kunatupatia mazoezi mazuri kwa ajili ya wakati wenye kuja!” Basi wafanyakazi wengi wenye kujitoa waanze mazoezi hayo hivi karibuni!

^ fu. 4 Wahubiri hao wenye kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri wametoka katika inchi ya Kanada, République Tchèque, Ufaransa, Ujerumani, Guadeloupe, Luxembourge, Nouvelle-Calédonie, Suède, Uswisi, Uingereza, na Amerika.

^ fu. 8 Masomo kwa Ajili ya Waeneza Injili wa Ufalme yamechukua nafasi ya masomo hayo. Watumishi wa wakati wote wenye kutumikia katika inchi zingine wenye kutimiza mambo yenye kuombwa wanaweza kuomba kusoma Masomo kwa Ajili ya Waeneza Injili wa Ufalme katika inchi kwenye wametoka ao katika inchi ingine kwenye masomo hayo wanafanywa katika luga yao ya kizalikio.