Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mwisho Utafika Wakati Gani? Mambo Yesu Alisema

Mwisho Utafika Wakati Gani? Mambo Yesu Alisema

Sawa vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, wakati Biblia inazungumuzia mwisho wa dunia, haionyeshe kama ni mwisho wa hii planete yetu ao mwisho wa wanadamu wote. Lakini, inapenda tu kuonyesha mwisho wa mambo yote ya mubaya yenye tuko naona mu dunia leo na mwisho wa wale wote wenye wako wanaiunga mukono. Lakini, Biblia ilishaonyesha ni siku gani hii mambo yote ya mubaya itaisha?

FIKIRIA MAMBO MBILI YENYE YESU ALIZUNGUMUZIA KUHUSU MWISHO:

“Kwa hiyo, muendelee kukesha, kwa sababu hamujue siku wala saa.”​—MATAYO 25:13.

“Mufanye angalisho, muendelee kukesha, kwa maana hamujue wakati wenye uliwekwa utafika wakati gani.”​—MARKO 13:33.

Hapa ku dunia, hakuna mutu mwenye anajua kabisa wakati mwisho utafika. Lakini, tayari Mungu alishachagua “wakati wenye uliwekwa,” ni kusema, “siku na saa” ya mwisho kufika. (Matayo 24:36) Ile inaonyesha kabisa kama hakuna namna tunaweza kujua kama mwisho uko karibu? Hapana. Yesu alionyesha wanafunzi wake matukio fulani yenye ingewasaidia wajue kama mwisho unakaribia.

ALAMA

Hii matukio, njo ingekuwa alama ya “umalizio wa mupangilio wa mambo (dunia).” Yesu alisema hivi: “Taifa litasimama kupigana na taifa na Ufalme kupigana na Ufalme, na kutakuwa upungufu wa chakula na matetemeko ya inchi mahali pamoja kisha pengine.” (Matayo 24:3, 7) Alisema pia kama, kutakuwa “magonjwa ya kuambukiza.” (Luka 21:11) Leo uko naona matukio yenye Yesu alitabiri?

Leo watu wanateseka juu ya vita, njaa, matetemeko ya inchi, na magonjwa mbalimbali. Kwa mufano, mu 2004, matetemeko ya inchi ya nguvu sana yenye ilitokea mu bahari ya India ilitokeza tsunami yenye iliua watu 225 000 hivi. Mu miaka tatu, ugonjwa wa Coronavirus uliua watu milioni 6.9 hivi mu dunia yote. Yesu alisema kama matukio ya vile, itaonyesha kama tuko karibu na mwisho wa dunia.

“SIKU ZA MWISHO”

Biblia inaita kipindi yenye inatangulia mwisho, kuwa “siku za mwisho.” (2 Petro 3:3, 4) 2 Timoteo 3:1-5 inaonyesha kama mu siku za mwisho watu watakuwa na mwenendo mubaya sana. (Ona kisanduku “ Mbele tu Mwisho Ufike.”) Leo uko naona watu wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda jeuri, na wenye hawaonyeshane upendo? Ile pia inaonyesha kama mwisho uko karibu sana.

Siku za mwisho zitafanya masiku ngapi? Biblia inaonyesha kama, zitakamata “kipindi kifupi cha wakati.” Kisha, Mungu ataharibu “wale wenye wanaharibu dunia.”​—Ufunuo 11:15-18, maelezo ya chini; 12:12.

DUNIA PARADISO IKO KARIBU!

Tayari Mungu alishaweka siku na saa yanye atamaliza mambo yote ya mubaya yenye kuwa mu hii dunia. (Matayo 24:36) Lakini, kuko habari njema. Mungu “hataki mutu yeyote aharibiwe.” (2 Petro 3:9) Iko anapatia wanadamu nafasi ya kujifunza kuhusu mapenzi yake na kumutii. Juu ya nini? Juu anapenda tuokoke na tuishi mu dunia mupya yenye itakuwa paradiso.

Mungu iko anaongoza kazi ya kufundisha watu mu dunia yote, ili wajifunze nini wanaweza kufanya juu waishi mu dunia mupya yenye itatawaliwa na mufalme wake. Yesu alisema kama habari njema ya Ufalme wa Mungu itahubiriwa “mu dunia yote yenye kuikaliwa na watu.” (Matayo 24:14) Mu dunia yote, Mashahidi wa Yehova wanapitishaka mamiliare ya saa mu kazi ya kuhubiri na kufundisha watu ujumbe wa Biblia wenye kuleta tumaini. Yesu alisema kama ile kazi ya kuhubiri itafanyika mu dunia yote mbele mwisho ufike.

Utawala wa wanadamu unakaribia mwisho wake. Lakini habari njema ni hii: Unaweza kuokoka wakati hii dunia itafikia mwisho na kuwa mu dunia paradiso yenye Mungu ametuahidi. Habari yenye kufuata itazungumuzia namna unaweza kuishi mu ile dunia mupya.

Unabii wa Yesu kuhusu “siku za mwisho” unatupatia sababu ya kuwa na tumaini