Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulizo la 3: Sababu Gani Mungu Anaacha Niteseke?

Ulizo la 3: Sababu Gani Mungu Anaacha Niteseke?

Ulizo la 3: Sababu Gani Mungu Anaacha Niteseke?

BABA ya Ian alikuwa mulevi sana. Ijapokuwa Ian alikuwa na vitu vyote vya kimwili alivyohitaji alipoendelea kukomaa, alikosa musaada kutoka kwa baba yake ambao ungemusaidia awe na utulivu wa moyoni na akilini. Ian anasema hivi: “Sikumupenda hata kidogo, zaidi sana kwa sababu ya ulevi wake na namna alivyokuwa anamutendea mama yangu.” Ian alipokomaa, alianza kushakia ikiwa Mungu iko. Niliwaza hivi: “Ikiwa Mungu iko kabisa, sababu gani anawaacha watu wateseke?”

Sababu gani tunajiuliza ulizo hilo? Hata ikiwa haupatwe na mateso katika maisha yako, kwa sababu ya kupenda haki unaweza kukasirika unapoona watu wasio na kosa wanateseka. Hata hivyo, kama Ian, unaweza kujiuliza maulizo mengi juu ya mateso, zaidi sana wakati unapambana na taabu ao wakati mutu fulani unayemupenda anagonjwa ao anakufa.

Watu fulani wamejibu ulizo hilo namna gani? Watu fulani wanaamini kama Mungu anatuacha tuteseke ili kutujaribu na kutufundisha kuwa wanyenyekevu na wenye huruma. Wengine wanawaza kama watu wanateseka kwa sababu ya makosa waliyotenda katika maisha yao ya wakati uliopita.

Majibu hayo yanaonyesha nini? Yanaonyesha kama ni vigumu kumupenda Mungu kwa sababu hatuhangaikie na hana huruma.

Biblia inafundisha nini? Biblia inafundisha waziwazi kama mateso yanayowapata watu si mapenzi ya Mungu. Inasema hivi: ‘Mutu akiwa chini ya jaribu, yeye asiseme: Mungu ananijaribu. Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na mambo maovu wala yeye mwenyewe hamujaribu yeyote.’ (Yakobo 1:13) Kwa kweli, kusema kama mateso yanayowapata watu ni mapenzi ya Mungu, hakupatane na mambo ambayo Biblia inafundisha juu ya sifa za Mungu. Sababu gani?

Upendo ni sifa moja kati ya sifa kubwa za Mungu. (1 Yohana 4:8) Ili kukazia jambo hilo, Biblia inamufananisha Mungu na mama mwenye kunyonyesha. Inauliza hivi: ‘Je, muke anaweza kumusahau mutoto wake anayenyonya hivi kwamba asimuhurumie mwana wa tumbo lake? Hata hawa wanawake wanaweza kusahau, lakini mimi mwenyewe sitakusahau wewe.’ (Isaya 49:15) Je, unawaza kama mama mwenye upendo anaweza kumutesa kimakusudi mutoto wake? Hapana, muzazi mwenye upendo anatuliza mateso ya mutoto wake. Vilevile, Mungu, anayefananishwa na muzazi, hawaletee watu mateso.​—Mwanzo 18:25.

Hata hivyo, watu wanaendelea kuteseka. Unaweza kujiuliza, ‘Ikiwa Mungu anatuhangaikia na ikiwa ni Mweza​-yote, sababu gani hamalize mateso?’

Kuna sababu fulani zinazomufanya Mungu aache mateso yaendelee. Tuzungumuzie sababu moja tu: Kwa kawaida ni watu ndio wanaoletea wengine mateso. Viongozi wengi wanaoonea watu na kuwaletea mateso hawatake kubadilika. Kwa hiyo, ili kumaliza mateso, Mungu atawaharibu watu kama hao.

Mutume Petro alieleza sababu gani Mungu hajaharibu watenda mabaya. Aliandika hivi: ‘Yehova hakawie kuhusiana na ahadi yake, kama watu fulani wanavyoona kukawia, bali yeye ni mwenye subira kwenu kwa sababu hatake yeyote aangamizwe bali anataka wote wafikie toba.’ (2 Petro 3:9) Uvumilivu wa Yehova Mungu unaonyesha kama yeye ni mwenye upendo na mwenye huruma.

Hata hivyo, Yehova Mungu atatenda hivi karibuni. Atawaharibu wale wanaowatesa watu wasio na kosa. Watu hao wanaowatesa wengine ‘watahukumiwa azabu ya uharibifu wa milele.’​—2 Wathesalonike 1:6-9.

Ian, aliyetajwa mwanzoni mwa habari hii, alipata majibu yenye kufurahisha kwa maulizo aliyokuwa anajiuliza juu ya mateso. Mambo aliyojifunza yalimusaidia kubadilisha mawazo yake. Usome habari yake kwenye ukurasa wa 13 wa gazeti hili.

Ili kujua mengi juu ya sababu zinazomufanya Mungu aache mateso yaendelee na namna atakavyoyamaliza, usome sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Unaweza pia kupakua kitabu hicho kwenye adresi yetu ya Internete www.ps8318.com

[Sanduku katika ukurasa wa 9]

Yesu Alifundisha Nini juu ya Mateso Yanayowapata Watu?

Yesu hakusema kama mateso yanayowapata watu ni mapenzi ya Mungu.

Alifundisha kwamba Mungu hawatese watu ili kuwapatia malipizi. Yesu aliponyesha wagonjwa, vilema, na vipofu. (Mathayo 15:30) Miujiza ambayo Yesu alifanya inatufundisha mambo haya mawili ya lazima: Jambo la kwanza, Yesu alitumia nguvu ya Mungu ili kutuliza mateso, lakini si kuyatokeza. Jambo la pili, huruma ndiyo ilimuchochea Yesu kuponyesha watu. Alipoona watu waliokuwa wanateseka, aliwasikilia huruma. (Mathayo 20:29-34) Yesu alionyesha kabisa namna Baba yake anavyojisikia anapoona watu wanateseka. Kwa hiyo, kupitia maneno na matendo yake, tunajifunza kwamba Mungu anaumizwa moyoni anapoona watu wanateseka na anataka kumaliza mateso.​—Yohana 14:7, 9.

Alionyesha kwamba mateso mengi ya wanadamu yanaletwa na Shetani Ibilisi. Yesu alisema kama Shetani “alikuwa muuaji alipoanza.” (Yohana 8:44) Tena, alionyesha kama Shetani Ibilisi ndiye ‘mutawala wa ulimwengu huu,’ yule “anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa.”​—Yohana 12:31; Ufunuo 12:9.

Alitutolea tumaini la wakati ambapo mateso yote yataisha. Aliwafundisha wafuasi wake kusali hivi: “Baba yetu uliye mbinguni, . . . Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.” (Mathayo 6:9, 10) Wakati Ufalme wa Mungu utakuja, mateso hayatakuwa tena duniani, hali itakuwa kama ilivyo mbinguni.

Katika ufunuo ambao alimupatia mutume Yohana, Yesu alionyesha namna maisha ya watu watakaotawaliwa na Ufalme wa Mungu yatakuwa. Wakati huo, Mungu “[atapanguza] kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”​—Ufunuo 1:1; 21:3, 4.