Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kitu cha Maana Sana cha Zamani Kinaokotwa Kwenye Uchafu

Kitu cha Maana Sana cha Zamani Kinaokotwa Kwenye Uchafu

NI NINI inakuja katika akili yako wakati unawaza juu ya rundo la uchafu? Pengine unaona kuwa mahali kama hapo kunapaswa kuwa uchafu na harufu mbaya. Kwa hiyo, hauwezi kuwazia kama unaweza kupata kitu cha maana mahali hapo, zaidi sana kitu cha bei kubwa sana.

Lakini, kumepita miaka mia moja tangu kitu kama hicho kilivumbuliwa nafasi kama hiyo, ni kusema, kwenye uchafu. Kitu hicho cha bei sana hakikukuwa utajiri wa kawaida lakini kitu fulani cha maana zaidi. Ni kitu gani? Sababu gani kuvumbuliwa kwa kitu hicho ni kwa maana kwetu leo?

KINAPATIKANA BILA KUTAZAMIA

Kwenye mwanzo wa miaka kati ya 1901 na 2000, Bernard Grenfell na Arthur Hunt, watu wenye elimu kwenye Masomo ya Juu ya Oxford, walitembelea Misri. Huko, katika marundo ya uchafu karibu na Bonde la Muto Nile, walivumbua vipande fulani vya karatasi za mafunjo (papyrus). Kisha hapo, katika mwaka wa 1920, wakati wanaume hao wawili walikuwa wanafanya liste ya vitu walikuwa navyo, Grenfell alipata vipande vingine vya karatasi za mafunjo vyenye vilichimbuliwa Misri. Alivitolea maktaba ya John Rylands ya Manchester, Uingereza. Lakini, wanaume hao wawili walikufa mbele ya kumaliza liste hiyo.

Colin Roberts, mutu mwengine mwenye elimu kwenye Masomo ya Juu ya Oxford, alimaliza liste hiyo. Wakati alikuwa anapanga vipande hivyo, alipata kipande kidogo cha karatasi chenye kuwa na ukubwa wa santimetre 9 juu ya 6. Alishangaa kuona kuwa maandishi hayo ya Kigiriki yaliyoandikwa kwa mukono yalikuwa na maneno fulani yenye alijua. Kwenye upande moja, kulikuwa maneno fulani ya andiko la Yohana 18:31-33. Kwenye upande mwengine, kulikuwa sehemu fulani za mistari ya 37 na 38. Roberts alitambua kuwa alikuwa amepata kitu cha maana sana.

KILIANDIKWA WAKATI GANI?

Roberts aliwazia kuwa kipande hicho cha karatasi ya mafunjo kiliandikwa zamani sana. Lakini, kiliandikwa wakati gani? Ili kujua, alilinganisha maandishi ya mukono yenye yalikuwa kwenye kipande hicho na maandishi mengine ya zamani yenye yalikuwa na tarehe; sayansi hiyo inaitwa paliografia. * Kwa kutumia njia hiyo, angeweza kukadiria ikiwa kipande hicho cha karatasi kiliandikwa wakati gani. Lakini alipenda kupata uhakika. Kwa hiyo, alikamata picha za kipande hicho, akazitumia watu watatu wenye kujifunza maandishi kwenye karatasi za mafunjo na kuwaomba watafute kujua kiliandikwa wakati gani. Watu hao walisema nini?

Watu hao watatu wenye elimu walichunguza namna maandishi yalipangwa, na muandiko, na wote walikubaliana kama kipande hicho kiliandikwa katika mwaka wa 125 hivi K.K.Y., miaka fulani tu kisha kifo cha mutume Yohana! Hata hivyo paliografia haiko njia ya hakika kabisa ya kujua ni wakati gani maandishi fulani yaliandikwa; mutu mwengine mwenye elimu alisema kama inawezekana maandishi hayo yaliandikwa wakati wowote kati ya mwaka wa 101 na 200. Lakini kipande hicho kidogo cha karatasi ndiyo ilikuwa na ingali maandishi ya zamani zaidi ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yenye imekwisha kupatikana.

KIPANDE CHA KARATASI CHA RYLANDS KINAONYESHA NINI?

Sababu gani kipande hicho cha karatasi cha Injili ya Yohana ni cha maana sana kwa watu wenye wanapenda Biblia leo? Kuna sababu mbili hivi. Sababu ya kwanza, namna kipande hicho kilikuwa inatusaidia kujua kama Wakristo wa kwanza waliona Maandiko kuwa ya maana.

Sababu gani kipande cha karatasi cha Injili ya Yohana ni cha maana sana kwa watu wenye wanapenda Biblia leo?

Kati ya mwaka wa 101 na 200 K.K.Y., kulikuwa maandishi ya namna mbili: vitabu vya kukunjwa na kodeksi. Vitabu vya kukunjwa vilikuwa vipande vya makaratasi ya mafunjo ao vipande vya ngozi vyenye viliunganishwa ao kushonwa pamoja ili kufanya karatasi moja ndefu. Karatasi hiyo ingeweza kukunjwa na kukunjuliwa wakati wowote ilikuwa lazima. Mara nyingi, kitabu cha kukunjwa kilikuwa na maandishi kwenye upande moja tu.

Lakini, kipande kidogo cha karatasi chenye Roberts alivumbua kilikuwa na maandishi ya mukono kwenye pande zote mbili. Hilo linaweza kuonyesha kuwa kilitoka katika kodeksi lakini haiko katika kitabu cha kukunjwa. Kodeksi ilitengenezwa kwa kushona pamoja vipande vya makaratasi ya mafunjo ao vya ngozi ili kufanya kitu chenye kufanana kitabu cha leo.

Kulikuwa faida gani ya kutumia kodeksi kuliko kutumia kitabu cha kukunjwa? Kwa kweli, Wakristo wa kwanza walikuwa waeneza-injili. (Mathayo 24:14; 28:19, 20) Walikuwa wanahubiri ujumbe wa Biblia kila mahali walikuta watu, ni kusema, nyumbani, katika masoko, na kwenye barabara. (Matendo 5:42; 17:17; 20:20) Kwa hiyo, kuwa na Maandiko katika kitabu kidogo kulikuwa na faida sana.

Pia kodeksi iliwezesha makutaniko na watu kuwa na kopi zao wenyewe za Maandiko. Kwa hiyo, Injili zilifanyiwa kopi tena na tena, na hilo lilisaidia ili Ukristo uenee haraka.

Kipande Cha Karatasi Cha Rylands Upande wa mbele na wa nyuma

Sababu ya pili yenye kufanya kipande cha karatasi cha Rylands kikuwe cha maana kwetu leo ni hii: Kinatuonyesha kuwa maandishi ya kwanza-kwanza ya Biblia yalienezwa kwa uaminifu. Kipande hicho kiko na maandiko kidogo tu ya Injili ya Yohana, lakini maneno ya maandiko hayo yako karibu sawa na yale yenye kuwa katika Biblia zetu leo. Kwa njia hiyo, kipande cha karatasi cha Rylands kinaonyesha kama habari ya Biblia haijabadilishwa hata kama imeandikwa tena na tena kwa muda murefu.

Bila shaka, kuna maelfu ya maandishi na vipande vya maandishi vyenye kuonyesha kuwa ujumbe wa kwanza-kwanza wa Biblia ulienezwa kwa uaminifu; kipande cha Rylands cha Injili ya Yohana ni kimoja tu kati ya hivyo. Katika kitabu chake, Werner Keller alisema hivi: “[Maandishi] hayo ya zamani yanahakikisha zaidi kama Biblia zetu za leo ni za kweli na hazikubadilishwa.” (The Bible as History)

Kwa kweli, imani yetu sisi Wakristo haitegemee vitu vya zamani vyenye kuvumbuliwa. Tunaamini kuwa “andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Timotheo 3:16) Hata hivyo, tunatiwa moyo sana kuona kuwa kitu hicho cha maana sana cha zamani kinahakikisha maneno haya yenye Biblia ilisema tangu zamani: “Neno la Yehova linadumu milele”!—1 Petro 1:25.

^ fu. 8 Kitabu kimoja kinasema kuwa “paliografia . . . ni sayansi yenye kujifunza maandishi ya zamani.” (Manuscripts of the Greek Bible) Kisha wakati fulani, namna ya kuandika kwa mukono inabadilika. Mabadiliko hayo yanaweza kuonyesha maandishi fulani yaliandikwa wakati gani, ikiwa yanaweza kulinganishwa na maandishi mengine yenye kuwa na tarehe ya hakika.