Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Siku ya Hukumu ni nini?

Sababu gani siku ya hukumu itakuwa wakati wa furaha?

Wakati wa zamani, Mungu alitumia waamuzi ili kuokoa watu wake wasitendewe tena bila haki. (Waamuzi 2:18) Biblia inasema kama Siku ya Hukumu ya wakati unaokuja itakuwa wakati wa furaha. Wakati huo Yehova, Muamuzi wa dunia yote, ataokoa wanadamu ili wasitendewe tena bila haki.—Soma Zaburi 96:12, 13; Isaya 26:9.

Mungu amemuchagua Yesu ili awahukumu kwa haki watu wazima na watu waliokufa. (Matendo 10:42; 17:31) Watu wengi wamekufa bila kumujua Mungu. Katika Siku ya Hukumu, Yesu atafufua watu hao ili wapate nafasi ya kumujua Mungu wa kweli na kumupenda.—Soma Matendo 24:15.

Sababu gani Siku ya Hukumu itafanya miaka elfu moja?

Watu waliokufa watafufuliwa katika kipindi cha miaka elfu moja. (Ufunuo 20:4, 12) Watakuwa na lazima ya wakati ili waweze kujifunza sheria za Mungu na kumutii. Tofauti na mawazo ya watu wengi, Biblia inaonyesha kama watu watahukumiwa kulingana na mambo yenye watafanya kisha kufufuliwa.—Soma Waroma 6:7.

Biblia inazungumuzia siku ya hukumu yenye itatokea bila watu kuwazia mbele ya ile miaka elfu moja kuanza. Kama vile habari kubwa ya gazeti hili inaonyesha, siku hiyo inaitwa pia mwisho. Katika siku hiyo, Mungu ataharibu watu wote wenye hawamuogope, ni kusema, watu wabaya. (2 Petro 3:7) Kwa hiyo, ni lazima tuonyeshe kama tunamupenda Mungu.—Soma 2 Petro 3:9, 13.