Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | MWISHO UNAKARIBIA?

“Mwisho”—Unamaanisha Nini?

“Mwisho”—Unamaanisha Nini?

Wakati unasikia maneno “Mwisho unakaribia!” ni nini inakuja katika akili yako? Unafikiria muhubiri mwenye kuwa kwenye jukwaa na iko na Biblia katika mukono, anafundisha kwa sauti kubwa na anafanya ishara nyingi za mwili? Ao unafikiria mwanaume fulani mwenye kuwa na ndevu nyingi na amevaa kanzu ndefu yenye kufungwa kamba kwenye kiuno, amesimama pembeni ya njia na anaonyesha watu alama fulani yenye kuonyesha mwisho wa dunia? Wakati watu fulani wanafikiria hali kama hizo wanaogopa, lakini wengine wanakuwa na mashaka ao hata wanaona kuwa ni habari za kuchekesha tu.

Biblia inasema hivi: ‘Mwisho utakuja.’ (Mathayo 24:14) Mwisho unaitwa pia ‘siku kubwa ya Mungu’ na “Har-Magedoni.” (Ufunuo 16:14, 16) Kwa kweli, dini zinafundisha mambo yenye kutofautiana juu ya mwisho, na jambo la kushangaza ni kwamba, mafundisho mengi yenye haiko wazi yanaongezeka. Lakini Biblia yenyewe inaeleza mambo waziwazi juu ya mwisho; inaonyesha mwisho unamaanisha nini na mwisho haumaanishe nini. Pia Neno la Mungu linatusaidia kujua waziwazi ikiwa mwisho unakaribia ao hapana. Na zaidi ya yote, linatuonyesha mambo tunaweza kufanya ili tuokoke! Kwanza kabisa, acha tuondoe mawazo yasiyo ya kweli na tuonyeshe mwisho unamaanisha nini. Biblia inasema “mwisho” unamaanisha nini kabisa?

MWISHO HAUMAANISHE NINI?

  1. MWISHO HAIKO UHARIBIFU MUKUBWA WA DUNIA KUPITIA MOTO.

    Biblia inasema hivi: ‘[Mungu] ameiwekea dunia musingi juu ya mahali pake palipofanywa imara; haitatikiswa mupaka wakati usio na kipimo, ao milele.’ (Zaburi 104:5) Andiko hilo, na maandiko mengine yanatuhakikishia kama Mungu hataharibu dunia wala hataruhusu dunia iharibiwe hata siku moja!—Mhubiri 1:4; Isaya 45:18.

  2. MWISHO HAIKO TUKIO LENYE LITATOKEA BILA KUPANGWA.

    Biblia inasema kuwa mwisho umepangwa; Mungu amekwisha kupanga ni wakati gani kabisa mwisho utakuja. Inasema hivi: ‘Kuhusu siku ile au saa ile hakuna mutu anayejua, wala malaika mbinguni wala Mwana, ila Baba. Muendelee kutazama, muendelee kukesha, kwa maana hamujue wakati uliowekwa ni gani.’ (Marko 13:32, 33) Ni wazi kuwa, Mungu (“Baba”) amekwisha kupanga “wakati uliowekwa” ambapo ataleta mwisho.

  3. MWISHO HAUTALETWA NA WATU AO NA VITU HATARI VYENYE KUANGUKA KUTOKA ANGANI.

    Mwisho utaletwa na nini? Andiko la Ufunuo 19:11 linasema hivi: “Nikaona mbingu imefunguliwa, na, tazama! farasi mweupe. Na yeye aliyeketi juu yake anaitwa Mwaminifu na wa Kweli.” Mustari wa 19 unaongezea hivi: ‘Nami nikamuona yule munyama-mwitu na wafalme wa dunia na majeshi yao wamekusanyika pamoja ili kupigana vita na yule anayeketi juu ya farasi na jeshi lake.’ (Ufunuo 19:11-21) Maneno mengi yenye kutumiwa katika maandiko hayo ni ya mufano, lakini tunaelewa jambo hili: Mungu atatuma jeshi la malaika ili likuje kuangamiza maadui wake.

Habari yenye Biblia inasema juu ya mwisho haiko habari ya mubaya lakini ni habari ya muzuri

MWISHO UNAMAANISHA NINI?

  1. MWISHO WA SERIKALI ZA WATU ZENYE ZIMESHINDWA.

    Biblia inasema hivi: ‘Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme [serikali] ambao hautaharibiwa kamwe. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama mupaka wakati usio na kipimo.’ (Danieli 2:44) Kama vile tumeona katika habari hii, “wafalme wa dunia na majeshi yao” wenye ‘watakusanyika pamoja ili kupigana vita na yule anayeketi juu ya farasi na jeshi lake,’ wataharibiwa kabisa.—Ufunuo 19:19.

  2. MWISHO WA VITA, JEURI, NA UKOSEFU WA HAKI.

    ‘[Mungu] atakomesha vita mupaka kwenye mwisho wa dunia.’ (Zaburi 46:9) ‘Wanyoofu ndio watakaa duniani, na wasio na lawama [kosa] ndio watakaobaki ndani yake. Nao waovu, watakatiliwa mbali kutoka duniani; nao wenye hila, watangolewa kutoka ndani yake.’ (Methali 2:21, 22) “Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.”—Ufunuo 21:4, 5.

  3. MWISHO WA DINI ZENYE ZIMEMUKOSEA MUNGU NA WATU.

    “Manabii wanatabiri uwongo, na makuhani wanatawala kwa maongozi yao. . . . Nanyi mutafanya nini wakati mwisho utakapofika?” (Yeremia 5:31, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo) ‘Wengi wataniambia siku hiyo: Bwana, Bwana, hatukutoa unabii katika jina lako, na kufukuza roho waovu katika jina lako, na kufanya matendo mengi yenye nguvu katika jina lako? Na hata hivyo nitawaambia waziwazi: Sikuwajua ninyi kamwe! Muondoke kwangu, ninyi wenye matendo ya uasi-sheria.’—Mathayo 7:21-23.

  4. MWISHO WA WATU WENYE WANAENDELESHA NA KUUNGA MUKONO HALI YENYE KUWA KATIKA ULIMWENGU LEO.

    Yesu Kristo alisema hivi: ‘Basi huu ndio musingi wa hukumu, kwamba nuru imekuja ulimwenguni lakini watu wamelipenda giza kuliko nuru, kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.’ (Yohana 3:19) Biblia inazungumuzia uharibifu wenye ulifanyika katika dunia yote wakati wa Noa, mwanaume mwenye imani. ‘Ulimwengu wa wakati huo uliangamia kwa garika ya maji. Lakini kwa neno hilohilo mbingu na dunia za sasa zimewekwa akiba kwa ajili ya moto nazo zinahifaziwa mupaka ile siku ya hukumu na ya kuangamizwa kwa watu wasiomwogopa Mungu.’—2 Petro 3:5-7.

Umeona kuwa “siku ya hukumu na ya kuangamizwa” ya wakati unaokuja inalinganishwa na uharibifu wa “ulimwengu” wa wakati wa Noa. Ni ulimwengu gani uliharibiwa? Dunia haikuharibiwa, lakini ni “watu wasiomwogopa Mungu,” ni kusema, maadui wa Mungu ndio ‘waliangamizwa.’ Katika “siku ya hukumu” yenye Mungu ataleta wakati unaokuja, watu wenye wanachagua kuwa maadui wa Mungu wataharibiwa pia. Lakini Mungu ataokoa marafiki wake kama vile aliokoa Noa na familia yake.—Mathayo 24:37-42.

Wazia namna dunia itakuwa muzuri sana wakati Mungu atakuwa ameharibu watu wabaya wote! Ni wazi kwamba, habari yenye Biblia inasema juu ya mwisho haiko habari ya mubaya lakini ni habari ya muzuri. Hata hivyo, unaweza kujiuliza hivi: ‘Biblia inatuonyesha ni wakati gani mwisho utakuja? Mwisho unakaribia? Namna gani ninaweza kuokoka wakati mwisho utafika?’