Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | MASHAHIDI WA YEHOVA NI NANI?

Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Namna Gani?

Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Namna Gani?

Tuko tengenezo la duniani pote lenye halijiunge na dini zingine. Hata kama makao yetu makubwa yanapatikana katika inchi ya Amerika, Mashahidi wengi wa Yehova wanaishi katika inchi zingine. Mashahidi wa Yehova milioni munane hivi wanafundisha watu Biblia katika inchi zaidi ya 230. Tunafanya hivyo ili kutii maneno haya ya Yesu: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote.”—Mathayo 24:14.

Kila mahali kwenye tunaishi, zamiri yetu inatuchochea kuheshimu sheria ya inchi. Lakini tunajikaza sana ili tusijiingize katika mambo ya siasa. Hiyo ni kwa sababu tunafuata muongozo wa Yesu wenye kuonyesha kuwa Wakristo “si sehemu ya ulimwengu.” Ndiyo sababu hatujiingize katika mambo ya siasa ao kuunga mukono vita. (Yohana 15:19; 17:16) Wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, Mashahidi wa Yehova walifungwa, waliteswa, na hata kuuawa kwa sababu walikataa kabisa kujiingiza katika vita. Askofu fulani wa zamani wa Ujerumani aliandika hivi: “Wako na haki ya kusema kama wao tu ndio kikundi kikubwa cha dini chenye, kwa sababu ya zamiri, kilikataa kujiunga na vita wakati wa utawala wa Nazi.”

Hata hivyo, hatujitenge na wengine. Yesu alisali hivi kwa Mungu juu ya wanafunzi wake: “Ninakuomba, si kwamba uwatoe ulimwenguni.” (Yohana 17:15) Ndiyo sababu unaweza kuona tunafanya kazi, tunaenda kununua vitu, na tunaenda kwenye masomo pamoja na watu wengine.

“[Mashahidi wa Yehova] wako na nguvu nyingi za kufuata kanuni za mwenendo. Tungetumikisha watu hao wasiojipenda wenyewe katika kazi kubwa-kubwa za kisiasa, lakini hakuna siku tutaweza kufanya hivyo. . . . Wanatambua mamlaka za serikali lakini wanaamini kama Ufalme wa Mungu tu ndio unaweza kumaliza magumu yote ya wanadamu”.—Gazeti Nová Svoboda, Czech Republic.