Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA

Mashahidi wa Yehova Ni Nani?

Mashahidi wa Yehova Ni Nani?

“Nilikuwa nimejua Mike kwa miaka mingi. Yeye ni Shahidi wa Yehova. Lakini sikuzote dini yake ilikuwa inanishangaza. Yehova ni nani? Sababu gani Mashahidi wa Yehova hawafanye sikukuu mbalimbali? Mike alijiunga katika kikundi kidogo cha kidini?”—Becky, Kalifornia, inchi ya Amerika.

“Wakati majirani wangu walianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova, nilijiuliza hivi: ‘Jina Mashahidi wa Yehova linamaanisha nini? Hilo ni jina lisilokuwa la kawaida kwa dini!’”—Zenon, Ontario, Kanada.

“Mimi na bibi yangu tuliwaza kama Mashahidi wa Yehova walitutembelea ili kutuonyesha kama tulifanya makosa kwa sababu hatukukuwa tunaenda kwenye kanisa. Na tuliwaza kama ikiwa dini kubwa-kubwa hazikukuwa na kitu chenye tulikuwa tunatafuta, dini ndogo isiyokuwa ya kawaida kama vile ya Mashahidi wa Yehova haingekuwa pia na kitu hicho.”—Kent, Washington, inchi ya Amerika.

“Kwa kweli, sikujua Mashahidi wa Yehova ni nani, na wanaamini nini.”—Cecilie, Esbjerg, Danemark.

Pengine umewaona wanahubiri nyumba kwa nyumba ao mahali pa watu wengi, wanagawanya vichapo vyenye kuzungumuzia Biblia na wanaomba kufundisha watu Biblia bila kulipa. Labda mumoja wao ndiye alikupatia gazeti hili. Lakini, unaweza kuendelea kujiuliza ikiwa Mashahidi wa Yehova ni nani. Inawezekana uko na mawazo kama ya mutu mumoja kati ya watu wenye tumetaja juu.

Ikiwa uko na maulizo na mawazo kama hayo, unaweza kupata wapi majibu? Namna gani unaweza kujua mambo yenye Mashahidi wa Yehova wanaamini kabisa, namna wanapata feza za kusaidia kazi yao iendelee na za kujenga mahali pao pa ibada, na sababu gani wanakutembelea nyumbani kwako na kuzungumuza na wewe mahali pa watu wengi?

Cecilie, mwenye tumekwisha kutaja anasema hivi: “Nilisoma mambo mengi juu ya Mashahidi wa Yehova kwenye Internete. Nilisikiliza habari za kuwazia na mawazo ya watu wenye ubaguzi juu yao. Hilo lilinifanya nikuwe na mawazo mabaya juu ya Mashahidi wa Yehova.” Lakini, baadaye alizungumuza moja kwa moja na Mashahidi wa Yehova na akapata majibu yenye kusadikisha juu ya maulizo yake.

Ungependa kupata majibu ya kweli ya maulizo yako juu ya Mashahidi wa Yehova? Tunakutia moyo uulize watu wenye kujua muzuri, ni kusema, Mashahidi wa Yehova wenyewe, ambao wanachapisha gazeti hili. (Methali 14:15) Tunatumainia kama habari zenye kufuata zitakusaidia kujua sisi Mashahidi wa Yehova ni nani, mambo tunaamini, na kuelewa kazi yenye tunafanya.