Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unafiki! Utaisha Siku Fulani?

Unafiki! Utaisha Siku Fulani?

ANAYIOTA alikomalia katika kisiwa kimoja cha Mediterania. Wakati alikuwa kijana, alipendezwa sana na mambo ya siasa. Kisha alikuwa mwandishi wa kikundi fulani cha siasa katika kijiji chao. Alienda hata nyumba kwa nyumba juu ya kutafuta feza za kusaidia kikundi hicho cha siasa. Lakini kisha wakati fulani, Panayiota alivunjika moyo. Hata kama watu wa kikundi hicho waliitana marafiki, mambo kama vile kupendelea watu wa jamaa, kupenda mambo makubwa, kukosa kuelewana, na wivu yaliendelea.

Daniel alikomalia katika inchi ya Irelandi katika familia yenye ilipenda dini sana. Jambo la huzuni ni kwamba anaendelea kukumbuka unafiki wa mapadri wenye walikunywa pombe sana, walicheza michezo ya feza, na kuiba feza kwenye sahani ya sadaka, na wakati huohuo walimuhubiria kama akifanya zambi, ataunguzwa katika moto.

Kwa miaka mingi, Jeffery alitumikia kompanyi moja ya mashua yenye kuwa na biro katika inchi ya Uingereza na Amerika. Kazi yake ilikuwa kuuzisha na kutangazia watu biashara za kompanyi hiyo. Anakumbuka namna mara nyingi watu wenye kuuza ao wenye kushindana nao walidanganya wakati walikuwa wanazungumuza na wakubwa wa serikali. Kwa unafiki, watu hao walikuwa tayari kusema jambo lolote ili kulinda mapatano yao.

Jambo la kuhuzunisha ni kwamba kuko mifano mingi zaidi ya hiyo. Leo unafiki unaenea sana katika karibu kila sehemu ya maisha ya wanadamu: siasa, dini, na biashara. Kwa kufaa, neno lenye kutafsiriwa “unafiki” linatokana na neno la Kigiriki lenye kumaanisha musemaji ao muchezaji mwenye kuwa mbele ya watu, mara nyingi mwenye kujifunika uso. Lakini kisha muda fulani, neno hilo lilikuja kumaanisha mutu yeyote mwenye kujifanya namna haiko ili kudanganya wengine ao kutimiza mipango ya kutafuta faida zake mwenyewe.

Wale wenye kutendewa kwa unafiki wanaweza kujisikia mubaya sana katika moyo, wanaweza kusikia mambo kama vile uchungu, kasirani, na kinyongo. Kwa sababu ya kuvunjika moyo, watu wenye kutendewa kwa unafiki wanaweza kujiuliza hivi: “Unafiki! Utaisha siku fulani?” Jambo la kufurahisha ni kwamba, Neno la Mungu linatupatia sababu za kuamini kama unafiki utaisha.

NAMNA MUNGU NA MWANA WAKE WANAONA UNAFIKI

Biblia inaonyesha kama unafiki haukuanzishwa na wanadamu, lakini ulianzishwa na kiumbe wa roho asiyeonekana. Katika mwanzo wa historia ya wanadamu, ili kumudanganya mwanamuke wa kwanza, Eva, Shetani Ibilisi alitumia nyoka ili kujificha na akajionyesha kuwa alitaka kumusaidia. (Mwanzo 3:1-5) Tangu wakati huo, watu wengi pia wamejifanya namna hawako, na wamefanya hivyo ili kudanganya wengine na kutimiza mipango ya kutafuta faida zao wenyewe.

Wakati taifa la Israeli la zamani liliingia katika mutego wa ibada ya uongo na unafiki wa kiroho, Mungu aliwaonya tena na tena juu ya matokeo mabaya ya mambo hayo. Kupitia nabii Isaya, Yehova Mungu alisema hivi: “Watu hawa wamekaribia na vinywa vyao, nao wamenitukuza kwa midomo yao mitupu, nao wameupeleka moyo wao mbali nami.” (Isaya 29:13) Wakati taifa hilo lilishindwa kubadilika, Mungu aliruhusu mataifa yenye nguvu yaharibishe nafasi kubwa ya ibada ya Israeli, ni kusema, Yerusalemu na hekalu lake. Kwanza nafasi hiyo iliharibiwa na Wababiloni katika mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, na mwishowe iliharibiwa na majeshi ya Roma katika mwaka wa 70 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Ni wazi kama Mungu havumilie unafiki milele.

Lakini Mungu na Mwana wake wanapenda sana watu wenye kutenda bila unafiki na udanganyifu. Kwa mufano, kwenye mwanzo wa utumishi wa Yesu duniani, mwanaume mumoja mwenye kuitwa Nathanaeli alimukaribia. Wakati tu Yesu alimuona, alisema hivi: ‘Ona, Muisraeli kwa uhakika, ambaye hamuna udanganyifu ndani yake.’ (Yohana 1:47) Nathanaeli, mwenye kuitwa pia Bartholomayo, alifikia kuwa kati ya mitume 12 wa Yesu.—Luka 6:13-16.

Yesu alipitisha wakati pamoja na mitume wake na aliwafundisha mawazo ya Mungu. Hawangepaswa kuwa wanafiki. Ili kuonya juu ya jambo hilo, Yesu alikemea kabisa matendo ya unafiki ya viongozi wa dini wa wakati huo. Ona matendo yao fulani.

Walitenda kwa “uadilifu [haki]” ili kujionyesha. Yesu aliambia watu wenye walikuwa wanamusikiliza hivi: ‘Mukuwe waangalifu sana kwamba musionyeshe uadilifu wenu mbele ya watu kusudi muonekane nao . . . kama vile wanafiki wanavyofanya.’ Pia aliwaambia watoe zawadi za rehema “katika siri,” ao kwa uficho. Wangepaswa kusali wakati wako peke yao, haiko tu ili kuonwa na watu wengine. Kwa kufanya hivyo, ibada yao ingekuwa yenye kutoka moyoni na ingekubaliwa na Baba yake.—Mathayo 6:1-6.

Walikuwa haraka kuhukumu wengine. Yesu alisema hivi: ‘Munafiki! Kwanza toa [ondoa] boriti lililo katika jicho lako mwenyewe, na ndipo utakapoona waziwazi jinsi ya kuutoa unyasi ulio katika jicho la ndugu yako.’ (Mathayo 7:5) Wakati mutu anakazia akili makosa ya wengine na japo yeye mwenyewe ana makosa makubwa, anajifanya aonekane namna haiko. Sababu ni kwamba, watu “wote wamefanya zambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.”—Waroma 3:23.

Walikuwa na makusudi mabaya. Siku moja, wanafunzi wa Mafarisayo na wafuasi wa kikundi cha Herode walimukaribia Yesu ili kumuuliza ulizo juu ya kodi. Kwa kutumia maneno ya kusifu-sifu, walimuambia Yesu hivi: ‘Mwalimu, tunajua wewe una ukweli nawe unafundisha njia ya Mungu katika kweli.’ Kisha wakamutilia mutego kwa kumuuliza ulizo hili: ‘Ni halali [inapatana na sheria] kumulipa Kaisari kodi ao hapana?’ Yesu akajibu hivi: ‘Kwa nini munanijaribu, enyi wanafiki?’ Yesu alikuwa na haki ya kuwaita wanafiki kwa sababu hawakukuwa wanatafuta jibu la ulizo lao kabisa, lakini walikuwa wanajaribu ‘kumutega kwa maneno yake.’​—Mathayo 22:15-22.

Wakati kutaniko la Kikristo lilianzishwa kwenye Pentekoste mwaka wa 33, watu walikuwa wanasema kweli na unafiki haukukuwa katika kutaniko. Wakristo wa kweli walijikaza sana ili wasikuwe na unafiki katika maisha yao. Kwa mufano, Petro, mumoja kati ya mitume 12 wa Yesu, aliwatia moyo Wakristo wenzake wakuwe “watiifu kwa ile kweli tokeo likiwa ni upendo wa kindugu usio na unafiki.” (1 Petro 1:​22) Mutume Paulo aliwatia moyo wafanyakazi wenzake waonyeshe ‘upendo kutokana na moyo safi na kutokana na zamiri njema na kutokana na imani bila unafiki.’—1 Timotheo 1:5.

NGUVU YA NENO LA MUNGU

Mafundisho ya Yesu na ya mitume, yenye kupatikana katika Biblia, ni yenye nguvu leo kama vile yalikuwa wakati wa mitume. Juu ya jambo hilo mutume Paulo aliandika hivi: ‘Neno la Mungu liko hai [lenye uzima] nalo lina nguvu na ni lenye makali zaidi kuliko upanga wowote wenye makali kuwili nalo linachoma hata kufikia kugawanya nafsi na roho, na viungo na urojorojo wake, nalo linaweza kutambua fikira na makusudio ya moyo.’ (Waebrania 4:12) Kujua mafundisho ya Biblia na kujikaza kuishi kulingana nayo, kumesaidia watu wengi kuachana na unafiki na kutenda bila udanganyifu. Fikiria mambo yenye watu tatu wenye kutajwa mwanzoni mwa habari hii walijionea.

Maisha ya Panayiota yalibadilika wakati alikubali kuenda kwenye mikutano katika Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova. Hakuona mutu yeyote mwenye alijionyesha kwa inje kuwa mwenye haki ili kuvutia wengine. Anasema hivi: “Hapo niliona watu wanaonyeshana upendo wa kweli na kuhangaikiana kutoka moyoni, nilikuwa sijaona jambo hilo miaka yote yenye nilikuwa katika mambo ya siasa.”

“Niliona watu wanaonyeshana upendo wa kweli na kuhangaikiana kutoka moyoni.”PANAYIOTA

Panayiota alianza kujifunza Biblia na akafanya maendeleo mupaka akafikia kubatizwa. Hiyo ilikuwa miaka 30 iliyopita. Sasa anasema hivi: “Nilipata kusudi la kweli katika maisha, haiko wakati nilikuwa ninaenda nyumba kwa nyumba ili kufanya matangazo ya kikundi cha siasa, lakini ni wakati nilianza kuhubiri juu ya Ufalme wa Mungu, njia pekee ya sisi kupata dunia yenye haki.”

“Singeendelea kuacha Wakristo wenzangu wanione namna sikukuwa.”—DANIEL

Daniel alifanya maendeleo ya muzuri katika kutaniko la Kikristo na akapewa kazi mbalimbali katika kutaniko. Kisha miaka kidogo, alifanya kosa fulani na zamiri yake ikaanza kumusumbua. Alisema hivi: “Kwa sababu niliendelea kukumbuka unafiki wenye nilikuwa nimeona katika kanisa miaka mingi iliyopita, niliona kama ni lazima niache kazi zenye nilikuwa nazo katika kutaniko. Singeendelea kuacha Wakristo wenzangu wanione namna sikukuwa.”

Jambo la kufurahisha ni kwamba, kisha muda fulani, Daniel alifanya mabadiliko na akaona kama anaweza kurudilia kazi zake katika kutaniko akiwa na zamiri safi, na kwa furaha alikubali tena kazi katika kutaniko. Sifa hiyo ya kukosa kujifanya namna mutu haiko ni ya kawaida kati ya watu wenye kutumikia Mungu bila unafiki. Wanajifunza ‘kutoa boriti’ katika jicho lao wenyewe mbele ya ‘kutoa unyasi’ katika jicho la ndugu yao.

“Sikupaswa kuendelea kuwa mutu mwenye kuuzisha kwa kutumia ujanja, mwenye kusema muzuri. . . . Zamiri yangu ilikuwa imeguswa.”—JEFFERY

Jeffery, mwenye alipitisha maisha yake katika biashara, alisema hivi: “Wakati niliendelea kuwa na ujuzi zaidi wa Biblia, nilitambua kama sikupaswa kuendelea kuwa mutu mwenye kuuzisha kwa kutumia ujanja, mwenye kusema muzuri, aliyekuwa tayari kusema jambo lolote ili kupewa mapatano ya biashara. Zamiri yangu ilikuwa imeguswa na maandiko ya Biblia kama vile Methali 11:⁠1, yenye kutuambia kama ‘mizani [kipimo] ya udanganyifu ni chukizo kwa Yehova.’ ” Tofauti na wale wenye waliuliza Yesu kuhusu kulipa kodi, Jeffery alijifunza kutendea Wakristo wenzake na watu wengine bila kuwa na makusudi mabaya.

Mamilioni ya Mashahidi wa Yehova katika dunia yote wanajikaza kutumikisha mambo yenye wamejifunza katika Biblia. Wanafanya bidii nyingi ili ‘kuvaa utu mupya ulioumbwa kulingana na mapenzi ya Mungu katika uadilifu wa kweli na ushikamanifu.’ (Waefeso 4:24) Tunakutia moyo utafute kujua Mashahidi wa Yehova ni nani, mambo wanaamini, na namna wanaweza kukusaidia kujifunza juu ya dunia mupya yenye Mungu ameahidi. Katika dunia hiyo, “uadilifu utakaa” na hakutakuwa tena unafiki.—2 Petro 3:13.

Wakristo wa kweli wanaonyesha “upendo kutokana na moyo safi na kutokana na zamiri njema na kutokana na imani bila unafiki.”—1 TIMOTHEO 1:5