Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Ilitabiri Nini juu ya Matetemeko Makubwa ya Inchi?

Biblia Ilitabiri Nini juu ya Matetemeko Makubwa ya Inchi?

 Matetemeko ya inchi ya mingi inatokea kila mwaka. Ya mingi ni ya kidogo-kidogo, lakini matetemeko makubwa ya inchi inaharibisha vitu mingi, inaleta mateso, na kuua watu. Matetemeko ya inchi inaleta pia tsunami yenye inaharibishaka sehemu za pembeni-pembeni za bahari na kuua watu wengi. Biblia ilitabiri kama kungekuwa hii matetemeko ya inchi?

Mu hii habari

 Biblia ilitabiri kama kungekuwa matetemeko ya inchi?

 Biblia inazungumuzia unabii wenye Yesu alisema juu ya matetemeko ya inchi. Acha tusome maneno yake mu vitabu tatu vya Biblia:

 “Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, na kutakuwa upungufu wa chakula na matetemeko ya inchi mahali pamoja kisha pengine.”​—Matayo 24:7.

 “Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa matetemeko ya inchi mahali pamoja kisha pengine; pia kutakuwa upungufu wa chakula.”​—Marko 13:8.

 “Kutakuwa matetemeko makubwa ya inchi, na mahali pamoja kisha pengine kutakuwa upungufu wa chakula na magonjwa ya kuambukiza.”​—Luka 21:11.

 Yesu alitangulia kusema kama “matetemeko makubwa ya inchi” ingetokea “mahali pamoja kisha pengine,” na ileile wakati vita, upungufu wa chakula, na magonjwa ya kuambukiza ingetokea pia. Wakati ile mambo yote ingetokea, ile ingeonyesha kama tuko tunaishi mu “umalizio wa mupangilio wa mambo” ao mu “siku za mwisho.” (Matayo 24:3; 2 Timoteo 3:1) Wakati tunachunguza muzuri mambo yenye Biblia inasema, tunaona kama “siku za mwisho” zilianza mu 1914 na haziyaisha bado.

 Matetemeko ya inchi yenye kutokea leo inatimiza unabii wa Biblia?

 Ndiyo. Unabii wa Yesu na mambo yenye alisema juu ya matetemeko ya inchi, inapatana kabisa na mambo yenye tuko naona leo. Tangu mwaka wa 1914, kulishatokea matetemeko makubwa ya inchi zaidi ya 1950, yenye iliua watu zaidi ya millioni mbili. a Ona mifano kidogo tu:

 2004​—Bahari ya India. Tetemeko ya inchi ya ukubwa wa 9.1 ilileta tsunami yenye ilifika mu inchi 12 na yenye iliua watu 225 000 hivi.

 2008​—China. Tetemeko ya inchi ya ukubwa wa 7.9 iliharibisha vijiji na miji, na inasemekana kama iliua watu 90 000 na kuumiza wengine 375 000 hivi, na kuacha mamilioni ya watu bila nyumba.

 2010​—Haiti. Tetemeko ya inchi ya ukubwa wa 7.0 yenye ilifuatiwa na matetemeko ingine ya kidogo-kidogo iliua watu zaidi ya 300 000 na kuacha zaidi ya watu milioni moya bila nyumba.

 2011​—Japani. Tetemeko ya inchi ya ukubwa wa 9.0 na tsunami yenye ilitokea iliua watu 18 500 hivi na kufanya watu wengine wengi wahamie fasi zingine. Wakati kituo fulani ya courant yenye kuitwa Fukushima iliharibika, ile ilifanya kukuwe askida kubwa ya nyuklia. Hata kisha miaka kumi, watu 40 000 hawakuweza kurudia kwao karibu na ile kituo juu ya kuogopa wasipumue hewa yenye sumu yenye ilikuwa ile fasi.

 Unabii wa Biblia juu ya matetemeko ya inchi uko na maana gani kwetu?

 Unabii wa Biblia juu ya matetemeko ya inchi inatuonyesha nini itatokea wakati wenye kuya. Yesu alisema: “Wakati mutaona mambo hayo yanatokea, mujue kwamba Ufalme wa Mungu unakaribia.”​—Luka 21:31.

 Biblia inafasiria kama Ufalme wa Mungu ni serikali ya kweli yenye iko mbinguni na Mufalme wake ni Yesu. Na ni ile Ufalme njo Yesu alifundishaka wanafunzi wake wasali juu ikuye.​—Matayo 6:10.

 Wakati wenye Ufalme wa Mungu utatawala ku dunia, Mungu atazuia misiba ya asili na hata matetemeko ya inchi juu isiletee tena watu mambo ya mubaya. (Isaya 32:18) Zaidi ya ile, atatosha maumivu yote ya kimwili na ya kiakili yenye matetemeko ya inchi inaleta leo. (Isaya 65:17; Ufunuo 21:3, 4) Juu upate maelezo zaidi, soma habari yenye kichwa “Ufalme wa Mungu Utatimiza Nini?

a Zile hesabu zinatoka ku Global Significant Earthquake Database yenye kusimamiwa na United States National Geophysical Data Center.