WIMBO 10
Tumusifu Yehova Mungu Wetu!
-
1. Tusifu! Yehova Mungu!
Tutukuze jina yake!
Tangaza, fundisha kama
Siku yake iko karibu.
Sasa Mungu alishaweka Yesu
Ku kiti ya Ufalme.
Twende tuambie watu wote
Baraka zote za Mungu!
(REFREE)
Tusifu! Yehova Mungu!
Tutangaze ukubwa wake!
-
2. Tuimbe! na kumusifu!
Kwa sauti ya furaha!
Tukuwe wenye bidii
Na tutangaze sifa zake.
Ni mukubwa sana lakini ni mwema
Na munyenyekevu.
Anatuhangaikia sana
Na kujibu sala zetu.
(REFREE)
Tusifu! Yehova Mungu!
Tutangaze ukubwa wake!
(Ona pia Zb. 89:27; 105:1; Yer. 33:11.)