Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Kuna Tofauti Gani?

Je, unaweza kutambua tofauti kati ya picha A na picha B? Andika majibu yako kwenye mistari iliyo hapo chini, na ukamilishe picha hizo kwa kuzipaka rangi.

DOKEZO: Soma Kutoka 25:10-22.

1. ․․․․․

2. ․․․․․

3. ․․․․․

4. Ni picha gani iliyo sahihi, picha A au picha B?

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Sanduku la agano liliwakilisha nini kwa Waisraeli?

DOKEZO: Soma Kutoka 25:22; Mambo ya Walawi 16:2.

Ni jambo gani lililokuwa la maana kuliko kuwa na Sanduku la Agano?

DOKEZO: Soma Yoshua 7:1-6, 11, 12.

Ili uwapendeze wazazi wako na Yehova kwa nini ni muhimu kutii?

DOKEZO: Soma 1 Samweli 15:22, 23; Waefeso 6:1-3.

UTENDAJI WA FAMILIA:

Kila mtu katika familia afanye utafiti kuhusu sanduku la agano. Kisha mkutane na kueleza mambo mliyojifunza. Kwa mfano, ni vitu gani vilivyowekwa kwenye Sanduku hilo? Choreni vitu hivyo na mzungumzie umuhimu wake.

DOKEZO: Soma Waebrania 9:4.

Sanduku hilo lilipaswa kubebwa jinsi gani? Ni nini kilichotukia Daudi alipokosa kutii maagizo ya Yehova ya kubeba Sanduku?

DOKEZO: Soma Kutoka 37:5; 1 Mambo ya Nyakati 13:7, 9-14; 15:12-15.

Kusanya na Ujifunze

Kata, kunja katikati, na uhifadhi

KADI YA BIBLIA 6 ABELI

MASWALI

A. Ni nani aliyemuua Abeli?

B. Yehova alikuwa na mtazamo gani kumwelekea Abeli na dhabihu yake?

C. Jaza mapengo. Abeli alifanya kazi ya ________.

[Chati]

4026 K.W.K. 1 W.K. 98 W.K.

Adamu aumbwa Aliishi miaka Kitabu cha

ya 3900 K.W.K. mwisho cha Biblia

kinaandikwa

[Ramani]

Aliishi nje ya bustani ya Edeni

Bustani ya Edeni?

ABELI

MAMBO MACHACHE KUMHUSU

Mwana wa pili wa Adamu na Hawa na anatajwa kuwa mtu wa kwanza mwenye imani katika Biblia. Abeli alionyesha kwamba alitaka kupata kibali cha Mungu kwa kutoa dhabihu iliyokubalika. Ingawa Biblia haionyeshi maneno yoyote ambayo Abeli alisema, anatuwekea kielelezo cha kufuata kupitia mfano na imani yake.—Mwanzo 4:1-11; Waebrania 11:4.

MAJIBU

A. Ndugu yake, Kaini.—1 Yohana 3:11, 12.

B. “Kwa kibali.”—Mwanzo 4:4.

C. Kuchunga kondoo.—Mwanzo 4:2.

Watu na Nchi

5. Majina yetu ni Dean na Jennifer, na tuna umri wa miaka 10 na 7. Tunaishi nchini Australia. Kuna Mashahidi wangapi wa Yehova nchini Australia? Ni 36,400, 63,400, au 93,400?

6. Ni alama gani inayoonyesha eneo tunaloishi? Chora duara kuzunguka alama hiyo, na uchore alama nyingine kuonyesha eneo unaloishi kisha uone kwenu ni umbali gani kutoka Australia.

A

B

C

D

Watoto Watafute Picha

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

● Majibu ya “MAZUNGUMZO YA FAMILIA” yanapatikana kwenye ukurasa wa 15

MAJIBU YA UKURASA WA 30 NA 31

1. Pete na miti inakosekana.

2. Makerubi wanapaswa kunyoosha mabawa yao juu ya kifuniko.

3. Nyuso za makerubi zinapaswa kuwa zimeelekezwa juu ya kifuniko.

4. B.

5. 63,400.

6. C.