Hamia kwenye habari

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Huwatembelea Watu Walio na Dini Zao?

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Huwatembelea Watu Walio na Dini Zao?

 Tumegundua kwamba watu wengi ambao tayari ni wafuasi wa dini wanapenda sana kuzungumzia habari za Biblia. Bila shaka, tunaheshimu haki ya mtu ya kuwa na imani tofauti na yetu, nasi hatuwalazimishi watu wakubali ujumbe wetu. Tunapozungumza kuhusu dini, tunajaribu kufuata ushauri wa Biblia unaotaka tufanye hivyo kwa “tabia-pole” na tumwonyeshe mtu yule mwingine “heshima kubwa.” (1 Petro 3:15) Tunatazamia kwamba watu fulani watakataa ujumbe tunaowaletea. (Mathayo 10:14) Hata hivyo, hatuwezi kujua ikiwa wataukubali au wataukataa mpaka kwanza tuzungumze nao. Pia tunatambua kwamba hali za watu hubadilika. Kwa mfano, mtu anaweza kuwa na shughuli nyingi siku moja asiweze kuzungumza lakini anaweza kuwa tayari kuzungumza nasi wakati mwingine. Na watu hukabili matatizo au hali tofauti ambazo lazima washughulike nazo, na hilo huwachochea wapendezwe na ujumbe wa Biblia. Kwa hiyo, tunajitahidi kuzungumza na watu zaidi ya mara moja.