Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Muzunguko wa Maisha ya Nyenje

Muzunguko wa Maisha ya Nyenje

NYENJE ni kidudu mwenye kufanana nzige, na anaishi katika kontinenti zote isipokuwa tu Antarktiki. Lakini, nyenje wenye kuishi kaskazini-mashariki mwa Amerika ni wa pekee. Nyenje hao wanatokea kisha kipindi fulani, na wameshangaza wanasayansi wa biolojia kwa miaka mingi.

Fikiria jambo hili: Mamilioni ya nyenje hao wanatokea bila watu kuwazia kwa majuma kidogo tu katika kipindi cha kuchipuka kwa majani. Wakati mufupi wenye wanafanya kwenye jua, wanatosha ngozi yao ya utoto, wanafanya makelele mengi, wanaruka, wanazaa, na kisha wanakufa. Jambo la kushangaza ni kwamba, kisha nyenje hao kufa, watoto wao wanatokea kisha miaka 13 ao 17, kulingana na aina yao. Ni nini inapata vidudu hao mbele ya miaka hiyo?

Ili kupata jibu, tunapaswa kuelewa muzunguko wa pekee wa maisha ya nyenje. Juma moja hivi kisha kutokea, vidudu hao wakubwa wanakutana ili kuzaa, na vidudu wa kike wanataga mayai kati ya 400 na 600 ndani ya matawi ya miti. Kisha, vidudu hao wakubwa wanakufa. Katika majuma fulani yenye kufuata, mayai yao yanapasuka na watoto wanatoka na kuangukia chini. Kisha, wanaingia ndani ya udongo kwenye wanakunywa maji ya mizizi ya miti kwa miaka mingi. Miaka 13 ao 17 kisha hapo, kizazi kipya cha nyenje wenye kukomaa kinatokea na kurudilia muzunguko wa maisha.

Kulingana na habari moja ya gazeti Nature, muzunguko wa ajabu wa maisha ya nyenje “umeshangaza sana wanasayansi kwa miaka mingi. . . . Hata leo, wanasayansi wa mambo ya vidudu wanajaribu kuelewa namna muzunguko wa maisha ya vidudu hao ulifanya mageuzi.” Hilo ni jambo lenye kuwa nguvu sana kuelewa juu ya wanyama.

Unawaza namna gani? Muzunguko wa maisha ya nyenje ulijitokeza wenyewe? Ao uliumbwa?