Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | VIJANA

Wakati Kunakuwa Mabadiliko Katika Maisha

Wakati Kunakuwa Mabadiliko Katika Maisha

MAGUMU

  • Kazi ya baba yako inalazimisha familia yenu ihame.

  • Rafiki yako mwenye unapenda sana anahamia mbali.

  • Ndugu yako mukubwa anaondoka nyumbani wakati anaoa ao dada yako mukubwa anaondoka nyumbani wakati anaolewa.

Unaweza kufanya nini wakati mabadiliko kama hayo yanatokea?

Muti wenye unaweza kukunjama bila magumu, unaweza kuendelea kusimama hata kama kunatokea upepo mukali. Kama muti huo, unaweza kujifunza “kukunjama,” ni kusema, kujua namna ya kufanya wakati mabadiliko yenye hauwezi kuzuia kabisa ao kuepuka yanatokea katika maisha. Mbele tuzungumuzie namna gani tunaweza kufanya hivyo, tuone mambo fulani yenye unapaswa kujua juu ya mabadiliko.

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Hauwezi kuepuka mabadiliko. Biblia inaonyesha jambo hili la kweli kabisa juu ya wanadamu: ‘Tukio lisilotazamiwa [ao, lenye hatuwazie] linawapata wote.’ (Mhubiri 9:11) Leo ao kesho, utaona kuwa maneno hayo ni ya kweli. Lakini, kila tukio lenye halitazamiwe haliko la mubaya. Tena, mabadiliko fulani yenye kuonekana leo kuwa ya mubaya yanaweza kuwa yenye faida kisha wakati fulani. Lakini, watu wengi wanafurahia kufanya mambo yenye wamezoea kufanya; kwa hiyo mabadiliko, yakuwe ya mazuri ao ya mubaya, yanafanya wajisikie mubaya.

Mabadiliko yanaweza kuhangaisha zaidi sana vijana. Sababu gani? Kijana mumoja mwenye kuitwa Alex * anasema hivi: “Tayari unapambana na mabadiliko ya ndani. Mabadiliko ya inje yanaongeza tu mahangaiko.”

Sababu ingine ni hii: Wakati mabadiliko yanawafikia, watu wakubwa wanaweza kuchunguza mambo mengi yenye yamekwisha kuwafikia ili kuona namna walifanya zamani. Lakini, ni mambo kidogo tu ndiyo yawekwisha kufikia vijana.

Unaweza kujipatanisha na hali. Kujipatanisha na hali ni uwezo wa kurudilia haraka hali ya kawaida kisha kupata hali fulani ya mubaya ao mabadiliko fulani. Mutu mwenye kujua kujipatanisha na hali havumilie tu hali ya mupya, lakini pia anaweza kuona namna hali fulani yenye kuonekana kuwa kizuizi inaweza kumuletea faida. Vijana wenye kujua kujipatanisha na hali hawakimbilie kutumia pombe ao dawa za kulewesha wakati wanapata mahangaiko mengi.

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Ukubali mabadiliko. Ni kweli ungetaka kuongoza maisha yako yote, lakini jambo hilo haliwezekane. Marafiki wataoa ao kuolewa, ao watahama; ndugu ao dada zako watakomaa na kuondoka nyumbani; hali fulani zinaweza kulazimisha familia yenu ihame, na kufanya uache marafiki na mambo unazoea. Ni muzuri kukubali mabadiliko kuliko kuacha mawazo mabaya yakuhangaishe sana.—Kanuni ya Biblia: Mhubiri 7:10.

Ukaze akili yako juu ya mambo yenye kuwa mbele. Kukaza akili juu ya mambo ya zamani ni kama kuangalia sana kioo cha motokari yako wakati unatembeza motokari kwenye barabara kubwa. Ni muzuri kuangalia katika kioo wakati fulani, lakini unapaswa kabisa kukaza akili yako kwenye barabara kwa kuangalia mbele. Ni hivyo pia wakati unapambana na mabadiliko. Ujikaze kukaza akili yako juu ya mambo yenye kuwa mbele. (Methali 4:25) Kwa mufano, unapanga kufanya nini mwezi kesho, ao miezi sita yenye kuja?

Ukaze akili yako juu ya mambo mazuri. Mwanamuke mumoja mwenye kuitwa Laura anasema hivi: “Kujipatanisha na hali kunategemea namna unaona mambo. Utafute mambo mazuri katika hali yako ya sasa.” Unaweza kuandika faida moja ao zaidi yenye hali yako ya sasa inakuletea?—Kanuni ya Biblia: Mhubiri 6:9.

Mwanamuke kijana mwenye kuitwa Victoria anakumbuka kwamba wakati alikuwa hajaeneza miaka 19, marafiki wake wote wa sana walihamia mbali. Anasema hivi: “Nilijisikia kuwa peke yangu, na nilipenda mambo yote yaendelee kuwa kama zamani. Wakati ninakumbuka mambo hayo, ninatambua kwamba ni wakati huo ndio nilianza kuwa mutu muzima. Nilifikia kutambua kama mutu anapaswa kufanya mabadiliko ili akomae. Tena, ni wakati huo ndio nilianza kuona kama iliwezekana kupata marafiki wengine wenye walikuwa karibu na mimi.”—Kanuni ya Biblia: Methali 27:10.

Kukaza akili juu ya mambo ya zamani ni kama kuangalia sana kioo cha motokari yako wakati unatembeza motokari kwenye barabara kubwa

Uwasaidie wengine. Biblia inasema hivi: ‘Muangalie, si faida za kibinafsi za mambo yenu wenyewe tu, bali pia faida za kibinafsi za wengine.’ (Wafilipi 2:4) Dawa ya muzuri ya kumaliza magumu yako ni kusaidia wengine kumaliza magumu yao. Anna, mwenye kuwa na miaka 17, anasema hivi: “Wakati nilikuwa ninakomaa, nilifikia kutambua kama kusaidia mutu mwenye kuwa na magumu kama yangu, ao yenye kupita yangu, kuliniletea faida!”

^ fu. 11 Majina fulani yamebadilishwa katika habari hii.