Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | NAMNA YA KUWA NA UWEZO JUU YA TABIA ZAKO

3 Usichoke

3 Usichoke

Kulingana na wazo moja lenye kujulikana sana, inaomba siku 21 ili mutu azoee kabisa tabia mupya. Lakini, uchunguzi umeonyesha kwamba watu fulani wanafanya muda kidogo tu ili kufanya mabadiliko makubwa, na wengine muda murefu. Hilo linapaswa kukuvunja moyo?

Fikiria hali hii: Wazia unapenda kuwa na tabia ya kufanya mazoezi ya mwili mara tatu kila juma.

  • Juma la kwanza, unatimiza mupango wako wa kufanya mazoezi ya mwili mara tatu.

  • Juma la pili, unafanya mazoezi ya mwili mara mbili tu.

  • Juma la tatu, unafanya tena mazoezi ya mwili mara tatu.

  • Juma la ine, unajikaza kufanya mazoezi ya mwili mara moja tu.

  • Juma la tano, unatimiza tena mupango wako wa kufanya mazoezi ya mwili mara tatu, na kuanzia hapo unaendelea kufanya mazoezi mara tatu kila juma.

Ilikuomba juma tano ili ufikie kuzoea tabia mupya. Pengine utaona kuwa ni muda murefu, lakini wakati utafikia mupango wako, utafurahi kwa sababu umekuwa na tabia mupya ya muzuri.

KANUNI YA BIBLIA: “Kwa maana huenda mwadilifu akaanguka hata mara saba, naye hakika atasimama.”Methali 24:16.

Biblia inatutia moyo tusichoke. Mutu anaweza kuanguka tena na tena. Lakini, jambo la maana zaidi ni kusimama kila mara wakati anaanguka.

Mutu anaweza kuanguka tena na tena. Lakini, jambo la maana zaidi ni kusimama tena kila mara wakati anaanguka

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

  • Usiseme mara moja kwamba umeshindwa kabisa kwa sababu tu umefanya tena jambo lenye uliamua kuacha. Ujue kama ili kutimiza mupango wako utapata magumu fulani.

  • Ukaze akili juu ya wakati wenye mambo yalikuendea muzuri. Kwa mufano, kama unapenda ukuwe na tabia ya kuzungumuza muzuri na watoto wako, ujiulize hivi: ‘Ni wakati gani kwa mara ya mwisho nilitaka kufokea watoto wangu, lakini sikufanya hivyo? Kuliko kuwafokea nilifanya nini? Namna gani ninaweza kufanya hivyo tena?’ Maulizo kama hayo yanaweza kukusaidia ukaze akili juu ya mambo yenye ulifanya muzuri kuliko kukaza akili juu ya mambo yenye haukuweza kufanya.

Unapenda kujua namna kanuni za Biblia zinaweza kukusaidia katika hali zingine za maisha, kama vile kupambana na mahangaiko, kuwa na familia yenye furaha, na kupata furaha ya kweli? Zungumuza na Mashahidi wa Yehova, ao fungua adresi yetu ya Internete, jw.org.