Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | UKO NA NGUVU YA KUVUMILIA MAGUMU YA MAISHA?

Tatizo: Unajisikia Mubaya Moyoni

Tatizo: Unajisikia Mubaya Moyoni

MARA nyingi unajisikia mubaya moyoni, pengine unasikia huzuni, hasira, ao kinyongo? Ikiwa ni hivyo, unaweza kukosa wakati ao nguvu ya kufanya mambo ya lazima kabisa kwako. Unaweza kufanya nini juu ya jambo hilo? *

MUFANO WA BIBLIA: DAUDI

Mara nyingi Mufalme Daudi alijisikia mubaya moyoni. Kwa mufano, alikuwa na mahangaiko na huzuni. Ni nini ilimusaidia aendelee kuwa na nguvu? Daudi aliacha mambo katika mikono ya Mungu. (1 Samweli 24:12, 15) Tena, aliandika namna alikuwa anajisikia moyoni. Na kwa sababu alikuwa mwanaume mwenye imani, alisali mara kwa mara. *

MAMBO GREGORY ANAFANYA

Kama vile tuliona katika habari ya kwanza, Gregory anateswa na ugonjwa wa kuwa na mahangaiko mengi sana. Anasema hivi: “Mahangaiko yangu yalikuwa mengi sana na sikukuwa na nguvu ya kuyazuia.” Namna gani Gregory alipata tena nguvu? Anasema hivi: “Ili kupata tena nguvu, niliitika musaada wenye bibi yangu na marafiki wangu walinitolea kwa upendo. Pia, niliongea na muganga, na nilijifunza mambo mengi juu ya ugonjwa wangu. Nilibadilisha mambo fulani katika maisha yangu, kisha nilianza kujisikia kuwa niko na nguvu ya kupambana na ugonjwa wangu, na kwamba haukukuwa na nguvu kunipita. Hata kama wakati fulani ninakuwa na mahangaiko, sasa ninajua ni mambo gani yananiletea mahangaiko hayo, na ninajua mambo ya kufanya ili nijisikie muzuri.”

“Moyo wenye shangwe ni dawa nzuri.” —Methali 17:22

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Ikiwa unateseka kwa sababu ya kujisikia mubaya moyoni, upime kufanya hivi:

  • Uandike nafasi fulani namna unajisikia moyoni.

  • Uelezee mutu wa jamaa ao rafiki fulani namna unajisikia moyoni.

  • Usiitike haraka kuwa uko na haki ya kujisikia namna unajisikia moyoni. Kwa mufano ujiulize, ‘Kuna mambo yenye kuhakikisha kabisa kuwa niko na haki ya kujisikia hivi?’

  • Usiendelee kuwa na mahangaiko, hasira, ao kinyongo. Lakini, utumie nguvu zako ili kufanya jambo fulani lenye faida zaidi. *

Jambo la Maana: Mara nyingi haiko hali zetu ndizo zinatufanya tujisikie mubaya moyoni, lakini ni namna tunaona hali hizo.

^ fu. 3 Wakati fulani mutu anaweza kujisikia mubaya moyoni kwa sababu ya tatizo fulani la afya lenye linaweza kuomba aone muganga. Gazeti Amuka! halipendekeze matunzo yoyote. Mbele ya kufanya uamuzi wa kipekee, kila mutu anapaswa kuchunguza kwa uangalifu ni matunzo gani atakubali.

^ fu. 5 Zaburi nyingi zenye kuwa katika Biblia ni sala za Daudi zenye aliandika.

^ fu. 13 Ili kupata habari zingine, soma habari kubwa yenye kichwa “Namna ya Kupiganisha Mahangaiko,” katika gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 7, 2015.