Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Walijitoa kwa Kujipendea​—Katika Afrika Mangaribi

Walijitoa kwa Kujipendea​—Katika Afrika Mangaribi

ALIPOKUWA akikomalia katika maeneo yenye umasikini ya Côte d’Ivoire, Pascal alitamani sana kuwa na maisha mazuri. Kwa kuwa alipenda sana muchezo wa kupigana kwa ngumi, kila mara alijiuliza, ‘Ninaweza kuenda wapi ili niwe mupiganaji wa ngumi mwenye kujulikana?’ Alipokuwa na miaka zaidi ya 20, alifikiri kwamba ilifaa aende Ulaya. Lakini kwa kuwa hakuwa na vikaratasi vya kumuruhusu kusafiri, alitaka kuingia Ulaya kwa uficho.

Katika mwaka wa 1998, akiwa na miaka 27, Pascal alianza safari. Alivuka mipaka na kuingia huko Ghana, alipita katika inchi ya Togo na katika Benini (Benin), na mwishowe alifika katika muji wa Birni Nkonni huko Nijeri. Sasa alifika mahali ambapo kulikuwa hatari kabisa. Ili kuenda kaskazini, alipaswa kuchukua motokari na kuvuka Jangwa la Sahara. Baadaye, kisha kufika kwenye Bahari ya Mediterania, alipaswa kuchukua mashua ili kuenda Ulaya. Hiyo ndio ilikuwa mipango yake, lakini kulitokea mambo mawili huko Nijeri yaliyosimamisha safari yake.

Kwanza, feza zake zilimalizika. Pili, alikutana na Noé, painia mumoja, aliyeanza kujifunza naye Biblia. Mambo aliyojifunza yalimugusa sana na yalibadili maoni yake kuhusu maisha. Aliacha miradi yake ya kimwili na akaanza kufuatia miradi ya kiroho. Katika Mwezi wa 12, 1999, Pascal alibatizwa. Ili kuonyesha shukrani yake kwa Yehova, Pascal alianza kazi ya upainia katika mwaka wa 2001 huko Nijeri​—katika muji ambamo alikuwa amejifunza kweli. Namna gani anaona utumishi wake? Anasema hivi: “Maisha yangu ni yenye maana sasa!”

FURAHA YA KUTUMIKIA MAHALI AMBAPO KUNA UHITAJI KATIKA AFRIKA

(2) Anne-Rakel

Kama Pascal, wengi wamevumbua kwamba siri ya kuwa na maisha yenye maana kabisa ni kufuatia miradi ya kiroho. Ili kufikia miradi hiyo, ndugu na dada fulani wametoka Ulaya na kuhamia Afrika ili kutumikia katika maeneo yenye uhitaji mukubwa wa wahubiri. Kwa mufano, Mashahidi 65 hivi wa Ulaya​—walio kati ya miaka 17 na 70—​wamehamia katika inchi za Afrika Mangaribi, ni kusema Benini, Bukinafaso, Nijeri, na Togo. * Ni nini iliwachochea kuchukua uamuzi huo muzito, na walipata matokeo gani?

Dada Anne-Rakel wa Denmaki anasema hivi: “Wazazi wangu walikuwa wamisionere huko Senegali. Kila mara walizungumuzia kwa furaha namna walivyokuwa wamisionere. Hilo lilinifanya nitamani kuwa misionere siku moja.” Miaka 15 iliyopita, wakati dada Anne-Rakel alikuwa na miaka 20 hivi, alihamia Togo ambako anatumikia katika kutaniko la luga ya ishara. Je, kuhama kwake kuliwatia wengine moyo? Anasema hivi: “Baadaye dada yangu mudogo na kaka yangu mudogo walihamia pia Togo.”

(1) Albert-Fayette na Aurele

Ndugu Aurele wa Ufaransa aliye na miaka 70 na aliye na bibi, anasema hivi: “Nilipoacha kazi miaka mitano iliyopita kwa sababu ya uzee, mawazo yangu yalikuwa kuishi Ufaransa na kungojea Paradiso hapo ao kutafuta namna gani ninaweza kupanua utumishi wangu.” Ndugu Aurele alifanya mipango ili kupanua utumishi wake. Kisha miaka 3, yeye na bibi yake, Albert-Fayette, walihamia huko Benini. Ndugu Aurele anasema hivi: “Kuamua kuja kutumikia Yehova hapa ndilo jambo nzuri zaidi kuliko yote ambayo tumekwisha kufanya.” Kisha anaongezea hivi kwa furaha: “Baadaye, sehemu za eneo langu lililo pembeni ya bahari zilianza kunifanya nifikirie Paradiso.”

Kumepita miaka 16 tangu ndugu Clodomir na bibi yake anayeitwa Lysiane, waondoke Ufaransa na kuhamia Benini. Mwanzoni, walikumbuka sana ndugu, jamaa na marafiki wao wa Ufaransa, na walifikiri kwamba pengine hawatazoea maisha ya huko. Lakini, hawakuwa na sababu ya kuogopa. Walipata furaha nyingi. Ndugu Clodomir anasema hivi: “Kwa miaka hii 16, tumekuwa na pendeleo la kusaidia mutu mumoja kila mwaka akubali ukweli.”

(3) Lysiane na Clodomir pamoja na watu fulani ambao wamesaidia kujua kweli

(6) Johanna na Sébastien

Ndugu Sébastien na bibi yake anayeitwa Johanna, walitoka Ufaransa na kuhamia Benini katika mwaka wa 2010. Ndugu Sébastien anasema hivi: “Kuna mambo mengi sana ya kufanya katika kutaniko. Kutumikia hapa ni kama vile kupata mazoezi mengi ya kiteokrasi kwa muda mufupi!” Watu wanaitikia namna gani katika mahubiri? Dada Johanna anasema hivi: “Watu wana kiu ya kusikia ukweli. Hata ikiwa hatuko katika mahubiri, watu wanatusimamisha katika barabara na kutuuliza maulizo kuhusu Biblia na kutuomba vichapo.” Kuhama kumekuwa na matokeo gani juu ya ndoa yao? Ndugu Sébastien anasema hivi: “Ndoa yetu imekuwa nguvu. Ninafurahia kuhubiri siku nzima pamoja na bibi yangu.”

Ndugu Eric na bibi yake anayeitwa Katy, wanafanya upainia katika eneo lisilokuwa na wakaaji wengi la kaskazini mwa Benini. Walipokuwa wakiishi Ufaransa miaka kumi iliyopita, walianza kusoma habari kuhusu kutumikia mahali ambapo kuna uhitaji mukubwa wa wahubiri na walianza kuzungumuza na watumishi wa wakati wote. Kufanya hivyo kuliwasaidia wawe na tamaa ya kuhamia inchi nyingine, na walifanya hivyo katika mwaka wa 2005. Ongezeko ambalo walijionea liliwashangaza. Ndugu Eric anasema hivi: “Kwa miaka miwili, kikundi chetu kidogo cha muji wa Tanguiéta kilikuwa na wahubiri 9; sasa kuna wahubiri 30. Siku ya Yenga, watu kati ya 50 na 80 wanahuzuria mikutano. Ni furaha kubwa sana kujionea ongezeko hilo!”

(7) Katy na Eric

MATATIZO AMBAYO WAMEPAMBANA NAYO

(5) Benjamin

Wale wanaohamia katika maeneo yenye uhitaji mukubwa wa wahubiri wanapambana na matatizo gani? Kaka ya Anne-Rakel anayeitwa Benjamin, ana miaka 33. Alipokuwa Denmaki katika mwaka wa 2000, alikutana na misionere mumoja aliyekuwa akitumikia huko Togo. Ndugu Benjamin anakumbuka hivi: “Nilipomuambia misionere huyo kwamba nilitaka kuwa painia, aliniambia: ‘Unajua, unaweza kufanya upainia huko Togo.’” Ndugu Benjamin alifikiria jambo hilo. Anasema hivi: “Sikuwa hata na miaka 20 wakati huo, lakini dada zangu wawili walikuwa tayari wakitumikia huko Togo. Kwa hiyo ilikuwa rahisi kwangu kuenda Togo.” Baadaye alihama. Lakini kulikuwa shida moja. Ndugu Benjamin anaeleza hivi: “Sikujua hata neno moja la Kifaransa. Miezi sita ya kwanza haikuwa rahisi kwa sababu sikuweza kuongea kabisa na watu.” Lakini alifanya maendeleo baadaye. Sasa ndugu Benjamin anatumikia kwenye Beteli ya Benini, anasaidia kusafirisha vichapo na anatumika katika biro inayoshugulikia na mambo ya ordinatere.

(8) Marie-Agnès na Michel

Ndugu Eric na bibi yake Katy, ambao tulizungumuzia mbele, walitumikia katika eneo la luga ya kigeni huko Ufaransa mbele ya kuhamia Benini. Waliona tofauti gani huko Afrika Mangaribi? Dada Katy anasema: “Haikuwa rahisi kupata mahali pazuri pa kuishi. Kwa miezi mingi tuliishi katika nyumba isiyokuwa na umeme na maji.” Ndugu Eric anaongezea hivi: “Majirani walipiga muziki kwa sauti ya juu mupaka usiku sana. Ilifaa kuwa wavumilivu na kubadilika kulingana na hali.” Lakini, wote wawili wanasema hivi: “Furaha ya kutumikia katika eneo hili ambalo halijahubiriwa inashinda matatizo yote tunayopambana nayo.”

Ndugu Michel na bibi yake anayeitwa Marie-Agnès, walio na miaka zaidi ya 50, waliondoka Ufaransa na kuhamia Benini miaka mitano iliyopita. Mwanzoni, walikuwa na wasiwasi. Ndugu Michel anasema hivi: “Wengine walilinganisha safari yetu na mutu anayetembea juu ya kamba akisukuma ngorofani ao bruete​—na sisi ndio tuliketi katika ngorofani hiyo! Ulinganifu huo ungeweza kuogopesha ikiwa haungejua kwamba mutu huyo anayetembea juu ya kamba ni Yehova. Kwa hiyo, tulihama ili kumutumikia Yehova, naye alitutegemeza.”

NAMNA YA KUJITAYARISHA

Wale ambao wamekwisha kuhamia mahali ambapo kuna uhitaji wanaonyesha kwamba ni jambo la maana kujitayarisha kwa kufanya mambo yanayofuata: Panga mambo mbele ya wakati. Jifunze kubadilika kulingana na hali. Tumia vizuri feza zako. Mutegemee Yehova.​—Lu. 14:28-30.

Ndugu Sébastien, ambaye tulizungumuzia mbele, anaeleza hivi: “Mbele ya kuhama, mimi na Johanna tuliweka feza kwa miaka miwili kwa kupunguza feza tulizokuwa tunatumia kwa ajili ya viburudisho na kwa kuepuka kununua vitu ambavyo hatuhitaji.” Ili kuendelea kutumikia katika inchi nyingine, wanafanya kazi ya kimwili kwa miezi fulani kila mwaka huko Ulaya; hilo linawasaidia kufanya upainia kwa miezi mingine huko Benini.

(4) Marie-Thérèse

Dada Marie-Thérèse ni mumoja wa dada ambao hawajaolewa 20 ambao wametoka inchi zingine ili kutumikia huko Afrika Mangaribi. Alikuwa anafanya kazi ya kutembeza bisi huko Ufaransa; lakini, katika 2006 alichukua mapumuziko ya mwaka mumoja ili kufanya upainia huko Nijeri. Kisha muda kidogo, alitambua kwamba hiyo ndio maisha ambayo alitaka kuwa nayo. Dada Marie-Thérèse anasema hivi: “Kisha kurudi Ufaransa, nilimuambia bwana wangu wa kazi kwamba nilitaka kubadili programu yangu ya kazi, na alikubali. Kwa hiyo, kuanzia Mwezi wa 5 mupaka Mwezi wa 8, ninafanya kazi ya kutembeza bisi huko Ufaransa, na kuanzia Mwezi wa 9 mupaka Mwezi wa 4, ninafanya upainia huko Nijeri.”

(9) Saphira

Wale ‘wanaotafuta kwanza Ufalme’ wanapaswa kuwa hakika kwamba Yehova atawatolea ‘vitu vingine vyote vya lazima.’ (Mt. 6:33) Kwa mufano: Fikiria mambo ambayo Saphira, dada asiyeolewa wa Ufaransa aliye na miaka 20 hivi anayefanya upainia huko Benini, alijionea. Katika mwaka wa 2011 alirudi Ufaransa ili apate feza za kutosha ambazo zingemusaidia kwa mwaka mwingine (mwaka wake wa sita) katika Afrika. Dada Saphira anaeleza hivi: “Kazi yangu ingemalizika Siku ya Tano, lakini nilihitaji tena kufanya kazi siku kumi ili nipate feza za kutosha ambazo zingenisaidia mwaka uliofuata. Nilibaki tu na juma zingine mbili huko Ufaransa. Nilimuelezea Yehova shida yangu. Kisha muda mufupi, shirika moja la kutafutia watu kazi liliniita na kuniuliza ikiwa ninaweza kutumika pa nafasi ya mutu fulani kwa majuma mawili.” Dada Saphira alienda Siku ya Kwanza mahali pa kazi ili azoezwe na mutu ambaye angemuachia nafasi yake. Anaeleza hivi: “Nilishangaa sana nilipovumbua kwamba yule ambaye angenizoeza alikuwa dada Mukristo ambaye aliomba siku kumi ili aende kuhuzuria Masomo ya Mapainia! Bwana wake wa kazi alikataa kumupatia siku hizo mupaka angepata mutu ambaye angemugomboa. Alisali Yehova amusaidie​—kama vile mimi nilivyofanya.”

CHANZO CHA FURAHA YA KWELI

Ndugu na dada fulani wametumikia katika Afrika Mangaribi kwa miaka mingi na wamefanya eneo hilo kuwa makao yao. Wengine wamebaki huko kwa miaka fulani na baadaye wamerudi katika inchi yao. Lakini hata mupaka sasa, wale ambao wametumikia mahali ambapo kuna uhitaji mukubwa wa wahubiri wanaendelea kufaidika na miaka waliyopitisha katika inchi ya kigeni. Wamejifunza kwamba furaha ya kweli inatokana na kumutumikia Yehova.

^ Biro ya tawi ya Benini inasimamia kazi katika inchi hizo ine zinazotumia Kifaransa.